• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MAAFISA USAFIRISHAJI WAKUMBUKWA CHUNYA

Imewekwa: November 18th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka amewaasa na kuwataka maafisa usafirishaji wenye tabia ya kujihusisha na mapenzi na wanafunzi kuacha mara moja kwani madhara ya tabia hiyo ni makubwa kwa mtuhumiwa, mwanafunzi na hata jamii kwa ujumla

Ameyasema hayo wakati akizindua mashindano ya mpira wa miguu yanayoraji kufanyika katika uwanja wa mpira wa Miguu sababa yanayojulikana kama Mayeka usalama Cup, aliyoyaandaa kwa lengo la kuhamasisha watu kujifunza elimu ya usalama kwanza kwa maafisa usafirishaji na baadaye abiria na wananchi wengine wa wilaya ya Chunya

 “Mtu anayekutwa na hatia ya kumpa Mimba mwanafunzi anaweza kupata kifungo cha maisha au miaka 20 niwaombe sana tuwalinde wanafunzi wote kwa pamoja na tuwaache watimeze ndoto zao” alisema Mhe Mayeka mkuu wa wilaya.

Pia Mhe Mayeka amewataka maafisa usafirishaji hao kujiepusha na vitendo viovu vinavyoweza kusababsha kupata kifungo cha maisha au adhabu mbalimbali jambo linaloweza kuathiri kazi zao pamoja na familia

 “Baadhi yenu mmehusishwa na matukio mabaya ya uporaji, unyanganyi, ujambazi na utoroshaji wa dhahabu na wengine wamekamatwa wakibeba nyara za serikali kama meno ya Tembo, mbao na mkaa hayo yote ni mambo mnayopaswa kuwa makini” Alisema Mhe Mayeka

Aidha Mhe Mayeka amewataka Maafisa usafirishaji hao kusoma mwenendo ya wateje wao kwani maafisa usafirishaji hao wamekuwa wakibeba wateja wengi na wenye tabia mbalimbali hivyo ni vyema kuwa makini na wateja hao ili kuepuka kuingizwa kwenye hatia lakini pia kuhatarisha hata maisha yao wao wenyewe

Kwa uande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya chunya Ndugu Tamim Kambona amesema kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri inatarajia  kujenga kitua cha Radio ‘CHUNYA FM’ ili kuweza kuitangaza vyema Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikiwa ni pamoja na kutangaza fursa mbalimbali zilipo katika sekta ya Michezo wakati huo akisema ujenzi wa uwanja wa michezo uko hatua mbalimbali za ujenzi na ukikamilika utasaidia kupunguza adha ya viwanja Chunya

“Tunatarajia kwa mwaka ujao tutajenga redio ya kwetu ya halmashauri ya wilaya ya chunya ili tuweze kuitangaza Chunya yetu, sambamaba na hilo ujenzi wa uwanja wetu wa mpira unaendelea ingawa kuna kususa sua kidogo kutokana na changamoto za kimfumo lakini mara itakao rejea tutaendelea na zoezi lile lakukamilisha kwa hatua za mwisho ili tuweze kutengeneza Eneo la kuchezea (Pitch)”.

Mashindano hayo yanayotaraji kuhusisha timu nne kutoka kwa maafisa usafirisha, yatadumu kwa wiki moja mpaka kupatikana kwa msindi . Michezo iliyohusika katika ufunguzi ni pamoja na kuvuta Kamba, kukimbiza kuku pamoja na Mpira wa miguu ambapo timu ya Madereva Bajaji na Madereva bodaboda walitoka suluhu ya bila kufungana katika Mchezo huo

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamimu Kambona akizungumza na Hadhara ilyojitokeza wakati wa ufunguzi wa Mayeka Usalama Cyp mwisho mwa juma katika viwanja vya sabasaba Chunya

Mkuu wa wilaya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka akikagua timu wakati wa mechi ya ufunguzi wa mashindano ya Mayeka Uslama Cup mwishoni mwa juma

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka akigawa vifaa kwa moja ya timu zitakazoshiriki katika ligi ya Mayeka Usalama Cup inayotaraji kuchezwa wilayani Chunya hivi karibuni

Timu zikiendelea na mchezo wa Ufunguzi wa Ligi ya Mayeka Usalama Cup inayotaraji kuchezwa hivi karibu wilayani Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.