• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE BATENGA: WASAIDIENI MAFUNDI WAZAWA KUJISAJILI NeST

Imewekwa: December 10th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaji Batenga amewaagiza viongozi wa Serikali walioko kwenye vijiji na kata za Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuwaongoza na kuwasaidia Mafundi wazawa pamoja na wananchi wenye uwezo wa kuwa wazabuni wa vifaa mbalimbali kujisajili kwenye mfumo wa Nest ili waweze kunufaika kwa kutoa huduma kwa Serikali wakati wa utekelezaji wa Miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yao

Ametoa agizo hilo leo 10/12/2024 wakati kamati ya Usalama ilipokuwa inakagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Nkung’ungu inayojengwa kwa fedha shilingi milioni mia tano themanini na tatu kutoka Serikali kuu

“Ninyi watendaji wa vijiji na kata, walimu wakuu na wakuu wa Shule waongozeni Mafundi wazawa pamoja na wananchi wanaoweza kuwa wazabuni katika miradi mbalimbali wajiunge kwenye mfumo wa Nest ili waweze kuomba tenda ili kutekeleza miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye maeneo yao kwani kufanya hivyo itapunguza baadhi ya usumbufu mnaokutana nao wakati wa utekelezaji wa miradi kwa kupitia mafundi wanaotoka mbali na eneo la ujenzi wa mradi”

Aidha Mhe Batenga ameonya kamati za Ujenzi kutopokea vifaa vyenye mapungufu au vibovu kwani vifaa vibovu ndio mwanzo wa kazi kukosa ubora huku akiwakumbusha kwamba ikibainika vifaa vyovyote vibovu vimepokelewa basi watawajibika

“Kamati msipokee vifaa/vitu vibovu, Naomba sana hilo. Na kama hamjaelewana mwambie aliyeleta vifaa vibovu kwamba aviweke pembeni mpaka vitakapokaguliwa. Tafadhari sana nimetoa tahadhari hii mapema kabisa maana atakayebainika tutagombana sana eneo hili” Aliongeza Mhe Batenga

Kaimu Mkurugenzi mtendaji Ndugu Cuthbert Mwinuka amesema Kuanzia tarehe 17/12/2024 kamati maalumu itapita kwenye kila mradi kutoa elimu ya namna ya kusimamia miradi inayotekelezwa ili kuongeza usimamizi na ufanisi wa utekelezaji wa miradi, ikiwa ni utekelezaji wa moja ya maagizo ya kamati ya usalama wilaya baada ya kukagua miradi kadhaa inayotekelezwa katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Kamati ya Usalama ya wikaya ya Chunya ikiongozwa na mwenyekiti wake Mkuu wa wilaya ya Chunya, imeanza Ziara leo 10/12/2024 ambapo miradi yenye thamani ya shilingi  milioni mia nane kumi na saba (817,159,028) imekaguliwa huku ziara hiyo ikitaraji kuendelea kesho tarehe 11/12/2024 ambapo miradi mingine yenye thamani ya Zaidi ya shilingi milioni mia sita (600,000,000) itakaguliwa

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Batenga (Aliyeshika karatasi Mkono wake wa Kulia) akizungumza Jambo wakati kamati ya Usalama ilipokuwa inakagua ujenzi wa Nyumba ya walimu (Two in one) shule ya Sekondari Kambikatoto

Mkuu wa wilaya ya Chunya akifafanua jambo wakati kamati ya usalama ilipokuwa inakagua ukarabati wa Bwalo la Chakula Shule ya Sekondari Lupa

Baadhi ya Majengo ya Shule ya Sekondari Nkung'ungu, Kamati ya Usalama wilaya ya Chunya pia ilipita na kukagua mradi huo ambao mpaka sasa uko asilimia 65

Kamati ya Usalama ikipokea taarifa ya ujenzi wa Vyumba viwili vya madarasa na matundu sita ya vyoo Shule ya Msingi Mtande, Kamati imepongeza na kusema Ujenzi unaendelea vizuri

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.