• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

HESHIMUNI MPANGO WA MATUMIZI BORA YA ARDHI KATIKA MAENEO YENU

Imewekwa: February 7th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaji Batenga amewataka wananchi wa wilaya ya Chunya kwa ujumla kuheshimu mpango wa matumizi bora ya Ardhi akidai ndio njia pekee na sahihi ya kuepusha migororo ya ardhi katika maeneo ya vijiji na kata ndani ya ya wilaya ya Chunya

Ametoa kauli hiyo jana tarehe 6/2/2024 katika mkutano wa Hadhara na wananchi uliofanyika kata ya Lualaje, kijiji cha Lualaje ikiwa ni kawaida yake kuongozana na watalamu kutoka idara na vitendo mbalimbali kwenda kujibu kero za wananchi katika maeneo ya vijiji na kata wanazoishi

“Ndugu wananchi kila kitu kina utaratibu wake, heshimuni mpango wa matumizi bora ya ardhi na watu wa kwanza kabisa kuheshimu mpango wa matumizi bora ya ardhi ni viongozi kuanzia ngazi ya chini kabisa ya uongozi mpaka ngazi ya juu” alisema Batenga

Aidha Mhe Batenga amewakumbusha wananchi wa wilaya ya Chunya kwamba Mkutano mkuu wa kijiji umepewa uwezo wa kumilikisha ardhi yenye ukubwa wa heka 50 tu, hivyo amewataka kuzingatia hilo ili kuepuka migogoro mbalimbali inayojitokeza ambayo imekuwa kero na inakwamisha maendeleo ya vijiji kwani muda mwingi unatumika kutatua migogoro

“Mkutano Mkuu wa kijiji una uwezo wa kupitisha umiliki wa ardhi yenye ukubwa wa heka 50 tu na sio vinginevyo, Hatuwezi kuendelea kutengeneza migogoro ya ardhi katika vijiji vyetu, sisi Chunya atakaye kiuka sharia, taratibu na miongozo ya ardhi tutamchukulia hatua kali” alisema Batenga

Diwani wa kata ya Lualaje Mhe Tusalim Mwaijande pamoja na kushukuru miradi mikubwa iliyojengwa katika kata hiyo ambayo ni pamoja na shule ya sekondari Lualaje, Daraja la Lualaje na maeneo mengine mengi amesema kata itawachukulia hatua wazazi wote ambao mpaka sasa hawajawapeleka watoto wanaotakiwa kuanza kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Lualaje.

“Tutawakamata wale wote ambao hawapeleki watoto shule, hatuwezi kujenga miradi kwa gharama kubwa alafu wazazi mshindwe kupeleka watoto shule sisi tutawakamata na kuwachukulia hatua kali” Alisema Mhe Mwaijande

Kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi kata ya Lualaje Katibu kata wa Chama hicho ndugu Subira Msindo amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ameitendelea haki Ilani ya Chama cha Mapinduzi kata ya Lualaje maana katika kipindi kifupi cha uongozi wake kata imepata Sekondari, Daraja zuri, wahudumu kwenye Zahanati zao, Walimu pamoja na mambo Mengine mengi

Diwani wa kata ya Lualaje Mhe Tusalim Mwaijande akitoa salamu za Kata na kuelezea Miradi mbalimbali iliyotekelezwa na Serikali ya awami ya sita katika kata ya Lualaje mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya pamoja na wananchi walio udhuria katika mkutano wa Hadhara

Baadhi ya Wananchi wa Kata ya Lualaje walio hudhuria Mkutano wa Hadhari wa Mkuu wa wilaya wenye Lengo la Kusikiliza na kutatua kero zinazo wakabili wananchi

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.