• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MWANGINDE AZINDUA SHULE YA SEKONDARI LUALAJE.

Imewekwa: January 21st, 2023

LUALAJE

MWENYEKITI wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe. Bosco Mwanginde amewataka wananchi wa wilaya ya Chunya kutunza, kulinda na kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ili idumu kwa muda mrefu na hatimaye kuwanufaisha watu wengine wengi.

Mhe. Mwanginde amesema hayo jana tarehe 20 January 2023 wakati alipoongoza hafla ya ufunguzi wa shule ya Sekondari Lualaje ambayo imejengwa kwa fedha kiasi cha Shilingi milioni 470 kutoka serikali kuu kwa lengo la kuendelea kusogeza huduma kwa wananchi wote bila kujali eneo analotoka

Aidha Mhe Mwanginde amewasisitizia wananchi wa lualaje kwamba Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan inawajali na inawatambua na ndio sababu inaendelea kuleta maendeleo mbalimbali ikiwepo ujenzi wa sekondari inayofunguliwa, miundombinu ya Barabara, vituo vya afya pamoja na miradi mbalimbali.

“Kuletwa kwa fedha katika kata hii ya Lualaje ni ishara tosha kwamba serikali inawajali, na inawathamini sana wananchi wake, na ufunguzi wa shule hii ni mwanzo kwani iko miradi mingine mingi serikali inaendelea kutekeleza katika maeneo yenu”

Katika kuhitimisha Hotuba yake katika hafla hiyo amewata wanafunzi, walimu na wazazi kwa pamoja kushirikiana ili kuhakikisha lengo la uwepo wa shule ya sekondari katika maeneo yao linatimia kwani kinyume na hapo itakuwa ni vigumu kupata matokeo chanya kwa wanafuniz na serikali kwa ujumla.

Pia Mhe Mwanginde amewaagiza watendaji wote kata na vijiji wilayani chunya kuanza kuchukua hatua mara moja kwa wazazi ambao bado hawaja wapeleka watoto shuleni na kuwataka kupeleka taarifa ofisini kwake mara moja.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamimu Kambona amewapongeza wananchi wa kata ya Lualaje kwa namna walivyoshiriki katika ujenzi wa shule hiyo ya sekondari na kuwataka kutunza, kulinda na kuhakikisha wanaendelea kushiriki katika miradi mingine mingi inayojengwa katika maeneo yao

Naye Afisa Elimu sekondari wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mwalimu Hamis Mapoto alitoa takwimu za wanafunzi waliopangwa katika shule hiyo ya Sekondari Lualaje ni wanafunzi 86, aidha ni wanafunzi 61 tu wamesharipoti shuleni hapo huku akisema tayari walimu saba wamepelekwa katika shule hiyo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya chunya Mhe. Bosco Mwanginde akikata utepe kuzindua majengo ya Shule ya Sekondari Lualaje.

Muonekano wa Majengo Katika Shule ya Sekondari Lualaje

Wanafunzi sambamba na wananchi mbalimbali waliojitokeza katika hafla ya Uzinduzi wa Shule ya Sekondari Lualaje

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona akizungumza katika hafla ya Uzinduzi wa Shule ya Sekondari Lualaje.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.