• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MAAGIZO MATANO YA DKT. SAMIA YATEKELEZWA KWA VITENDO CHUNYA.

Imewekwa: September 4th, 2024

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa kupitia Mkoa wa Mbeya ndugu Ndele Mwaselela amesema  viongozi wa Wilaya ya Chunya wametekeleza kwa vitendo maagizo matano ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan,

Pongezi hizo alizitoa wakati akizungumza na wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Chunya Septemba 2, 2024 huku akisema, Rais Samia alifika Chunya Agosti, 6 mwaka 2022, akihutubia mkutano wa hadhara, Rais alitoa maagizo matano ikiwemo kuziba miaya ya upotevu wa fedha na kukusanya mapato ili kuwaletea wananchi maendeleo.

“Rais Samia, alitoa maagizo matano ambayo kimsingi yote yametekelezwa kwa vitendo na Viongozi wa Wilaya ya Chunya, hongereni sana kwa kazi nzuri muliyoifanya” alisema Mwaselela.

Pamoja na mambo mengine Mwaselela amewapongeza viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwa kusanya fedha vizuri jambo linalopelekea utekelezaji wa Ilani katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuwa halisia.

“Kwenye kukusanya mapato nimeambiwa hapa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya imevuka lengo kwa kusanya asilimia 150 na kuziba mianya ya upotevu wa fedha kwa kulipa na kukusanya fedha kupitia mfumo” alisema Mwaselela.

Aidha Mwaselela amesema, Rais aliagiza ujenzi wa  stendi mpya kubwa na ya kisasa Chunya, ambapo sasa  Halmashauri ya Wilaya Chunya imeshatenga Shilingi Bilion 2.2 kwaajili ya stendi hiyo na Mkandarasi ataingia mkataba wa ujenzi wa Stendi hiyo siku ya Jumatatu, Septemba 9, 2024.

“Halmashauri ya Wilaya ya Chunya imetenga kiasi cha shilingi Billion 2.2 kujenga stendi ya kisasa na itajengwa ndani miezi tisa hadi kukamilika na stendi hiyo itajengwa Itewe karibu na sheli ya LY” amesema Mwaselela.

Mheshimiwa Mwaselela ameongeza kuwa, agizo lingine ilikuwa ni uboreshwaji wa miundombinu na kununua vifaa tiba vya Hospitali ya Wilaya ya Chunya ambapo fedha za zilishafika na tayari kazi imefanyika.

“Serikali ilileta bilion 1.7 kwaajili ya kununua vifaa tiba na kuboresha miundombinu ya Hospitali ambapo Billioni 1.1 ni vifaa tiba na milioni mia sita ilikuwa  ni kuboresha miundombinu”

Agizo la tano ilikuwa upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa Chunya, ambapo Mwaselela amesema asilimia 65 maji yanapatikana kwenye Wilaya hiyo.

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Chunya, mhandisi Elineno Sanga amesema mpaka ikifika mwezi Mei mwakani maji yatafika kwa wananchi kwa asilimia 85 na lengo la kufikia asilimia 100 linaendelea kufikiwa.

Wakati huo huo wananchi waliiomba Serikali kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji, ujenzi wa barabara, ujenzi wa kituo cha polisi, na kutengenewa maeneo ya uchimbaji wa madini ambayo inatoa ajira nyingi kwa vijana na kina mama wa Wilaya ya Chunya.

MNEC aliwaahidi wananchi wa Wilaya ya Chunya kuwa, Chama cha Mapinduzi kimesikiliza na kimezichukua changamoto zote zilizoibuliwa na kwenda kuzifanyia kazi kwa haraka na kuwaletea maendeleo wananchi wa Wilaya hiyo.

Mjumbe wa Halmashauri kuu CCM taifa Mkoa wa Mbeya ndugu Ndele Mwaselela akicheza na wananchi pamoja na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM)  wakati alipotembelea kitongoji cha Itumbi  kwaajili ya Kuzungumza na Wananchi wa kitongoji hicho.

Wananchi na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi(CCM)  wakimsikiliza Mjumbe wa Halmashauri kuu CCM Taifa ndugu Ndele Mwaselela alipokuwa akisikiliza na kutatua kero za wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kitongoji cha Itumbi. kata ya Makongolosi 


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.