• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MKURUGENZI ATAJWA CHUNYA KUNG’ARA SHIMISEMITA DODOMA

Imewekwa: October 24th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Chunya imeendelea kung’ara katika mashindano ya SHIMISEMITA yanayoendelea jijini Dodoma kwa timu mbalimbali za watumishi kutoka Halmashauri zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku sababu kubwa ikitajwa kuwa namna Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuwa chachu kubwa ya Timu hiyo na hatimaye kesho kutupa karata yake dhidi ya Tanga Jiji kwa hatua ya kumi na sita bora


Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwa upande wa mpira wa Miguu imeingia hatua ya kumi na sita bora baada ya kushinda michezo miwili, kudroo mchezo mmoja na kupoteza mchezo mmoja dhidi ya wenyeji walima zabibu Dodoma Jiji hivyo kujikusanyika pointi saba nyuma ya Dodoma Jiji mwenye pointi 8,  wakati huo huo timu ya mpira wa mikono (Handball bado  iko hatua za makundi pamoja na Mpira wa pete (Netball) huku mchezo wa Riadha utaanza kesho


Akizungumza kwa njia ya simu kiongozi wa Msafara wa watumishi kutoka Halmashauri ya wilaya ya Chunya ambaye pia ndiye kocha wa timu ya mpira wa miguu Bwana Vicent Msolla amesema siri ya watumishi kujituma na kupambana ni kurudisha fadhira kwa Mkurugenzi jinsi anavyoishi na watumishi na hata kuridhia watumishi 35 kusafriri kwenda Dodoma kushiriki mashindano hayo kwani Halmashauri nyingine zimeshindwa na hata waliofanikiwa sio kwa idadi kubwa kama ilivyo Halmashauri ya wilaya ya Chunya


“Namna mwajiri anavyojitoa kwa watumishi, amekuwa ni chachu kubwa kwa hawa watu maana njia nzima wamekuwa wakimsema yeye tu na hata kuruhusu idadi kubwa ya watumishi kushiriki mashindano hayo maana ziko halmashauri zimeleta watu wawili au watatu


Pili mimi kama kiongozi wao nimewambia tunalo deni kubwa kwa halmashauri yetu hivyo lazima tuongeze bidii kuhakikisha tunafikia hatua ambayo ni nzuri

Kwaajili ya maandalizi ya hatua ya kumi na sita bora ambayo ni mtoano sisi tumekubaliana kwa pamoja kujitunza maana siri ya michezo ni kujitunza ili tufanye vizuri hatua ya kumi na sita bora maana timu zilizoingia ni bora kuliko hatua tulizovuka” Amesem Msolla


Naye Kapteni wa timu ya mpira wa Miguu ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bwana Mshigati amesema siri ya Mafanikio ni uongozi bora wenye kuwapenda watu anaouonesha Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya hivyo wachezaji wanaona hili ni deni la kulilipa kwa Halmashauri ya wilaya ya Chunya na namna pekee ya kulipa deni hilo ni kufanya vizuri kila hatua


“Kimsingi michezo hii ni ya watumishi hivyo sisi kama watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya tumejitoa kuipambania Halmashauri yetu, Wachezaji wana morali, kila mmoja anajitoa kwa jihadi kubwa na hatimaye tumevuka hatua ya makundi sasa tunaingia hatua ya mtoano.


Sababu kubwa kuliko zote ya sisi kufanya vizuri ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya maana kitendo cha Kuruhusu wachezaji na viongozi  35 kuja kushiriki michezo hii sio kitu kidogo maana naweza kusema Chunya inaweza kuwa Halmashauri ya kwanza kuja na wachezaji wengi lakini pia tumetoka na gari yetu kutoka Chunya, na gari hiyo tunayo hapa Dodoma inatuchukua maeneo ambayo tunakaa kutupeleka viwanjani na kuturudisha jambo ambalo hauwezi kuliona kwa halmashauri zingine kwa hivyo hilo kwetu ni deni ambalo tunahangaika kulilipa kwa kiongozi wetu” Alisema Mshigati Kempteni wa timu ya mpira wa Miguu


Naye kepteni wa timu ya kuvuta kamba kwa upande wa wanawake Bi Devotha Mwasaga amesema wao kama Mabingwa watetezi bado timu kutoka Chunya ina khali ya kuchukua Ubingwa tena, huku akisikitika Kukosa wachumba wakati wa Mashindano hayo kutokana na namna ambavyo wamewabuluza wapinzani katika mashindano ya Vuta kamba


“Sisi huku kila tukipita tunaambiwa watumishi wanawake kutoka Chunya tunaogopwa na sababu ni mchezo wa kuvuta kamba na sababu iko wazi kabisa tumekuja tukiwa na maokoto ya kututosha na katika hilo lazima tumshukuru kiongozi wetu kutuwezesha kwa kiwango kikubwa namna hii” alisema Bi Mwasaga


Adha Bi Mwasaga amesema upande wa mpira wa pete (Netball) timu ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya imetolewa kwenye michuano huku sababu zikitajwa zikiwemo Mamluki kwenye timu nyingi za Halmashauri jambo ambalo Halmashauri mojawapo kuondolewa kwenye Mashindo kwa kutumia Mamluki wengi (kuchukua watu wasio watumishi), pia timu yao kutokujua kanuni mpya za mpira huo imepelekea kuwa na makosa mengi sana wakati wa michezo yao jambo lililo gharimu timu ya halmashauri ya wilaya ya Chunya


Pia Bi Mwasaga amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji kwa namna alivyowawezesha kushiriki mashindano hayo pamoja na ushirikiano anaoendelea kuwapatia kwa kuwapo moya wakati wote na kwa kila hatua


Mashindano hayo yanahusisha michezo Mbalimbali kwa watumishi kutoka Halmashauri Mbalimbali huku Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikishiriki michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete, handball, kuvuta kamba, karata na mchezo wa bao

Badhi ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakijianda kwa mazoezi kwenye moja ya viwanja vinavyotumika kwa mashindano ya SHIMISEMITA jijini Dodoma

Timu ya kuvuta Kamba ikiongoza na kampeni Devota Mwasaga (Kusho kwa aliyevaa kofia) wakiwa kwenye picha ya pamoja

Timu ya Mpira wa Pete ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakiwa kwenye picha ya pamoja kwenye moja ya viwanja vinavyotumika kwa mashindano

Timu ya mpira wa miguu ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikiongozwa na Kocha Vicent Msola kushota kabla ya moja ya michezo yao hapo Jijini Dodoma

Timu ya mpira wa Miguu kabla ya Mchezo wao wakiwa wameshika Bendera ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuashiria wanaednelea kuiwakilisha vyema Halmashauri kwenye Mashindano hayo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.