• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MADIWANI H/SHAURI YA CHUNYA WAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Imewekwa: July 13th, 2022

WAHESHIMIWA madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya wamewapongeza Wataalamu wa Halmashauri na kuwataka kuhakikisha wanatekeleza miradi yote inayoendelea katika wilaya hiyo kwa ubora na kuikamilisha kwa wakati uliopangwa

 Pongezi hizo zilitolewa wakati wa ziara ya Madiwani hao walipotembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri, Mh Bosco Mwanginde amesema, lengo la ziara hiyo ni kujiridhisha juu ya fedha wanazozituma kwenda kwenye miradi kama zinafanya kazi iliyokusudiwa.

"Tunawapongeza kwa utekelezaji wa miradi kwani tunaona kuwa miradi mingi inayotekelezwa ndani ya Wilaya ya Chunya inaonesha imetekelezwa kwa kiwango kizuri na thamani ya fedha inaonekana, Waheshimiwa Madiwani wameutaka uongozi wa Halmashauri kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa kukamilika ili iweze kuwanufaisha wananchi na sio mradi unaanzishwa na kubaki kiporo,“ alisema Mwanginde.

"Ilikuwa inatokea huko nyuma mradi unakaa mpaka miaka mitatu, lengo letu ni kutatua matatizo kama tumeanza lazima tuukamilishe huo mradi” Aliongeza Mwanginde.

Aidha Madiwani wameielekeza menejimenti kufanya marekebisho kwa baadhi ya miradi ambayo waliitolea ushauri ili kuifanya miradi hiyo kuwa na tija kwa jamii na Wilaya kwa ujumla.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Chunya Ndg. Tamim Kambona amewahakikishia Madiwani kuwa watayafanyia kazi maelekezo yote na ushauri ambao wameutoa katika miradi yote, ambapo Kambona amesema Halmashauri imejipanga kuhakikisha kwenye vituo vyote vya afya vyenye changamoto ya maji Halmashauri itachimba visima ili kuondoa changamoto hiyo.

“Mwaka huu wa fedha tutaanza na katika vituo tutaanza vile ambavyo vimeanza kutoa huduma” Alisema Kambona.

Ziara hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri, Mheshimiwa Bosco Mwanginde sanjari na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Ndg. Tamim Kambona, Waheshimiwa Madiwani walikagua ujenzi wa shule shikizi Manyili iliyopo kijiji cha Sipa kitongoji cha Manyili, ujenzi wa kituo cha Afya Kambikatoto pamoja na kituo cha Afya Mafyeko.

Aidha Waheshimiwa Madiwani walitembelea ujenzi wa hospitali ya Wilaya, soko la madini, kituo cha afya Sangambi, ujenzi wa uzio katika mnada wa mapogoro pamoja na ujenzi wa jengo la utawala.



Waheshimiwa Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya wakikagua Ujenzi wa Jengo la IMD katika hospitali ya wilaya yaChunya

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Dr. Darison Andrew aliyevaa shati Jeupe akitoa maelezo kwa Waheshimiwa Madiwani wa halmashauri walipotembelea hospitali ya wilaya kukagua miradi inayotekelezwa haspitalini hapo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.