• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KILIO CHA GHARAMA ZA UCHIMBAJI VISIMA VYA MAJI CHUNYA CHATUA BUNGENI LEO

Imewekwa: November 8th, 2023

Gharama kubwa za uchimbaji wa visima vya maji kupitia mitambo ya serikali iliyonunuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuwarahisishia wananchi kupata maji zimetua Bungeni leo kupitia Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe Masache Njelu Kasaka baada ya kuhoji ukubwa wa Gharama  ya kutumia mitambo hiyo ukilinganisha na Mitambo Binafsi ya uchimbaji wa visima wilayani Chunya


Mhe Masache ameiuliza serikali kupitia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo 8/11/2023 katika bunge linaloendela jiji Dodoma kwamba uchimbaji wa Maji kupitia mitambo ya serikali imekuwa na gharama kubwa kuliko mitambo ya Taasisi Binafsi suala ambalo sio lengo la Serikali huku akiitaka serikali kutazama upya bei hizo ili lengo la Serikali inayoongozwa Na Mhe Dkt Samia suluhu Hassan la kumtua Mama Ndoo Kichwani litimie wilayani Chunya


“Serikali imekuwa na nia njema kuendela kutatua changamoto ya maji hasa kwenye maeneo yetu na imeweza kununua magari ya kuchimba visima na kuyagawa kwenye mikoa yetu, lakini Changamoto ni gharama kubwa ambayo inajitokeza pale taasisi za serikali zinapotaka kuyatumia magari hayo je ni upi mwongozo wa Serikali unaoelekeza matumizi ya magari haya gharama ziwe chini kuliko wachimbaji Binafsi?” Mhe Masache aliuliza


Naibu waziri wa maji Mhe Maryprisca Mahundi amesema Lengo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ni kuona watu wanatumia mitambo hii kutatua kero ya Maji hivyo serikali itaangalia uwezokano wa bei kupungua kiasi cha Taasisi na wananchi kumudu na hatimaye kuendelea kuitumia mitambo hiyo kutatua changamoto za maji maeneo yao


“Mhe Naibu Spika hizi gharama ni kutokana na ubora wa kazi unaofanywa na wataalam wetu, unaweza kuchimbiwa kwa gharama ndogo na mtu binafsi lakini baada ya muda  unaanza kulalamika unapata maji yaliyo chini ya ubora  lakini sisi gharama zetu zinaonekana kubwa lakini ubora wa maji na sababu ni kwamba sisi tunaweza kwenda chini  mita 200 ndo maana tunakuchaji milioni 20, mtu binafsi anaweza kwenda mita 70 na akakuchaji milioni tano ukaona ni ni rahisi  kwahiyo ubora wa maji unaenda kwa kutofautina na hapo ndipo gharama inapokuwa kubwa , lakini kwa kuzingatia Mhe Rais anahitaji kuona magari haya yanaendelea kutumiwa na watu wengi tutaendeleo kuona kadiri tuwezavyo gharama inakuwa rafiki” alijibu Naibu waziri wa Maji Mhe Mahundi


Ikumbukwe hivi karibu Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka  katika kikao cha Kawaida cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Chunya alisema Uchimbaji wa Maji kupitia mitambo iliyonunuliwa na Mhe Rais ili kuwasaidia wananchi wa Tanzania wakiwepo wanachunya imekuwa kubwa kuliko mitambo ya watu binafsi na kuagiza wahusika kufika ofisini kwake kuzungumia suala hilo ili kuona uwezekano wa kupendekeza kwa mamlaka zinazohusika kutazama suala hilo ili mitambo hiyo iwasaidie wananchi wengi zaidi kama ambavyo serikali inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassani ilivyokusudia


Kilio hicho cha gharama za kutumia mitambo ya serikali kuchimba visima vya maji kufika Bunge la Jamhuri ya Muunganmo wa Tanzania kupitia mwakilishi wa wanachunya kwenye Bunge hilo inaonesha namna ambavyo viongozi wa wilaya ya Chunya wanavyohangaika kwa pamoja kuhakikisha kero za wananchi wa wilaya ya Chunya zinaptiwa majibu kwa wakati


Bunge linaendelea na vikao vyake vyenye lengo la kujadili ripoti ya Mdhibi na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) na kuanza maandalizi ya Mpango wa Serikali kwaajili ya mwaka wa fedha ujao ambapo wananchi wa wilaya ya Chunya (ambalo ni Jimbo la Uchaguzi la Lupa) wanawakilishwa na Mbunge wa Jimbo hilo  la Lupa Mhe Masache Njelu kasaka.

Mbunge wa Jimbo la Lipa Mhe Masache Njelu Kasaka akiuliza swali mapema leo Bungeni kuhusu gharama za uchimbaji wa visima kutumia mitambo ya serikali

Naibu waziri wa Maji Mhe Maryprisca Mahundi akijibu swali la Mhe Mbunge wa Jimbo la Lupa mapema leo

Mbunge wa Jimbo la Lupa Mhe Masache Kasaka (Wa katikati) akisikiliza kwa makini majibu ya Naibu waziri wa Maji kuhusu kero ya gharama kubwa za kutumia mitamvo ya serikali ya kuchimba maji ukilinganisha na mitambo Binafsi

Picha ikionesha Bunge la Jamhuri ya Munngano wa Tanzania likiendelea na shughuli zake Jijini Dodoma mapema leo 

Mitambo (Magari) yanayolalamikiwa kutoza gharama kubwa katika uchimbaji wa visima vya maji ukilinganisha na mitambo au magari Binafsi kwa Mkoa wa Mbeya mitambo hii iko wilayani Chunya kwa sasa

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.