• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE. SHUMBI, JUHUDI ZA UKUSANYAJI WA MAPATO ZIENDELEE KWA KASI ZAIDI.

Imewekwa: October 22nd, 2024

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Mheshimiwa Ramadhani Shumbi amewataka Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  kwendelea kushikamana na kusimama kwa nguvu moja  katika kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ili kuhakikisha Halmashauri  inaendelea kufanya vizuri  katika ukusanyaji wa mapato na kuvuka lengo lililokusudiwa la  kukusanya Shilingi Bilioni 38 kutoka vyanzo vya mapato ya ndani na nje  mwaka wa fedha 2024/2025 ili kuharakisha maendeleo ya Wilaya ya Chunya.

 Hayo ameyasema Septemba, 22/2024 kwenye kikao cha Baraza la madiwani lililoketi katika ukumbi Halmashauri ya Wilaya ya Chunya jengo jipya la Utawala.

Aidha, Mheshimiwa Shumbi amesema Halmashauri imeidhinisha kukusanya kiasi cha bilioni 38 kutoka vyanzo vya ndani na nje, mpaka kufika mwezi Septemba, 2024 Halmashauri imekusanya kiasi cha shilingi bilioni 12 sawa na asilimia 33 ya makusanyo yote huku akihimiza kuendeleza kasi ya ukusanyaji mapato .

“Halmashauri ya Wilaya ya Chunya inaendelea kuwa miongoni mwa Halmashauri zinazofanya vyema katika maeneo mbalimbali ikiwemo ukusanyaji wa mapato ambapo hadi kufikia robo ya kwaza tumeweza kukusanya mapato kwa asilimia 30 ikiwa ni zaidi ya asilimia 5 ya lengo la ukusanyaji mapato, kazi ya ukusanyaji mapato ni yetu sote nasisitiza zoezi hili liendelee kwa kasi mpaka utakapomalizika mwaka wa fedha  2024/2025” amesema Mhe. Shumbi.

Ameongeza kwa kusema, Halmashauri itaendelee kudhibiti mianya yote ya upotevu wa mapato kwa kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano ili kufikia malengo ya ukusanyaji mapato na kuwaletea wananchi maendeleo kupitia ilani ya chama cha mapinduzi, amesema Mhe. Shumbi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe. Mbaraka Alhaji Batenga amemtaka Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kufuatilia madeni ya wadau mbalimbali ikiwemo kampuni ya Tumbaku ambayo inadaiwa zaidi ya Shilingi bilioni 3 ili kufikia lengo la kukusanya shilingi bilioni 38 katika mwaka wa fedha 2024/2025.

“Halmashauri ya Wilaya ya Chunya tumepanda daraja kutoka asilimia 40 mpaka asilimia 60 katika kutekeleza miradi ya maendeleo, lengo la mwaka wa fedha 2024/2025 ni kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni 38, Mkurugenzi fuatilia tunaowadai wote ikiwemo kampuni ya Tumbaku tunaowadai shilingi bilioni 3.5” amesema Mhe. Batenga.

Katika hatua nyingine, Mhe. Batenga amewataka madiwani wa Wilaya ya Chunya kuwahimiza wananchi wao kwenda kupiga kura kuchagua viongozi wa serikali za mitaa itakapofika tarehe 27 Novemba, 2024 huku akieleza idadi ya wananchi waliojiandikisha ni asilimia 80 kati ya wananchi 18,544 ya idadi ya wakazi katika kata zote 20 za Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

“Asilimia 80 ya waliojiandikisha kwenye daftari la mkazi lazima ionekane kwenye zoezi la kupiga kura kila mmoja kwa nafasi yake ahakikishe anawahimiza wananchi kwenda kupiga kura” amesema Batenga.

Mkutano wa Baraza la Madiwani robo ya Kwanza  kwa kipindi cha Julai hadi Septemba umehudhuriwa na Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya, katibu wa chama cha Mapinduzi, Wataalam mbalimbali kutoka Halmashauri , Wananchi pamoja na Waandishi wa Habari.

waheshimiwa Madiwani wakiendelea kupitia taarifa mbalimbali za robo ya kwanza kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Septemba wakati wa kikao cha baraza la robo ya kwanza kilichoketi katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri (Jengo jipya la Utawala).

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.