• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE BATENGA AMEANZA NA BARABARA ZA ITUMBI NA SAMBILIMWAYA

Imewekwa: January 15th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mrakibu mwandamizi wa Uhamiaji Mhe Mbarak Alhaj Batenga amefanya mazungumzo na Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Mbeya ili kupata ufumbuzi wa haraka kwa changamoto ya Barabara ya kuelekea Sambilimwaya na Barabara ya Matundasi –Itumbi kwani maeneo hayo yana idadi kubwa ya watu lakini yana uzalishaji mkubwa unaochangia pato katika Halmashauri na Taifa kwa ujumla

Mazungumzo hayo yamefanyika leo ofisini kwa Mkuu wa wilaya na baadaye kufanya ziara ya kuzitembelea barabara hizo, Mkuu wa wilaya ya Chunya amemwambia Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Mbeya  kwamba barabara ya Matundasi-Itumbi itazamwe kwa upya kulingana na shughuli za kiuchumi zilizopo katika eneo hilo kwani zinamchango mkubwa kwa Halmashauri na Taifa lakini Barabara ya Mnazi mmoja kwenda Sambilimwaya ikiwezekana iingizwe haraka kwenye mtandao wa barabara na ianze kutengenezwa ili wananchi wanaoishi kwenye kitongoji hicho waendelee kuifurahia serikali ya awamu ya sita

“Najua TARURA mna mchakato wenu wa namna ya kuingiza barabara kwenye mtandao wenu ili ianze kutambulika lakini naomba mchakato ufanyike kwa haraka ili wananchi wanaoishi kwenye kitongozi hicho wapate barabara, lakini Barabara ya Matundasi-Itumbi itazamwe kwa jicho la pekee sana kwani idadi ya wakazi wa eneo hilo ni kubwa lakini pia shughuli za uzalishaji mali zinazoendelea zinamchango mkubwa kwenye mapato ya Taifa hilo” Amesema Mhe Batenga

Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Mbeya Mhandisi Albert Kindole amekiri kuwepo kwa uhitaji mkubwa wa matengenezo ya Barabara hizo baada ya kuzikagua huku akisema pamoja na milioni 92 ambazo tayari Mkandarasi ameanza kazi katika barabara ya Itumbi lakini barabara hiyo imetengewa shilingi milioni 450 kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kwaajili ya Matengenezo makubwa

“Mheshimiwa Mkuu wa wilaya nimekubaliana na mazungumzo tuliyofanya pale ofisini, ni kweli barabara hizi ni muhimu, uwepo wa Mabasi 17 hapa Itumbi ni ishara tosha kwamba Barabara hiyo ni muhimu na inahitaji matengenezo ili kuwarahishia wananchi upatikanaji wa usafiri, hivyo pamoja na million 92 ambazo tayari mkandarasi yupo kazini pia kwa mwaka 2024/2025 Barabara hii imetengewa shilingi milioni 450, Pamoja na hayo nafikiri ofisi yangu itaenda kuandika andiko maalumu ili barabara hii iweze kujengwa kwa kiwango cha lami hapo mbeleni” Amesema Mhandisi  Kindole

Diwani wa kata ya Matundasi Mhe Kimo Choga amesema wananchi wa Matundasi wanapenda maendeleo na wako tayari kujitoa kwani kupitia nguvu za wananchi pamoja na michango mbalimbali ya wadau tayari wameendelea na ujenzi wa majengo mbalimbali kwaajili ya sekondari ambayo tayari ilishapewa jina na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya wakati alipofanya ziara yake katika kitongoji cha Itumbi na kubaini changamoto ya umbali wa shule ya Kata hiyo ambayo imejengwa Matundasi umbali wa Kilomita 12

Ernest Mwakibete, Adamu Mwampiki, Godfrey Mataluma, Oden Mwakanyamale, Mussa Mohamed na wengine kwa niaba ya wananchi wengine walimweleza Mkuu wa wilaya kuhusu changamoto mbalimbali zinazohitaji kutatuliwa huku Barabara ikiwa changamoto kubwa na imezungumzwa na watu wote waliopata nafasi na imeshapatiwa majibu

Ziara hiyo iliyohusisha kamati ya Usalama ya wilaya pamoja na meneja wa TARURA Mkoa sambamba na meneja wa TARURA wilaya ya Chunya imekuja ikiwa ni siku chache baada ya kamati ya siasa kupita kukagua utekelezaji wa Ilani na baadaye kamati ya Fedha, uchumi na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya kupita kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya huku miradi ya TARURA ikiwa ni kati ya miradi iliyokaguliwa

Meneja wa wakala wa barabara za vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Mbeya Mhandisi Albert Kindole (Aliyenyoosha mkono) akizungumza jambo kwa Mkuu wa wilaya ya Chunya mapema leo kabla ya ziara ya kukagua barabara za Sambilimwaya na Itumbi

Mkuu wa wilaya ya Chunya akiongozana na kamati ya usalama ya wilaya sambamba na Meneja wa TARURA Mkoa wa Mbeya wakikagua barabara ya Matundasi-Itumbi mapema leo

Diwani wa kata ya Matundasi Mhe Kimo Choga akipiga magoti mbele y aMeneja wa wakala wa barabara za vijijini na mijini TARURA Mkoa wa Mbeya Mhandisi Albert Kindole akiomba kutengezwa kwa barabara ya Matundasi-Itumbi ili wananchi wake waweze kusafiri pamoja na kufanya shughuli nyingine za kiuchumi kwa urahisi

Baadhi ya wananchi wa Kitongoji cha Itumbi wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Batenda alipowatembelea na kuzungumza nao mapema leo (Pamoja na hali ya Mvua wananchi hao waliendelea kumsikiliza Mkuu wa wilaya kwa makini)

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.