• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KATIBU TAWALA AWATAKA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI ZINGINE KWENDA KUJIFUNZA CHUNYA.

Imewekwa: January 10th, 2025

Katibu tawala Mkoa wa Mbeya ndugu Rodrick Mpogolo amewataka wakurugenzi watendaji wa Halmashauri zingine za Mkoa wa Mbeya kwenda kujifunza katika Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  kujua ni kwa namna gani Halmashauri hiyo imefanikiwa kupima maeneo yote ya taasisi ili na wao waweze kufanya hivyo katika maeneo yao kwani kufanya hivyo ni kutekeleza adhima ya serikali ya kuhakikisha maeneo yote ya taasisi yanapimwa .

Kauli hiyo ameisema leo Tarehe 10 Desemba 2024 alipokuwa akikagua ujenzi wa shule mpya ya sekondari katika kata ya Nkung’ungu wakati alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali  ya elimu inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

“Chunya mnastahili pongezi na niwatake wakurugenzi wengine waje Chunya wajifunze ni kwanini Chunya wameweza kupima maeneo ya tasisi na sasa hivi wako kwenye mchakato wa kuyakatia hatimiliki wakati Halmashauri zingine ukiwauliza swali hili ni mtiani kwao ,  Afisa elimu utanisaidia kupata takwimu za hali ya upimaji wa taasisi kwenye halmashauri ya wilaya ya chunya na tuwatake wakurugenzi wengine waje wajifunze chunya  ,maana hili ni agizo la serikali kuhakiisha maeneo yote ya taasisi za serikali yanapimwa na kuwa na hatimiliki.alisema “.Mpogolo

Aidha Katibu Tawala ametoa siku 14 kuhakikisha miradi wa Ujenzi wa shule Mpya ya Sekondari kata ya Nk’ungu’ngu , Ujenzi wa mabweni 2 na vyumba 6 vya madarasa ,  ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na matundu 6 ya vyoo Shule ya Msingi Mtande pamoja na ujenzi wa  matundu  19 ya vyoo Shule ya Msingi Makongolosi unakamilika  huku akiwataka kuongeza rasilimali watu ili kuhakikisha kazi zilizosalia zote zinakamilika

Kaimu Afisa elimu Mkoa wa Mbeya ndugu Robert Mfugale  ametoa rai kwa Afisa elimu na  wataalamu Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kuhakikisa kazi zilizosalia zinakamilika kwa wakati uliopangwa ili kuwaondolea adha wanafunzi watakoporejea Shuleni kwani serikali imetoa pesa nyingi kwaajili ya  ujenzi wa miradi mbalimbali ili kutatua changamoto kwa wananchi.

Afisa Mipango na uratibu Mkoa wa mbeya ndugu Juma Maduhu pamoja na Mkadiriaji wa mejengo QS. Issa Jabiri kwa pamoja wametoa msisitizo kwa wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya pmbali na kukimbizana na muda wanapaswa  kuhakikisha taratibu zote za ujenzi zinazingatia viwango vinavyotakiwa   pamoja na kuhifadhi nyaraka zote za  utekelezaji wa miradi .

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Ndugu Tamimu Kambona amekiri kuyapokea maaggizo na maelekezo yote yaliyotelewa  na Katibu tawala Mkoa wa Mbeya pamoja na wataalamu wake na kuhaidi kuyafanyia kazi kwa wakati uliopangwa kwa kuzingatia Viwango na ubora  wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Diwani wa Kata ya Nk’ungu’ungu Mhe Aden Tajak  mbali na kumushukuru Mhe. Rais  ametoa shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Chunya  na Wananchi wa kata hiyo kwa Ushirikiano  na usimamizi mkubwa wanaowapa katika kuhakikisha Shule hiyo inakamilika  kwani kukamilika kwa Shule hiyo kutawapunguzia adha wanafunzi waliokuwa wakitembea umbali wa kilometa 12 kwaajili ya kwenda kusoma katika Shule ya Sekondari iliyopo kata ya Lupa.

Katika ziara hiyo ya katibu tawala Mkoa wa Mbeya ametembelea miradi yenye thamani Zaidi ya billion moja na kukagua hatua iliyofikiwa  na mambo mengine  ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Shule mpya ya sekondari kata ya N’kung’ungu, Ujenzi wa Vyumba vya madarasa na vyoo shule ya Msingi Mtande, Ujenzi wa Mabweni na vyumba vya madarasa Shule ya Sekondari Makongolosi Pamoja na ujenzi wa vyoo  Shule ya Msingi Makongolosi.

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya ndugu Rodrick Mpogolo akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi Mtande kata ya Mamba Wilayani Chunya.

Kaimu Afisa elimu Mkoa wa Mbeya ndugu Roberth Mfugale akitoa rai juu ya kuzingatia muda wa ukamilishwaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na Matundu ya Vyoo katika miradi mbalimbali ya elimu Wilayani Chunya.

Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Eng Charles Kway akitoa ufafanuzu kwa katibu Tawala wa Mkoa  ndugu Rodrick Mpogolo walipotembelea na kukagua ujenzi wa shule ya sekondari kata ya Nku'ng'ungu  Wialayani Chunya


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.