• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE BATENGA, “SERIKALI INAPENDA AINA HIYO YA USHIRIKIANO”

Imewekwa: July 12th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga amewashukuru viongozi wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) jimbo la Lupa kwa moyo wao wa kujitoa kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita ya kuwaletea wananchi maendeleo kwa kutoa mifuko mia moja ya Saruji kwa uongozi wa Mamlaka ya mji mdogo wa Makongolosi ili saruji hiyo itumike kujenga miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kujengwa.

Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi saruji hiyo kwa uongozi wa kata ya Bwawani na kata ya Makongolosi iliyofanyika leo tarehe 12/07/2024 kwenye viwanja vya soko la Makongolosi Mhe Batenga amesena Serikali inapenda aina hiyo ya ushirikiano kwani unalenga kuwahudumia wananchi wale wale ambao upande wa Serikali wanaitwa wananchi na upande wa Madhehebu huitwa waumini

“Kila kata hapa imepokea mifuko hamsini ya saruji, bwawani imepokea mifuko hamsini Makongolosi imepokea mifuko hamsini, Nirudie tena kuushukuru uongozi wa Kanisa la TAG kwa jinsi ambavyo waliguswa kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na kutoa saruji mifuko mia moja yenye thamani ya zaidi ya  milioni mbili, wameonesha moyo wa kujitolea sana na sio kwamba wao hawana miradi bali ni kuwahudumia wananchi, na huu ndo ushirikiano tunaoupenda” Amesema Mhe Batenga

Aidha Mhe Batenga amewashukuru viongozi wa dini zote kwa namna ambavyo wanaunga mkono juhudi za kuwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania kwa namna tofauti tofauti kwani zipo taasisi mbalimbali zinazo milikiwa na madhehebu mbalimbali zinatoa huduma kwa wananchi maeneo mbalimbali

“Madhehebu ya dini yanachangia sana katika kutoa huduma kwa jamii, kama mnavyofahamu kuna shule, vyuo katika viwango mbalimbali, hospitali vyote vinamilikiwa na madhehebu ya dini lakini huwahudumia wananchi, hivyo sisi Serikali tuna uhusiano mzuri kabisa na madhehebu yote maana sote tunawahudumia wananchi wale wale kwa namna moja au nyingine” Ameongeza Mhe Batenga

Awali akitoa taarifa ya uwepo wa Saruji hiyo mtendaji mkuu wa Mamlaka ya Mji mdogo Makongolosi Ndugu Linus Mwanitega akimwakilisha Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya amesema Saruji hiyo ilikabidhiwa na uongozi wa Kanisa la TAG ikiwa ni hitimisho la maadhimisho ya miaka 85 ya kanisa lao na lengo lao ilikuwa ni kuungana na Serikali kuendelea kujenga miundombinu katika kata mbalimbali za Mamlaka ya mji mdogo wa Makongolosi.

Kwa niaba ya wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo la kukabidhi saruji hiyo, Bwana Efrahim Kanyenye ambaye pia ndiye mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Makongolosi amewashukuru viongozi wa Kanisa la TAG kwa kuwaptia saruji hiyo na ameiomba Serikali kuendelea kupeleka miradi kwenye kata hiyo kwani wataisimamia kwa weledi

Mtendaji wa Mamlaka ya Mji mdogo wa Makongolosi Bwana Linus Mwanitega akifafanua jambo mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya wakati alipokuwa akisikiliza kero za wananchi wakati wa Hafla ya kukabidhi saruji kwa uongozi wa Kata ya Bwawani na Makongolosi mapema leo

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Makongolosi Ndugu Efrahim Kanyenye akitoa shukrani zake kwa kanisa la TAG baada ya kata yake kupokea mifuko Hamsini ya Saruji kutoka kwa uongozi wa Kanisa hilo iliyokabidhiwa leo na Mkuu wa wilaya ya Chunya

Sehemu ya Saruji iliyokabidhiwa kwa uongozi wa kata ya Bwawani na Makongolosi mapema leo, Saruji hiyo ilitolewa na Uongozi wa Kanisa la TAG Jimbo la Lupa ili kuungana na Serikali katika kutekeleza miradi ya Maendeleo katika wilaya ya Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.