• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE.BATENGA, UKIMWI BADO UPO TUENDELEE KUCHUKUA TAHADHARI.

Imewekwa: December 1st, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya mhe.Mbaraka Alhaji Batenga  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya amewataka wananchi kuendelea kujikinga  na kuchukua tahadhari, kwani Ugonjwa wa Ukimwi bado upo licha ya juhudi ambazo zinaendelea kufanywa na serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali,  bado tiba na chanjo ya ugonjwa huo bado haijapatikana.

Kauli hiyo ameitoa leo Desemba 1/ 2024 katika siku ya  Maadhimisho  ya UKIMWI duniani yamefanyika kimkoa katika  Uwanja wa Shule ya Msingi Itete kata ya Ifumbo Wilaya ya Chunya yaliyobebe kauli mbiu isemayo “Chagua njia sahihi, tokomeza UKIMWI"  ambapo jamii imeweza kuchangia damu kupima pressure na kisukari pamoja na kupata elimu.

“Niwaombe ndugu zangu tuendelee kujitokeza kupima afya zetu kwani UKIMWI bado upo  pamoja na jitihada ambazo zinaendelea kufanyika lakini Tiba bado haijapatikana wala chanjo bado haijapatikana tukilitambua hilo  tutaendelea kujikumbusha kwamba UKIMWI bado upo  hivyo tuishi kwa kujikinga na  kuchukua tahadhari “amesema Mhe. Batenga.

Aidha Mhe Batenga ameongeza kuwa msingi wa kwanza wa mtu ni kuwa na afya njema kwani maendeleo pesa na mambo mengine yanapatikana kwa kuwa na Afya njema  huku akitoa rai kwa wanaume kujitokeza kupima Afya zao badala ya kutegemea vipimo vya wake zao kwamba  majibu ya wake zao ndio majibu yao kwani jambo hilo si sahihi afya ni jambo la mtu binafsi na si jambo la familia.

“Wanaume achene kutembea na majibu ya vipimo vya wake zenu hasa  yanapokuja majibu mazuri,Wanaume acheni tabia hiyo   kwani  anayepata ugonjwa huu ni mtu na si familia na si lazima mke akiugua na mume  naye lazima augue au mke akiwa mzima na mume lazima awe mzima  hivyo kila mtu akapime yeye mwenyewe ajue afya yake na si kuulizia majibu ya mtu mwingine” amesema Mhe.Batenga

Awali akitoa salam katika Maadhimisho diwani wa kata ya Ifumbo Mhe Weston Mpyila kwaniaba ya wanachunya na wananchi wa Ifimbo ameshukuru maadhimisho hayo kuadhimishwa  katika Wilaya ya Chunya kimkoa kwani imekuwa nafasi nzuri ya wao  kujifunza  kupitia  mada mbalimbali kutoka kwa Wadau na wataalam lakini pia nyimbo na burudani  zenye jumbe tofauti tofauti ili  kutoa elimu  kuhusu Ugonjwa wa UKIMWI ili jamii iendelee kuchukua tahadhari na kuendelea kujikinga

Akisoma taarifa ya hali ya utowaji wa huduma za VVU na UKIMWI Mratibu huduma za Ukimwi  Mkoa wa Mbeya  Dkt Deo Magongwe amesema kuwa lengo la maadhimisho  ni kuongeza uelewa katika jamii na kuijulisha jamii kufahamu mafanikio na changamoto zinazoikabili dunia juu ya tatizo la maambukizi ya VVU na UKIMWI pamoja na  kuandaa mikakati mbalimbali ya namna ya kukabiliananazo

Wadau mbalimbali  wakiwemo SHDEFHA, DSW ,NIMRI   kwa pamoja wameendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya kujikinga na kuendelea kuchukua tahadari dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI ikiwa ni pamoja na kuhamasisha jamii kuendelea kupima Afya zao, kutumia kinga ili kulinda Afya zao kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla .

Maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani huadhimishwa kila mwaka Tarehe 1 Desemba ili kuelimisha jamii dhidi ya Ugonjwa wa Ukimwi pamoja na kuchukua tahadhari, katika Mkoa wa Mbeya Maadhimisho haya yamefanyika Wilaya ya Chunya  ambapo yamehudhuriwa na watalamu mbalimbali kutoa Mkoani, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Vikundi vya burudani na Wananchi.

Mkuu wa Wilayaya Chunya Mhe.Mbaraka Alhaj Batenga  ametembelea banda la damu salama kujionea wananchi wakichangia damu wakati wa Maadhimisho ya siku ya UKIMWI dunani iliyofanyika kimkoa katika Wilaya ya Chunya.

Diwani wa kata ya Ifumbo Me.Weston Mpyila akieleza namna ambavyo elimu waliyoipata itawasaidia kuendelea kuchukua tahadhari na kujikinga dhidi ya UKIMWI wakati wa maadhimisho siku ya UKIMWI duniani yaliyoadhimishwa katika kata ya Ifumbo Uwanja wa Shule ya Msingi Itete.

Mratibu wa huduma za UKIMWI Mkoa wa Mbeya Dkt Deo Magongwe akisoma taarifa ya hali ya maambukizi ya VVU na UKIMWI Mkoa wa Mbeya wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI  yaliyofanyika Wilayani Chunya.

Mkuu wa Wilayya ya Chunya Mhe.Mbaraka Alhaj Batenga akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau kutoka shirika la DSWpamoja na wataalam mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani  wilayani Chunya

Wananchi wa kata ya Ifumbo  wakifuatilia elimu mbalimbali kuhusu UKIMWI wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI yaliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Itete kata ya Ifumbo.



Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.