• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MWONEKANO WA MTU UNATEGEMEA MTU ANAKULA NINI.

Imewekwa: October 28th, 2024

Afisa lishe Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Simoni Mayala ametoa rai kwa wanafunzi kuzingatia masuala ya lishe kwani jinsi mtu anavyoonekana leo inategemea na vyakula ambavyo mtu anakula  hivyo  mtu kuwa na mwonekano mzuri na wenye afya anapaswa kuzingatia mlo kamili ukiambatana na makundi mbalimbali ya vyakula.

Kauli hiyo amezungumza leo Octoba 10/2024 wakati akitoa elimu kuhusu masuala ya lishe  ikiwa ni pamoja na kufundisha makundi mbalimbali ya chakula kwa Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makala iliyopo Kata ya Matundasi Wilaya ya Chunya.

“Niwaombe wanafunzi mzingatie sana masuala ya lishe kwani lishe ni muhimu sana kwenu ikiwemo protini kwani inaujenga mwili lakini hiyo hiyo protini ndani yake kuna mafuta ambayo yanatunza kumbukumbu na utengenezaji wa ubongo hivyo wazazi wakati mwingine wanaponunua maziwa tuwe tunakunywa ili akili iweze kuchangamka” . alisema Mayala

Aidha Afisa lishe ameelezea makundi mbalimbali ya vyakula kama vile nafaka , mizizi, vyakula jamii ya mikunde, wanyama ,mafuta , Mboga mboga na matunda  pamoja na umuhimu wake  ikiwa ni pamoja na kuulinda mwili dhidi ya magonjwa kuupa mwili nguvu na afya pamoja na mambo mengine mengi huku akisisitiza kujiepusha kula vyakula vyenye kemikali nyingi.

Naye Afisa elimu  Watu wazima  na Elimu  nje ya Mfumo maalumu  divisheni ya elimu Sekondari  Mwalimu Lukelo Mng’ongo amewataka wanafunzi kuyazingatia masuala ya lishe ambayo wamefundishwa lakini pia kwendelea kusoma kwa bidii Zaidi  huku akitoa rai kwa wanafunzi wa kidato cha nne  kwendelea kujiandaa vyema na mtihani wa taifa ulioko mbele yao.

Maadhimisho ya wiki ya lishe  yameambatana na utoaji elimu juu ya mambo mbalimbali kuhusiana na lishe kwa wanafunzi ili kuwawezesha kujua na kutambua umuhimu wa   lishe  na jinsi ya kuzingatia lishe bora kwa afya  zao  imeenda sambamba na kauli mbiu isemayo “Mchongo ni afya yako, Zingatia Unachokula”.

Afisa elimu  Watu wazima  na Elimu  nje ya Mfumo maalumu  divisheni ya elimu Sekondari  Mwalimu Lukelo Mng’ongo akitoa rai kwa wanafunzi kuongeza bidii  zaidi katika masomo yao ili waweze kufanya vizuri kwenye mitihani iliyoko mbele yao.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makala kata ya Matundasi  wakiendelea kufuatilia elimu ya Lishe   

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.