• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE. MWANGINDE AWATAKA MADIWANI CHUNYA KUKAMILISHA MIRADI INAYOANZISHWA KWA NGUVU ZA WANANCHI.

Imewekwa: January 28th, 2025

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Mhe. Bosco Mwanginde ametoa rai kwa waheshimiwa madiwani kuhakikisha miradi yote inayoanzishwa kwa nguvu za wananchi inakamilika kwa asilimia miamoja (100%) na sio kutegemea Halmashauri kukamilisha miradi hiyo , halmashauri itaongeza nguvu pale itakapo  wezekana kufanya hivyo.

Kauli hiyo ameotoa Mhe. Mwanginde  tarehe 27/01/2025 wakati wa kikao cha baraza la kujadili na kupitia randama  ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kilichoketi katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri jengo jipya la utawala.

Miradi yote inayoanzishwa kule kwenye vijiji na kata ni miradi ya kwetu Madiwani kwa wananchi wetu, tunatakiwa kuianzisha miradi na kuikamilisha kwa asilimia mia moja(100%), pale tunapokuwa na uwezo katika Halmashauri basi Halmashauri itaongeza nguvu lakini sio kuanzisha mradi na kuachia njiani kwamba  Halmashauri itamalizia kwani hiyo inaweza kusababisha mradi kuchukua muda mrefu kukamilika. Amesisitiza Mhe. Mwanginde.

 Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe.Mbaraka Alhaj Batenga ametoa pongezi kwa vyama vya siasa na waheshimiwa madiwani kwa kufanikisha uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mafanikio makubwa, amani na utulivu nakusihi hali hiyo iendelee hadi kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu 2025.

Aidha, Mhe.Baenga amewaeleza waheshimiwa madiwani kusudi la  Halmashauri kuanzisha kituo cha redio cha Halmashauri kitakachosaidia kufikisha taarifa na elimu ya mambo mbalimbali kwa wananchi wa Chunya na maeneo jirani kwa uraisi zaidi, Vilevile, amepongeza juhudi mbalimbali zinazofanyika katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ambapo hadi mwezi January 2025, Halmashauri imekusanya mapato Tsh. Bilioni 7.9 sawa na asilimia tisini na moja (91%) ya lengo la makadirio ya kukusanya Tsh. Billion 8.7 iliyopangwa kukusanywa kwa mwaka.

Afisa mipango na uratibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Bi Janeth Mwaigoga akisoma randama ya mpango wa bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  kwa mwaka wa fedha 2025/2026 amesema kuwa vipaumbele  vya halmashauri  katika bajeti hiyo ni pamoja na kutenga fedha na kuviwezesha vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu, kuboresha huduma za kijamii, kuongeza ukusanyaji wa mapato  pamoja na mambo mengine mengi.

Kikao cha baraza cha kujadili na kupitia makadirio ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026  kimehudhuriwa na waheshimiwa madiwani, kamati ya ulinzi na usalama, wataalamu wa halmashauri ya Wilaya ya Chunya , wataalamu kutoka taasisi mbalimbali pamoja na wadau wa vyama vya siasa.

Afisa mipango na uratibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Bi Janeth Mwaigoga Akisoma randama ya bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 wakati wa kikao cha baraza cha kujadili randama hiyo

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe.Mbaraka Alhaj Batenga  akitoa pengezi kwa waheshimiwa madiwani na wajumbe wa kikao cha balaza la kujadili radama ya bajeti kwa mwaka 2025/2026 kilichoketi ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri jengo jiya la Utawala.

 Diwani wa kata ya Lupa Mhe Daniel Mwafyele akitaka ufafanuzi juu ya miradi itakayotekelezwa wakati wa kikao cha kujadili randama ya bajetii kwa mwaka wa fedha 2025/2026.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.