• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MBUNGE WA JIMBO LA LUPA “HATUJAWAANGUSHA NA HATUTAWAANGUSHA”

Imewekwa: October 7th, 2023

Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe Masache Njeru Kasaka amewataka wananchi wa jimbo la Lupa waendelee kuiamini serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwani mpaka sasa imeendelea kutekeleza ahadi zote zilizoahidiwa mwaka 2020 na bado inaendelea kutekeleza.


Ametoa kauli hiyo leo tarehe 05/10/2023 wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nkwangu kwanza kuwapa mrejeso kuhusu Bunge la bajeti na kueleza shughuli mbalimbali zilizofanyika na ambazo zinaendelea kufanyika pamoja na kusikiliza kero za wananchi hatimaye kuzipatia suluhu kero hizo.


“Mimi na viongozi wenzangu hatujawaangusha na hatutawaangusha maana tukiwaangusha maana yake tumemwangusha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Mama Samia Suluhu Hassan jambo ambalo sisi watumishi wenu mliotutuma kuwasemeeni maeneo mbalimbali hatuwezi kufanya hivyo maana hata ninyi ni mashahidi kwamba ahadi tulizo ahidi tunaendelea kuzitekeleza”.


Akijibu kero mbalimbali za wananchi Mhe Mbunge amesema Wilaya ya Chunya imetengewa fedha zaidi ya Milioni mia nane kwaajili ya kununua vifaa tiba kwa mwaka huu wa fedha 2023/2024 hivyo Zahanati ya kijiji cha Nkwangu itakuwa ni moja kati ya wanufaika wa vifaa hivyo ili wananchi waendelee kupata huduma katika zahanati hiyo huku akiwata viongozi kuwapa mrejesho wananchi kuhusu fedha za maendeleo zinazoletwa na hata michango ya wananchi.


“Hakikisheni wananchi wanapata taarifa ya fedha za serikali zinazoletwa kujenga miradi mbalimbali pamoja na fedha zinazotokana na michango yao ili kuepuka usumbufu kwani wananchi wamekuwa wakilalamika kwamba wanachaga fedha lakini hawaoni kilichofanyika lakini ukifuatilia unakuta fedha hizo zimefanya mambo mazuri lakini wananchi hawajui”.


Diwani wa kata ya Upendo Mhe. Mh. Richard N. Itelekelo amemshukuru Mhe Mbunge kwa namna ambavyo ameendelea kuwa mstari wa Mbele kuwapigania wananchi wa wilaya ya Chunya hasa kata ya Upendo kwani miradi mbalimbali kama vile uchimbaji wa visima, ujenzi wa shule ya sekondari, ujenzi wa zahanati na mingine mingi inatekelezwa katika kata ya Upendo kwa fedha kutoka serikalini.


Awali akisoma taarifa kwa niaba ya wananchi mbele ya Mbunge wa jimbo la Lupa Mtendaji wa kijiji cha Nkwangu ndugu Andrew Msoya amesema kijiji kinakabiliwa na Chnagamoto mbalimbali zikiwepo Barabara, kukosekana kwa mawasiliano, Nyumba za watumishi waliopo katika kijiji hicho, vifaa tiba katika zahanati hiyo pamoja na vitanda na Friji la kutunzia chanjo kwaajili ya watoto jambo ambalo husababisha watoto wanaostahili kupata chanjo kukosa chanjo hiyo hivyo kuhatarisha maisha yao.


Mbunge wa jimbo la Lupa yupo katika Ziara yake ya kawaida kuwatembelea wananchi ili kuwapa mrejeso wa bunge la Bajeti lililotamatika mwezi juni, kusikiliza kero za wananchi na kutafuta suluhu na kueleza namna ambavyo serikali inaendelea kutekeleza majukumu yake ili kuleta maendeleo kwa wanachunya wakiwepo wananchi wa kijiji cha Nkwangu. Ziara hiyo itaendelea kesho tarehe 8/10/2023 kwa kata ya Mkola.

Wanacnhi wa kijiji cha Nkwangu wakiwa katika hali ya furaha na shangwe na wengine wakiwa wameinua juu matawi ya miti huku wakishangilia wakati wa mapokezi ya Mbunge wa jimbo la Lupa wakati alipotembelea kijiji hicho wakati wa ziara ya kuwatembelea wananchi wa Jimbo la Lupa

Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe Masache (aliyesimama, Mwenye shati la drafti ndogo) akiinamisha kichwa chake ishara ya kupokea kero ya vifaa tiba katika zahanati ya kijiji cha Nkwangu wakati umoja ya wanawake wa Chama cha mapinduzi walipowasilisha kero hiyo kupitia igizo fupo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.