• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

LINDENI UMOJA WENU WANACHAMA WA MTANILA AMCOS MTAFANIKIWA ZAIDI

Imewekwa: December 6th, 2024

Katibu tawala wa wilaya ya Chunya Ndugu Anaklet Michombero amewataka na kuwahimiza wanachama wa Vyama mbalimbali vya Ushirika vilivyo wilayani Chunya kuhakikisha wanalinda Umoja katika vyama vyao kwani mgawanyiko huleta mtafaruka na wakati mwingine kukosa umoja kunaweza kuhatarisha Vyama vyao.

Ametoa kauli hiyo leo wakati alipoaalikwa kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama Cha Msingi cha Ushirika Mtanila uliofanyika leo tarehe 6/12/2024 kwenye Ukumbi mdogo wa Ghala la Mtanila ambapo pia aligawa vifaa mbalimbali kama vile Kompyuta, Mashine ya kudurufu karatasi, vitanda, meza, dawati na viti vilivyonunuliwa na Chama hicho kwa lengo la kuigusa jamii yao inayowazunguka.

“Niwaombe muendelee kuwa wamoja na kwakufanya hivyo mtaendelea kuzalisha kwa faida kiasi cha kupata faida ambayo mnaweza kurudisha kwa Jamii kama mlivyofanya leo, Niwaombe sana lindeni umoja huu, Niwakumbushe mara zote mgawanyiko husabishwa na mambo makubwa mawili moja watu wanaotaka madaraka ambayo wanaweza wakawa wameyakosa kwenye chama hiki hivyo huanzisha vyama vingine ili wapate vyeo lakini sababu nyingine ni madeni, niwambie ukikimbia na Deni utalipa hata ukiwa Chama kingine” Amesema Michombero.

Naye Kaimu mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Cuthberth Mwinuka awali akimkaribisha Mgeni rasmi amepongeza utulivu na juhudi ya wanachama wa Chama cha Msingi cha Mtanila ndiyo msingi wa mambo makubwa na Mazuri yanayofanywa na Chama hicho kwani kupitia utulivu wao wanajihusisha moja kwa moja kwenye uzalishaji.

Kaimu meneja Mkuu wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Tumbaku CHUTCU Ndugu Juma Shinshi amesema Mtanila ni chama kilichoshika nafasi ya kwanza kwenye uzalishaji wa Tumbaku kwa Msimu uliopita ambapo walizalisha tani milioni moja  laki tano amewapongeza Chama hicho kwa kuzingatia ubora kwani katika upangaji wa viwango vya ubora Chama hicho kilikuwa nafasi ya nne.

Mwenyekiti wa Chama Cha msingi cha Ushirika cha Mtanila Ndugu Isaya Daniel Husen amesema wao kama Chama ni kawaida kutoa vitu mbalimbali kwa Jamii inayowazunguka kwani Mbali na vifaa vilivyotolewa leo, Chama hicho tayari kimefanya shughuli mbalimbali kwa jamii ya Mtanila ikiwepo ujenzi wa vivuko, Fursa kwenye kituo cha Afya na nyingine huku akisema kwasasa wamekubaliana kujenga wodi kwenye kituo cha Afya cha Mtanila.

“Kwasasa tumekubaliana kushiriki katika Shughuli mbalimbali za Ujenzi wa Wodi kwenye kituo cha Afya cha Mtanila ambapo kwa kuanzia tulitoa tripu kumi za mawe na kwasasa tumeruhusu matrekta yetu ya Chama Cha Mtanila Amcos kutumika kwenye shughuli za Ujenzi wa kituo hicho mpaka kitakapokamilika” Amesema Isaya.

Walimu wanufaika wa vifaa mbalimbali vilivyotolewa na Chama cha Msingi cha Mtanila wamesema vifaa hivyo vitasaidia sana kupunguza changamoto zilizokuwepo maeneo mbalimbali, huku wakiwataka vyama vingine vilivyopo maeneo yao kuiga namna Chama hicho kilivyoona umuhimu wa kuwekeza kwenye elimu jambo linalosaidia kuinua taaluma katika jamii

Chama Cha Msingi cha ushirika cha Mtanila kimefanya mkutano wake wa mwaka leo tarehe 6/12/2024 huku lengo kubwa likiwa ni kupitia utekelezaji wa makubaliano ya mkutano uliopita na kuweka mipango kwaajili ya Msimu wa kilimo unaoendelea na lengo likwa ni kufika tani Zaidi ya milioni mbili

Kaimu Mkurugenzi mtendaji wilaya ya Chunya Ndugu Cuthberth Mwinuka akizungumza Jambo wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Msingi cha Ushirika Mtanila Mapema leo

Mwenyekiti wa Chama Cha Msingi cha Ushirika Mtanila Ndugu Isaya Husen akizungumza Jambo wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Chama Hicho yliofanyika mapema leo tarehe 6/12/2024

Baadhi ya wanachama wa Chama Cha Msingi cha Ushirika Mtanila wakisiskiliza maelezo kutoka kwa katibu Tarafa wa Tarafa ya Kipembawe Ndugu Kasim kirondomara wakati wa Mkutano wao wa mwaka ulioketi leo tarehe 06/12/2024

Wanachama wa Chama Cha Msingi cha Ushirika cha Mtanila wakipitia na kufuatilia kwa makini kila jambo linaloendelea kwenye mkutano wa mwaka wa Chama hicho ulioketi mapema leo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.