• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO IMERIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI CHUNYA

Imewekwa: October 9th, 2024

Kamati ya Fedha, Uongozi na mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Chunya imeridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Chunya huku usimamizi mzuri wa Mkurugenzi Mtendaji pamoja na wataalamu wengine ukitajwa kuwa ndio sababu ya miradi hiyo kutekelezwa vizuri.

Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Mhe. Bosco Mwanginde akizungumza kwa niaba ya kamati ya hiyo mapema Oktoba 7, 2024 katika viwanja vya Shule ya Msingi Chemichemi iliyopo kata ya Chalangwa amesema kamati hiyo imeridhishwa na kasi ya mradi huo wa ujenzi wa madarasa mawili na ofisi moja katika shule hiyo.

“Kamati ya fedha na mipango imeridhishwa na kasi ya utekelezaji wa ujenzi wa shule ya Chemichemi, Halmashauri itasaidia pale mulipokwama kupitia mapato ya ndani kukamilisha ujenzi” amesema Mhe. Mwanginde.

Aidha, Kamati hiyo kupitia mwenyekiti wa kamati iliagiza uongozi wa kamati ya ujenzi wa shule ya msingi Chemichemi kuhakikisha wanakamilisha mradi huo ambapo wameagizwa kwamba ifikapo mwezi Disemba 2024 mradi uwe umekamilika na kwakufanya hivyo  kutaongeza tija kwa wanafunzi kuendelea na masomo lakini kupokea wanafunzi wengine mwaka ujao.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa madarasa hayo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi ChemiChemi Mwalimu Crispin Laurent Lugwira amesema anaipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa kutoa fedha Shilingi millioni saba kwenye ujenzi wa majengo mawili na Ofisi moja katika shule hiyo huku akibainisha kazi zilizobaki kuwa ni kupiga lipu, kubeba mchanga kwaajili ya sakafu, kupaka rangi na kununua samani ikiwemo madawati.

“Tunawapongeza Halmashauri kwa kutuletea fedha za ujenzi na kazi inaendelea kazi tulizonazo kwa sasa ni kupiga lipu, kubeba mchanga kwaajili ya sakafu, kupaka rangi pamoja na kununua madawati ” amesema Lugwira.

Akifafanua baadhi ya hoja kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Chunya, Mkuu wa Idara ya elimu Awali na msingi Mwalimu Ferd Mhanze amesema idara ya elimu msingi itachangia mafuta ya gari lita 100 ili kurahisisha uchukuaji wa mchanga kujaza kwenye msingi wa vyumba vya madarasa mawili ambapo juhudi hizo zitasaidia kuharakisha ukamilishwaji wa mradi kwa wakati.

Kamati ya Fedha imefanya ziara yake ya kawaida kwa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/2025 kukagua miradi ya Maendeleo ambayo inatekelezwa na Halmashauri ya wilaya ya Chunya ili kushauri au kutafuta namna sahihi ya kuhakikisha miradi itekelezwa kwa viwango, kwa wakati na kwa ufanisi kulingana na thamani ya fedha zilizotolewa na Serikali.

"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"

Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi ChemiChemi Mwalimu Crispin Laurent Lugwira akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi mbele ya Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati kamati hiyo ilipotembelea Shuleni hapo kukagua maendeleo ya ujenzi

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakiambatana na wataalam kutoka Halmashauri wakifuatilia kwa karibu maelezo kuhusu utekelezaji wa mradi katika Shule ya Msingi Chemichemi iliyopo kata ya Chalangwa


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.