• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

VIJANA SASA KUWEZESHWA KUCHIMBA DHAHABU CHUNYA.

Imewekwa: August 24th, 2024


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  Kitaifa 2024  ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava amekabidhi leseni 11 za uchimbaji madini kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chunya ndugu Tamim Kambona kwaajili ya kuwezesha Vijana kuchimba Madini kwa vitalu vyenye ukubwa wa ekari  151.8 vyenye gharama ya zaidi ya millioni sita vilivyopo msitu wa hifadhi wa Mbiwe  kata ya Matundasi.

Akizungumza kwenye Mkesha wa Mwenge wa uhuru uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Makongolosi Agosti 24 mwaka huu, Mzava alisema kuwapatia leseni wachimbaji wadogo ni kurasimisha na kuongeza mnyororo wa thamani kwa vijana walioamua kujiajiri kupitia sekta hii ya madini.

“Ninyi viongozi wetu wa Wilaya mmetafsiri maono ya Mhe. Rais kwa vitendo kwa kuwapatia leseni kundi hili la vijana ili waweze kujikwamua kiuchumi kupitia shughuli ya uchimbaji na hii ndio dhana ya uwezeshaji Vijana kiuchumi” alisema Mnzava.

Mzava aliwahimiza Viongozi wa Wilaya kuwawezesha mitaji wachimbaji wadogo kupitia kundi la vijana ili kuongeza mnyororo wa thamani kwenye sekta ya madini ambayo ni chanzo kimojawapo cha kuingiza mapato kwenye Wilaya hiyo.

Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya jamii, Bi Marietha Mlozi  akisoma taarifa ya mpango maalum  wa urasimishaji wa wachimbaji wa dogo katika sekta ya madini  kwenye sherehe za Mwenge alisema, vijana  watapata manufaa mbalimbali ikiwemo kujiajiri na kuweza  kuajiri vijana wengine na kujiongezea kipato.

“Kupitia Programu maalum ya urasimishaji kwa wachimbaji wadogo  kutawawezesha vijana hawa kunufaika  moja kwa moja na rasirimali za Taifa na kuwezesha kuwa na maeneo ya uhakika ya uchimbaji wa madini” alisema Mlozi

Mlozi aliongeza kuwa, mpango wa urasimishaji kwa wachimbaj utawawezesha kupata mikopo ya riba nafuu pamoja na kujitegemea kufanya shughuli hii ya uchimbaji kwa ufanisi.

Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Chunya umekimbizwa umbali wa kilometa 287.4 na miradi mbalimbali yenye thamani ya shilingi milioni mia nane imezinduliwa, kutembelewa na miradi mingine  kuwekewa mawe ya msingi.

Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya jamii, Bi Marietha Mlozi  akisoma taarifa ya mpango maalum  wa urasimishaji wa wachimbaji wa dogo  kwa kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa 2024 ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava

kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2024 kitaifa ndugu Godfrey  Eliakimu Mnzava akipokea taarifa ya mpango maalum wa urasimishaji wachimbaji wadogo  kutoka kwa Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii bi Marietha Mlozi Wilayani Chunya wakati wa Mkesha wa Mwenge wa Uhuru .



Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.