• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MKAZINGATIE YOTE MTAKAYOFUNDISHWA KWAAJILI YA KUTEKELEZA MAJUKUMU YENU KIKAMILIFU.

Imewekwa: December 19th, 2024

Afisa Mwandikishaji jimbo la Uchaguzi Lupa wakili Athuman Bamba ametoa wito kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi za kata  kuzingatia yale yote watakayofundishwa  ili yakawasaidie kutekeleza majukumu yao  kikamilifu na kwa weledi mkubwa katika zoezi la Uboreshaji wa Daftari la kudumu la Mpiga kura .

Wito huo umetolewa leo Desemba 19 /12/2024 wakati  ufunguzi wa Mafunzo kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

“Ni muhimi mkazingatia yote mtakayofundishwa hapa, kwani Tume inatarajia  baada ya mafunzo haya  mtapaswa kutoa mafunzo haya kwa waendeshaji wa vifaa vya Bayometriki na Waandishi wasaidizi ambao watahusika na Uandikishaji wa wapiga kura kwenye daftari la kudumu la mpiga kura Vituoni “amesema  Wakili Bamba

Sambamaba na wito huo, amewataka  waandikishaji wasaidizi  ngazi ya kata wenye uzoefu kuwasaidia waandikishaji wasaidizi wenzenu  ambao hawajawahi kushiriki katika  zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la mpiga kura  ili waweze kutekeleza majukum yao kikamilifu na kwa weledi

 Aidha amewataka  Maafisa  waandikishaji wasaidizi ngazi  ya kata  kuvitunza vifaa vyote vya Uchaguzi vitakavyotumika   katikia Uboreshaji wa daftari la mpiga kura  ikiwa ni pamoja na kuzigatia maelekezo yote yatakayo tolewa na Tume  katika zoezi la Uandikishaji    ili muweze kuyafanyia kazi kwa usahihi  na ufanisi wakati wa zoezi litakapokuwa limeanza.

Mafunzo yaliyotolewa ni pamoja na namna ya  ujazaji wa fomu wa fomu mbalimbali zitakazotumika wakati wa uandikishaji ,namna ya  kutumia mfumo wa kuandikisha wapigakura(voters registration system VRS pamoja na matumizi sahihi ya vifaa vya uandikishaji wa wapiga kura. Mafunzo haya  yameenda sambamba na kuapishwa kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata .

Mafunzo kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata yanatolewa na Maafisa waandikishaji wa jimbo la Lupa kwa siku mbili tarehe 19 na Tarehe 20/12/2024 ikiwa ni maandalizi ya  uboreshaji wa dafteri la kudumu la mpiga kura kuelekea  Uchaguzi Mkuu  unaotarajiwa kufanyika mwaka 2025 , Mafunzo hayo yamehudhuriwa na Maafisa mbalimbali kutoka Tume ya Uchaguzi , Maafisa waandikishaji ngazi ya jimbo , Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Chunya, Afisa Uchaguzi Wilaya ya Chunya  na  Maafisa waandikishaji wasaidizi gazi ya Kata.

Afisa Mwandikishaji  jimbo la Lupa wakili Athumani Bamba akifungua Mafunzo kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri Jengo jipya la Utawala.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Chunya  Mhe.James Mhanusi akitoa maelekezo kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi  kabla ya kuwaapisha Maafisa Hao  wakati wa afunzo ya uboreshaji wa Daftari la kudumu la Mpiga kura .

Maafisa waandikishaji wasaidizi wakifuatilia somo la namna ya ujazaji wa fomu mbalimbali za uandikishaji wa wapigakura  yaliyofundishwa na  Afisa mwandikishaji wa Jimbo  la Lupa dkt Lukas Theodory katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri uliopo Jengo jipya la Utawala.

Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata wakila kiapo wakati wa Mafunzo ya uboreshaji Daftari la kudumu la Mpiga kura yaliyotolewa katika ukumbi wa Halmashauri Jengi jipya la Utawala 



Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.