• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE BATENGA; RAIS ANAZIJUA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI NA ANAZITATUA ZOTE

Imewekwa: May 29th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaji Batenga amewahakikishia wananchi wa wilaya ya Chunya kwamba Mhe Rais Samia Suluhu Hassan anatambua changamoto zote zinazowakumba wananchi wa Chunya na anazipatia Majibu Changamoto moja baada ya nyingine huku akirejerea Ujenzi wa Kituo cha Afya Kambikatoto, Ujenzi wa Shule ya Sekondari na sasa Utekelezaji wa mradi wa Maji unaotaraji kuanza hivi karibuni.

Akizungumza na wananchi wa kata ya Kambikatoto leo tarehe 29/5/2024 baada ya kumkabidhi mkataba wa Utekelezaji wa Mradi huo Mhandisi Richard Juma kutoka Kampuni ya EquiplusCompany Limited inayotaraji kutekeleza mradi huo Mhe Batenga amewataka wananchi kuwa na Imani na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwani changamoto zote zinapatiwa Suluhu kwa wakati

“Kurahisisha upatikanaji wa Matibabu ya Kibingwa Mhe Rais ametuletea madaktari Bingwa hapa hapa wilayani Chunya, Kituo cha Afya kimejengwa hapa Kambikatoto, Sekondari imejengwa hapa na wanafunzi tayari wanasoma hapa ndugu wananchi Mhe Rais Hajawafikia? Niwaombe muendelee kuiamini Serikali hii ya awamu ya sita na ndo maana leo Mradi wa maji unaanza kutekelezwa hapa kwenu” Amesema Mhe Batenga

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya Meneja wa RUWASA wilaya ya Chunya Mhandisi Olineno Sanga amesema Halmashauri ya wilaya ya Chunya imepokea fedha zaidi ya Bilioni tano ili kutekeleza miradi mbalimbali ya maji ndani ya wilaya ya Chunya huku akisema miradi mingine imekwisha kamilika na mingine iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

“Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya wilaya ya Chunya tumepokea fedha bilioni tano na milioni mia tisa ambapo bilioni nne zimepelekwa wenye mradi wa Maji wa Matwiga wakati pesa zinazobaki zimepelekwa kwenye miradi mbalimbali ikiwepo uchimbaji wa visima katika vijiji kwa Bitimanyanga, Mafyeko, Mtanila, Lupa na Mamba na miradi ya Uchimbaji wa visima inatakiwa kuisha tarehe 30 juni” Amesma Mhandi Sanga

Mhandisi kutoka Kampuni ya Equiplus Company Limited Mhandisi Richard Juma kwa niaba ya Kampuni yake amesema wamejipanga kutekeleza mradi huo kwa ubora, ufanisi na mradi utatekelezwa ndani ya muda uliopangwa huku akiishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuiamini Kampuni hiyo katika kutekeleza mradi huo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Bosco Mwanginde amewashukuru sana wananchi wa kata ya Kambikatoto kwa namna wanavyoshiriki katika ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye maeneo yao huku akiwataka kufanya hivyo pia kwenye mradi maji unaotaraji kuanza kutekelezwa katika kata ya Kambikatoto.

Mradi wa Maji unaotaraji kutekelezwa katika kata ya Kambikatoto utagharimu fedha shilingi milioni mia tano tisini na tano, unajengwa na Kampuni inayoitwa Equiplus Company Limited ambapo utajengwa kwa miezi sita hivyo mradi huo utakamilika mwezi Disemba na utakapokamilika utahudumia wananchi wa kijiji cha Kambikatoto kwa asilimia mia moja

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga (Aliyavaa Shati la Drafti) akimkabidhi Mkataba wa utekelezaji wa Mradi wa Maji Mhandisi Richard Juma kutoka Kambuni ya 

Equiplus Company Limited itakayotekelezaji ujenzi wa mradi wa maji Kambikatoto

Meneja wa RUWASA wilaya ya Chunya Mhandisi Olineno Sanga akizungumza Jambo wakati wa mkutano wa Hadhara Kambikatoto kabla ya Mkuu wa wilaya ya Chunya Kumkabidhi mkandarasi mkataba wa ujenzi wa mradi wa Maji

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Bosco Mwanginde akizungumza na wananchi wa kata ya Kambikatoto wakati wa Mkutano wa kumkabidishi Mkandarasi mkataba wa utekelezaji wa mradi wa maji katika kijiji cha Kambikatoto

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga ( Wa kwanza Kushoto na amevaa shati la Drafti) akiwa pamoja na viongozi Mbalimbali wakipokea taarifa ya kisima ambacho kitatumika kugawa maji kwenye kijiji cha kambikatoto baada ya miundombinu yake kukamilika

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.