• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MIICO yawapiga Msasa wakulima, wafugaji

Imewekwa: March 9th, 2022

MRADI wa kuendeleza haki na ulinzi wa ardhi kwa wazalishaji wadogo kwa uhakika wa chakula umefanya kikao cha wadau wa masuala ya ardhi Wilaya ya Chunya Machi 8, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Mradi huo unaoendeshwa na shirika la MIICO unatekelezwa katika mikoa mitatu ambayo ni Mbeya, Rukwa na Njombe ambapo kwa upande wa Mkoa wa Mbeya, mradi huo unafanyika Wilayani Chunya katika Kata za Sangambi na Upendo.

Akizungumza katika kikao hicho Mkurugenzi wa MIICO Bi. Catherine Mulanga amesema lengo la programu hiyo ni kuwawezesha wazalishaji wadogo hasa wakulima na wafugaji katika kuhakikisha wanapata ardhi bora kwa ajili ya uzalishaji.

“Tunalenga katika kuhakikisha wazalishaji wadogo wanaweza kupata ardhi, wamiliki kisheria, ni haki yao lakini kuhakikisha tunakuwa na uhakika wa chakula”. Alisema Bi. Catherine.

“Leo tumekuwa na kikao hiki ili kuwakutanisha wadau wa ardhi, sio wa Kata za Sangambi na Upendo peke yao, ila ni wadau wote wanaohusiana na ardhi katika Wilaya ya Chunya, kwa pamoja tujadili masuala yanayohusu ardhi katika Wilaya yetu.” Aliongeza Bi. Catherine.

Programu hiyo inatekelezwa na shirika la MIICO ambalo linatekeleza mradi wa ushawishi wa upatikanaji wa ardhi bora kwa wazalishai wadogo katika Wilaya ya Chunya kata za Sangambi na Upendo kwenye vijiji 6 ambavyo ni Sangambi,Shoga, Itundu, Nkwangu,Upendo na Lola.

Mradi huo umewajengea uwezo wananchi katika kutambua sheria mbalimbali na matumizi bora ya ardhi ambapo kupitia mradi huu wananchi mbalimbali wameweza kutambua umuhimu wa kufanya mpango wa matumizi bora ya ardhi, ambapo jumla ya wananchi 153 wamejiandikisha kwa ajili ya kupimiwa maeneo yao ili kupata hati za kimila.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa kikao Mh. Bosco Mwanginde ambaye ni Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Chunya ameliomba Shirika la MIICO kufika katika maeneo mengi zaidi ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya matumizi bora ya ardhi.

“Mimi naomba Shirika lenu liweze kutanuka, badala ya kata mbili liongeze wigo kwenye maeneo mengine kwa namna yoyote ile ili watu wapate elimu ya ardhi ili kuondoa migogoro tunayokutana nayo huko.” Alisema Mwanginde.

Aidha Mwanginde ameutaka uongozi wa ardhi Wilaya kuhakikisha vijiji vyote ambavyo havina ramani na bikoni vipatiwe ili kuweza kuondoa migogoro ya ardhi kwenye maeneo hayo.

Pia amewataka MIICO kwa kushirikiana na Maafisa Ardhi wa Wilaya kuhakikisha wanakwenda kwa wananchi kutoa elimu ya matumizi bora ya ardhi ili jamii iwe na uelewa wa masuala ya ardhi.

“Msiishie tu kwa sisi viongozi hii nafikiri ikienda kwenye mikutano ya hadhara wananchi wakipata elimu itakuwa ni vyema zaidi, kama mtapanga ratiba yenu kwenda kutoa elimu kwenye maeneo mbalimbali kwenye mikutano ya hadhara inaweza kuwa na maana kidogo.” Alisema Mwanginde.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.