• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KESI ZA UBAKAJI NA ULAWITI SIO ZA MAELEWANO

Imewekwa: February 2nd, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mh. MAYEKA SIMON MAYEKA amewataka wananchi waliojitokeza katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria kutofumbia macho kesi za ubakaji na ulawiti kwakuwa zinaathari mbaya kwa jamii kwani athari zake zinadumu kwa muda mrefu

Mayeka ametoa kauli hiyo (jana) katika kilele cha hitimisho ya wiki la sheria wilayani Chunya hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) ambapo yeye alikuwa mgeni rasmi na maewaonya viongozi na wananchi waliojitokeza kuepuka maelewano katika kesi za ulawiti na ubakaji kwani zina athari kubwa kwa jamii

“Msitake maelewano katika kesi za namna hii, mtoe ushirkiano mapema, tuchukue hatua mapema ili haki itendeke. Hasa viongozi wetu wa vijiji wanashawishika kufanya mazungumzo na mara nyingi ni pale aliyefanya ni ndugu”

Aidha Mayeka ameendelea kuhimiza jamii kukataa, kupinga na kuzuia mila na maadili potofu kuwafikia watoto wetu kwa nguvu zetu zote kwani kinyume na hapo siku zijazo tutakuwa na Taifa la hovyo, lisilo na maadili, Hivyo ni jukumun letu sote kuhakikisha tunalinda maadili yetu kama nchi

Katika kuhitimisha hotuba yake Mayeka ameendelea kuhimiza wazazi na walezi wote wilayani Chunya kuhakikisha watoto waliochaguliwa kujiunga na masomo katika shule za sekondari wapelekwe shule, huku akiwataka Mahakimu kuendelea kuwashughulikia wazazi wanaogoma kuwapatia watoto haki za msingi ikiwepo kuwapatia elimu

Awali akitoa taarifa Mbele ya Mgeni rasmi Hakimu Mkazi Mfawidhi wa wilaya ya Chunya James Julius Mhanusi amesema katika maadhimisho ya wiki ya sheria wilayani chunya wamefanya shughuli mbalimbali ikiwepo kutoa elimu katika shule mbalimbali za sekondari na msingi zilizopo wilayani Chunya pia wametembelea wananchi katika kata mbalimbali ili kuwapelekea elimu ya sheria za nchi

Hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya ya chunya amesema kasi ya usikilizaji wa kesi wilayani chunya ni mzuri kwani kesi nyingi zimepatiwa ufumbuzi kwa wakati hivyo kuwarahisishia wananchi kwanza kuepukana na gharama za kufika mahakamani mara kwa mara lakini pia kumaliza kesi kwa wakati kunasaidia wananchi kupata muda wa kuendelea na shughuli za uzalishaji mali

Mhanusi ameongeza kuwa Mahakama ya wilaya ya Chunya pamoja na uwepo wa hakimu mmoja wa mahakama hiyo lakini imesikiliza zaidi ya mashauri 464 kati ya mashauri 560 ambapo mashauri yaliyofunguliwa mwaka 2022 na yale machache ambayo walivuka nayo mwaka 2021.

Kwakuhitimisha hotuba yake mbela ya Mgeni rasmi, Hakimu mkazi mfawidhi amewataka wadau wote wa mahakama wilayani chunya kuendelea kuwa na Imani na mahakama zote wilayani humo kwani wao wataendelea kutekeleza jukumu lao kikamilifu kila wakati

 Maadhimisho ya wiki ya sheria wilayani chunya yamefanyika kuanzia tarehe 22/01/2023 mpaka tarehe 29/01/2023 ambapo shughuli mbalimbali zimefanyika katika maeneo tofauti tofauti ndani ya wilaya huku kilele chake kikiwa ni tarehe 01/02/2023, Kauli mbiu ya maadhimisho ya wiki ya Sheria mwaka 2023 ni “Umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi katika kukuza uchumi endekevu; Wajibu wa Mahakama na wa

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.