• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Mkuu wa Wilaya Chunya ataka usafi wa viwango

Imewekwa: March 2nd, 2022

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe. Mayeka Simon Mayeka amewataka Watendaji na Wataalam wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kutekeleza majukumu ya usimamizi wa usafi na mazingira.

Mhe. Mayeka ameitoa rai hiyo leo alipohudhuria semina ya Mafunzo ya Utekelezaji wa Usafi wa mazingira iliyoendeshwa na AMREF kwa Watendaji wa Kata, Vijiji na Wataalam wa Halmashauri katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri.

Mh. Mayeka alisema, suala la Usafi wa Mazingira ni jukumu la Serikali na kueleza kuwa, kama kuna washirika wanaosaidia jukumu hilo ni kwa sababu tu wameamua kusaidia.

“Usafi wa Mazingira ni suala la msingi la kwako, kama kuna taasisi au Shirika limekuja ni kutusaidia tu, mimi nilikuwa sioni kama ilikuwa sahihi AMREF waje kuhimiza ujenzi wa vyoo wakati kuna Mtendaji wa Kata, Kijiji na Afisa Tarafa”. Mh Mayeka alisema.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa, suala la ujenzi wa vyoo na usafi wa mazingira sio kazi ya AMREF bali ni kazi ya Serikali kuwahimiza wananchi kuwa na vyoo bora pamoja na usafi wa mazingira kiujulma.

"Niwashukuru sana AMREF kwa sababu hayo ni majukumu yetu, wanatusaidia lakini na sisi tunapaswa tuyachukue kama ya kwetu, tusiwaachie AMREF, isionekane ni majukumu yao." Alisema Mayeka.

"Kwenye Wilaya yetu suala la usafi wa mazingira kiukweli ni mbaya hali sio nzuri sana, mazingira yetu bado ni machafu hasa kwenye minada huko.

Aidha,Mhe. Mayeka amewataka viongozi hao kubadilika na kuanza kutimiza majukumu yao kiweledi kabla ya kusubiri msaada kutoka kwenye makampuni,mashirika au taasisi binafsi

“Mimi niwatake sasa baada ya mazungumzo ya leo mbadilike, nendeni mkafanye majukumu yenu, wala hakuna sababu ya kusubiria AMREF au mtu mwingine, hayo yapo ndani ya uwezo wenu, wewe upo Bitimanyanga mnada umeisha suala la usafi ni jukumu lenu kuhakikisha mnaacha mazingira yakiwa safi." Alisisitiza DC Mayeka.

Nae Mh. Alex Kinyamagoha Diwani wa Kata ya Itewe amesema, suala la usafi wa mazingiza kwa Wilaya ya Chunya bado lipo nyuma sana na mazingira mengi ni machafu.

“Binafsi nilipata bahati ya kutembea huko hasa tarafa ya kipembawe, hali ni mbaya, Chunya bado tuna kaya ambazo hazina vyoo.” Alisema Mhe. Kinyamagoha

"Wenzetu hawa wa AMREF wamekuja na suluhisho kwa wale wasioweza na wameshindwa kabisa, hawana vyanzo vya mapato, wamefanya muunganiko na watu wa Equit bank, wewe kama hauna fedha utakopeshwa na benki wao watakusimamia ufanye maendeleo, ujenge choo bora ili uepukane na maradhi ya mlipuko." Alisema Mhe. Kinyamagoha.

Watendaji wa Kata, Vijiji na Maafisa Elimu kata wakiwa katika Semina ya Mafunzo ya Utekelezaji wa Usafi na Mazingira iliyo endeshwa na AMREF kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mh Mayeka Simon MAyeka Akizungumza na Washiriki walioudhuria Mafunzo ya Utekelezaji wa Usafi wa Mazingira wilaya  ya Chunya iliyoendeshwa na AMREF

Afisa Afya Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bw. David Mwakasege Akiwasilisha mada kwenye Semina ya Utekelezaji wa Usafi wa Mazingira kwa Watendaji wa Kata,Vijiji pamoja na Maafisa Elimu kata waliohudhuria Semina hiyo iliyo ratibiwa na AMREF

Afisa Mradi wa AMREF Bi. Rebeca Magurusa Akielekeza jinsi ya Ujazwaji wa fomu mbalimbali za Majuimuisho ya Takwimu za Usafi wa Mazingira Ngazi ya Kata katika Kijiji kwa Watendaji wa Kata, Vijiji na Maofisa Elimu kata walio hudhuria Semina hiyo.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.