• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MAJENGO HAYA YAANZE KUTUMIKA IFIKAPO MEI 25, RC HOMERA.

Imewekwa: April 27th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuhakikisha Majengo yanayojengwa katika Hospitali ya wilaya ya Chunya mbayo yapo hatua za mwisho yaanze kutumika ifikapo Mei 25 ili lengo la serikali la kuwapatia huduma wananchi wake litimie

Ametoa maelekezo hayo tarehe 26/4/2023 alipokagua mradi wa upanuzi wa Hospital ya wilaya ya Chunya na baadaye kuweka jiwe la msingi la upanuzi wa Hospitali hiyo ambapo majengo mbalimbali yanajengwa ikiwepo Jengo la wagonjwa wa Nje (OPD), Wodi ya wanaume na wodi ya wanawake, Jengo la upasuaji, Jengo la Mama Ngojea na majengo mengine.

“Nimezungmza nao, nimewambia kwamba kufika tarehe 25/05/2023 majengo haya yaanze kutumika haya ya upasuaji ili wakinamama na kinababa wenye changamoto za uzazi basi waanze kupata huduma katika majengo haya. Na tumshukuru mweshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuleta pesa zaidi ya Bilioni 1.4 katika awamu mbalimbali ili kuendelea kuleta huduma kwa wananchi”

Mkuu pia amewataka viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Chunya kusimamia ujenzi wa miradi hiyo ili iendelee kuleta tija kusudiwa kwa wananchi

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka Saimon Mayeka amemhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwamba ataendelea kumuwakilisha mweshimiwa RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pamoja na Mkuu wa Mkoa katika kuhakikisha miradi inasimimiwa ipasavyo ili ilete tija iliyokusudiwa kwa watanzania wanoishi wilayani Chunya

“Kitu ambacho naweza kukuahidi ni usimizi wa miradi hasa fedha zilizokuja kwenye ujenzi wa hospitali hii, .Nichukue fursa hii kumshukuru mweshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwakuendelea kuleta pesa za miradi mbalimbali ikiwepo fedha za upanuzi wa hospitali yetu ya wilaya ya Chunya tofauti na historia inavyoeleza kwamba hospital hii hapo awali ilikuwa zahanati”

Naye Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe. Ramadhani Shumbi amesema pamoja na miradi yote inayoendela kujengwa katika wilaya ya chunya wataisimamia ipasavyo kuhakikisha inajengwa kwa ubora stahiki

“Pamoja na miradi yote inayoendela hapa chunya, nikuhakikishie kwamba kama Halmashauri ya wilaya tuko vizuri na tutaendela pokea pesa za miradi na kuisimamia vizuri, Niseme tu wilayani Chunya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inatekelezwa vizuri. Na wananchi wa chunya wako pamoja na Rais pamoja na wewe katika kuhakikisha maendeleo yanapatikana”

Mkurugenzi Mtednaji halmashauri ya wilaya Ndugu Tamim Kambona amesema kama Halmashauri wataendelea kutenga fedha pale panapobidi ili kuendela kujenga maeneo watakayoona inafaa yajengwe Na tunamshukuru Mweshimiwa Rais kwa mwaka ujao ametutengea fedha zaidi ya Milioni 800 kwaajili ya kuendeleza ujenzi katika hospitali ya wilaya ya chunya.

Awali akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya Daktari Darison Andrew ameeleza hatua mbalimbali ambazo hospitali imekuwa ikichukua kuhakikisha miundombinu inaboreshwa ambapo moja ya juhudi ni andiko la mradi iliyopelekea UNICEF kufadhiri ujenzi wa majengo mbalimbali ikiwepo jengo la Mama Ngojea

“Mheshimiwa Mkuu wa mkoa hospitali imeendela kuchukua hatua mbalimbali katika kuboresha miundombinu ya hospitali, Kupitia UNICEF 2021 walitusaidia Kuchimba maji, 2022/2023 wametusadia kujenga majengo mbalimbali pamoja na kukarabati majengo kadhaa hapa katika hopspitali yetu ambapo gharama yake inakadiriwa kuwa bilioni moja na milioni mia mbili”

Kilele cha sherehe za Maadhimisho ya siku ya Muungano ambayo hufanyika kila tarehe 26/4 ya kila mwaka, kwa mwaka huu ilifanyika wilayani Chunya Kimkoa mabapo Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera. Kabla hajafika katika viwanja vya Shule ya Msingi Bwawani ambapo maadhimisho hayo yalifanyika Mkuu wa Mkoa alikagua uwanja wa mpira wa miguu unaojengwa katika kata ya Mbugani na baadaye alitembelea hopsitali ya wilaya ya Chunya ambapo baada ya kukagua ujenzi unaoendela hospitalini hapo, aliweka jiwe la msingi la upanuzi wa hospitali hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera mwenye Miwani akizungumza jambo na Watendaji wa Halmashauri wakati akikagua Ujenzi wa majengo unaoendelea kwenye Hospitali ya wilaya, kulia kwake ni Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka mwenye suti nyeusi.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera akikata utepe kuashiria Upanuzi wa Hospitali ya wilaya ya Chunya

Mhe. Juma Z. Homera  Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Akipanda Mti (Mparachichi) katika Hospitali ya wilaya ya Chunya


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.