• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE MASACHE ACHANGIA MIFUKO 230 YA SARUJI KATA YA CHALANGWA

Imewekwa: October 10th, 2023

Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe Masache Njelu Kasaka amechangia mifuko mia mbili na thelasini (230) ya Saruji katika kata ya Chalangwa ili kuungana na wananchi kuhakikisha miradi ya maendeleo inakamilika huku akiwaahidi wananchi hao kuendeleo kuiomba serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kuendelea kuleta fedha ili kutatua kero mbalimbali za wananchi wa Jimbo la Lupa wakiwepo wananchi wa Kata ya Chalangwa.


Akizungumza kwa nyakati tofauti leo tarehe 10/10/2023 wakati wa ziara yake ya kupokea  na kutatua kero  za wananchi katika mikutano miwili tofauti amesema yeye kama mtoto wa jimbo la Lupa lazima ashiriki kikamilifu kuhakikisha kero mbalimbali za wananchi zinatatuliwa ili wananchi waendelee na shughuli zao za kawaida za kujipatia kipato na hatimaye ujenzi wa Jamii na Taifa imara kwa kuimarisha uchumi wa mwananchi mmoja mmoja.


“Nimeona juhudi zenu za ujenzi wa Bweni katika shule ya Sekondari ya kata ya Chalangwa na mimi kama mwenzenu lazima niwaunge mkono tukamilishe ujenzi huo ili watoto wetu wapate mazingira mazuri ya kusoma hivyo nitachangia mifuko mia moja (100) ya saruji ili mwendelee na ujenzi huo. Na kwakuwa Afya ndio kila kitu maana bila uimara wa afya zetu basi hakuna kinachoweza kufanyika na pia nimeona  juhudi zenu katika ujenzi wa wodi katika kituo cha afya cha Chalangwa  lazima nishiriki kuimarisha afya za wanachunya nitachangia mifuko mia moja (100) kwenye kituo cha Afya”.


Mhe Masache  amechangia mifuko 30 ili kuunga mkono ujenzi wa Josho katika kijiji cha Itumba kilichopo kata ya Chalangwa ili kutatua changamoto ya josho eneo hili ikiwa ni ombi kutoka Mwananchi wa eneo hilo alipopata nafasi ya kutoa kero yake mbele ya Mbunge wa Jimbo la Lupa alipotembelea kijiji hicho leo ili kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia suluhu zinazowekana kwa wakati huo na kuchukua kero zilizo nje ya uwezo wake na kuendelea kutafuta suluhu ili wananchi waendelee na shughuli za uzalishaji mali.


Mhe Diwani wa Kata ya Chalangwa Mhe Haji Chapa amesema wananchi wa kata ya Chalangwa wanaishukuru serikali kwa namna ambavyo fedha nyingi zimeletwa katika kata hiyo ingawa bado kuna changamoto mbalimbali kama vile Maji, umeme na  daraja la izumbi hivyo amemwomba Mbunge wa Jimbo la Lupa kuendelea kuwapambania wananchi wa Chalangwa na Chunya Kwa ujumla wake ili changamoto hizo zipate suluhu kama ilivyo kwenye afya kwani uwepo wa kituo cha Afya Chalangwa umeleta suluhu ya Changamoto zote kwa upande wa Afya.


Fanuel Dickson Mbalamwezi, Samwel Wiston, Luciana Shonza, Mwakisole Edwin na Mawazo Jailos kwa niaba ya wananchi wengine wameishuru serikali ya Jamhuri ya Muungano pamoja na Mbunge wa jimbo la Lupa kwa namna ambavyo wameendelea kutatua kero za wananchi wa Kata ya Chalangwa huku wakiendelea kuomba kusaidiwa kupata walimu katika shule za Msingi katika kata hiyo, maji ya uhakika pamoja na usimamizi wa Mbolea ya Ruzuku ili waweze kufanya vizuri katika kilimo msimu ujao.


Mbunge wa Jimbo la Lupa bado anaendelea na ziara ya kukutana na wananchi ili kuwapa mrejesho wa utekelezaji wa yale aliyotumwa kuyatekeleza lakini pia kuchukua kero na changamoto nyingine ili aendelee kutafuta suluhu kwana kwa kushirikiana na wnanchi na zile nyingine kuenda kuiomba serikali kupitia bunge kusaidia kuleta suluhu yake. Ziara itaendelea kesho kwa kata ya Ifumbo ambapo mikutano miwili itafanyika kuanzia kijiji cha Lupamaketi na baadaye kijiji cha Ifumbo

Mbunge wa Jimbo la Lupa (Katika aliyevaa suti ya Blue) akihutubia wananchi wa kijiji cha Chalangwa

Diwani wa kata ya Chalangwa Mh. Haji Chapa akizungumza kwa furaha mambo yaliyotekelezwa kwenye kata hiyo na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kabla ya kumkaribisha bunge wa Jimbo la Lupa wakati wa ziara ya kuzungmza na wananchi wa Itumba

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Itumba  Mwalimu Sadock Waiton Gallaakitoa shukrani zake kwa niaba ya Shule ya Msingi Itumba kwa Mbunge wa Jimbo la Lupa kwa namna alivyoshiriki katika kuchangia ujenzi wa majengo mbalimbali katika shule hiyo

Mbunge wa Jimbo la Lupa akieleza jambo wakati alipokuta na uongozi wa Jumuhiya ya watumia maji kata ya Chalangwa kabla ya kuanza mikutano ya ndani na mikutano ya hadhara wakati wa ziara yake ya kuzungumza na wanancchi wa kata ya Chalangwa 

Katibu wa umoja wa vijana wa wilaya ya Chunya Ndugu Mayeye akizungumza jambo kwenye kikao cha viongozi wa Jumuhiya ya watumia maji kata ya Chalangwa wakati Mbunge wa Jimbo la Lupa alipotembelea kata ya Chalangwa

Mbunge wa Jimbo la Lupa pamoja na viongozi wa jumuhiya ya watumia maji kata ya Chalangwa wakati wa Mazungmza yao kuhusu changamoto ya maji katika kata hiyo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.