• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MKATUMIE WELEDI WENU KUTEKELEZA JUKUMU MLILOKABIDHIWA.

Imewekwa: December 23rd, 2024

Afisa Mwandikishaji jimbo la Lupa  wakili Athuman Bamba amewataka Waandikishaji  wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki kuhakikisha wanatumia weledi na ubora uliowapa nafasi ya kuteuliwa na tume kutekeleza jukumu la uboreshaji wa    daftari la mpiga kura huku akiwahimiza kutumia vizuri na kuvitunza vifaa watakavyokabidhiwa kwaajili ya kazi.

Hayo ameyasema leo tarehe 23/12/2024 wakati akifungua mafunzo kwa Waandishi wasaidizi wa vituo na waendesha vifaa vya Bayometriki yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya (Sapanjo)

 “Ninatoa wito kwenu kuhakikisha mnatumia vizuri vifaa hivyo ,mnavitunza vifaa vyote vitakavyotumika katika uboreshaji wa daftari la  kudumu la Mpiga kura kwa kuzingatia maelekezo yatakayotolewa na tume kwani kwa kufanya hivyo mtafanya kazi kwa usahihi na kwa weledi wakati wa zoezi litakapokuwa limeanza”amesema Wakili Bamba.

Aidha wakili Bamba amewasisitiza waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya Bayometriki kuzingatia mafunzo yote yatakayofundishwa ili wakafanye kazi inayotarajiwa kwa weledi ,bidii moyo na kujituma pamoja na kutumia uzoefu wao kuwasaidia wenzao ambao hawana uzoefu  ili zoezi liweze kufanyika kwa usahihi na weledi mkubwa

Mafunzo yameenda sambamba na kuapishwa kwa Waandikishaji wasaidizi na waendesha Vifaa vya bayometriki  pamoja na kufundishwa mada mbalimbali  juu ya   namna bora ya ujazaji wa fomu mbalimbali zitakazotumika wakati wa uboreshaji wa daftari la kudumu la Mpiga kura, kutumia mfumo wa kuandikisha wapiga kura (voters registration system VRS) pamoja na matumizi sahihi ya  ya vifaa vya uandikishaji wa wapiga kura .

Mafunzo kwa waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya Bayometriki jimbo la Lupa yanatolewa na Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata kwa kusaidiana na Maafisa wa Tume kutoka Halmashauri na Makao makuu, Mafunzo hayo yatadumu   kwa siku mbili tarehe 23/12 na Tarehe 24/12/2024 ikiwa ni maandalizi ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la Mpiga kura litakaloanza tarehe 27/12/2024 na kuhitimishwa Tarehe 02/01/2025   ikiwa ni maandalizi kuelekea Uchaguzi Mkuu  unaotarajiwa kufanyika mwaka  Octoba 2025.

  “Kujiandikisha kwa Mpiga kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora”.

Afisa Mwandikishaji jimbo  la Lupa Wakili Athuman Bamba akizungumza na waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya Bayometriki wakati akifungua mafunzo katika Ukumbi wa Sapanjo wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Waandikishaji wasaidizi na Waendesha Vifaa vya Bayometriki wakiapa wakati wa Mafunzo ya Uboreshaji daftari lakudum la Mpiga kura  yaliyofanyika katika Ukumbi wa Sapanjo wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Afisa Mwandikishaji Msaidizi ngazi ya kata  ndugu Ntundu Chapa akifundisha namna ya ujazaji wa fomu  mbalimbali  wakati wa mafunzo kwa waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa jimbo la Lupa 

Waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya Bayometriki wakifuatilia mafunzo yanayoendelea kutolewa na Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata  katika Ukumbi wa Sapanjo wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.



Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.