• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MAFUNZO MLIYOPEWA NDIO ZANA ZA KUWAWEZESHA KUTEKELEZA MAJUKUMU YENU.

Imewekwa: December 24th, 2024

Afisa Mwandikishaji jimbo la Lupa Wakili Athuman Bamba ametoa rai kwa Waandikishaji wasaidizi wa Vituo na Waendesha vifaa vya Bayometric kuyatumia vizuri mafunzo waliyoyapata ikiwa ni pamoja na kuendelea kupitia rejea mbalimbali walizopewa kwani mafunzo hayo ndio zana za kuwawezesha kutekeleza majukumu yao vyema.

Ametoa rai hiyo  leo Tarehe 24/12/2024 wakati akifunga Mafunzo ya  siku mbili kwa Waandikishaji wasaidizi wa Vituo na waendesha vifaa vya Bayometriki  yaliyokuwa yakifanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya (Sapanjo).

“Ninatoa Wito kwenu kuendelea kutumia muda wenu wa ziada kusoma na kupitia maelekezo yote mliyopewa ili kuongeza uelewa zaidi kuhusu wajibu na majukum yenu katika zoezi la Uboreshaji wa Daftari la kudumu la Mpiga kura kwani Mafunzo mliyopewa ndio dhana ya kuwawezesha kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi.”amesema Wakili Bamba

Aidha Wakili Bamba amewaambia Waandishi wasaidizi wa Vituo na waendesha vifaa vya bayometriki kuwa wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sheria , kanuni,  miongozo na  maelekezo yaliyotolewa na Tume  ili kazi  ya Uboreshaji wa Daftari la kudumu  la Mpiga kura ikatendeke kwa uadilifu na haki.

Naye Mwenyekiti wa mafunzo hayo Mwl.Isakwisa Kaminyoge   kwa niaba ya washiriki wa Mafunzo  hayo ameishukuru timu ya wataalam kutoka Tume , Maafisa wa Jimbo na Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata   kwa mafunzo waliyotoa pamoja na kuwaasa washiriki hao kwenda kufanya kazi waliyopangiwa kwa uaminifu, uadilifu na weledi mkubwa kwani wameaminiwa.

Mafunzo ya siku mbili kwa Waandikishaji wasaidizi wa Vituo na Waendesha vifaa vya Bayometriki yalijikita katika mada za ujazaji wa fomu mbalimbali zitakazo tumika katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la Mpiga kura, fomu za kiapo, pamoja na mafunzo ya nadharia na vitendo juu ya namna ya kuandikisha wapiga kura kwa kutumia mfumo wa kujiandikisha Wapiga kura (voters registration system ,VRS)  ikiwa ni maandalizi  ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura  litakalo anza Tarehe 27/12/2024 na kutamatika Tarehe 2/1/2025.

Afisa Tehama kutoka Tume Huru ya Taifa ya uchaguzi  ndugu Overblessing Msuya akielezea vifaa mbalimbali vilivyomo katika  BVR KIT  wakati wa mafunzo kwa waandishi wasaidizi wa vituo na  waendesha vifaa katika   Ukumbi wa Halmashauri  ya Wilaya ya Chunya ( Sapanjo).

Mmoja ya washiriki wa  mafunzo bi Nelly Magasha akiwaeleza washiriki wengine namna vifaa mbalimbali  vinavyounganishwa.

Waandikishaji wasaidizi wa vituo na waendesha vifaa vya Bayometriki wakiendelea kufanya mazoezi juu ya matumizi ya vifaa mbalimbali  vitakavyotumika katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la Mpiga kura.

Waandisjhi wasaidizi wa vituo na waendesha vifaa vya Bayometriki wakifuatilia mafunzo  katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya (Sapanjo).


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.