• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

“HATUWEZI KUKUBALI MUHARIBU FEDHA ZA SERIKALI WAKATI SISI TUPO, TUTAMUWAJIBISHA MTU”

Imewekwa: October 3rd, 2023


Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Baraza la madiwani Halmashauri ya wilaya ya Chunya imewatahadharisha watumishi wanaoshindwa kusimamia fedha za serikali zinazoletwa wilayani Chunya kwaajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo jambo linalopelekea miradi kushindwa kukamilika kwa wakati na wakati mwingine kukosa ubora unaokusudiwa na serikali


Akizungumza kwa niaba ya kamati hiyo nyakati tofauti tofauti mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Bosco S Mwanginde amesema watawawajibisha mara moja watumishi ikibainika kuna matumizi yasiyofuata muongozo wa matumizi ya fedha, utekelezaji wa miradi chini ya kiwango na hata miradi kukosa ubora unaostahili


“Ninyi watumishi na viongozi wa serikali mnaosimamia miradi yetu hakikisheni mnasimamia kwa weledi sisi kama kamati hatuwezi kukubali muharibu fedha za serikali au msimamie hovyo hovyo au mtekeleze mradi chini ya kiwango lazima tutawawajibisha mara moja maana serikali inapoleta fedha huku lengo lake ni kutatua kero za wananchi lakini mkisimamia vibaya maana yake tutashingwa kutatua kero za wananchi” alisema Mwenyekiti wa kamati


Aidha kamati hiyo imetoa maagizo mbalimbali kulingana na mradi husika ambapo baadhi ya maagizo hayo ni kuondoa dawati ambazo hazina viwango ili ziletwe zenye viwango sawa na maelekezo ya serikali, bei ya samani lazima izingatie uhalisia kutoka eneo moja na eneo lingine, lakini pia mafundi ambao hawajakamilisha utekelezaji wa miradi yao wasilipwe mpaka watakapokamilisha kazi zao


Kamati pia imeagiza trekta la Halmashauri ya wilaya pamoja na Lori kupelekwa mara moja kambikatoto ili kupunguza gharama za kubeba mchanga, Kuchota maji pamoja na kubeba mawe ili kuharakisha ujenzi wa shule ya sekondari inayojengwa katika kata hiyo kwani lengo la serikali ni ifikapo Januari mwaka 2024 lazima Shule hiyo ianze


Kamati hiyo ipo kwenye ziara ya Robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/2024 Julai-Septemba ambapo miradi yenye thamani ya shilingi bilioni moja na milioni mia tisa (1,953,104,028) imekaguliwa kwa siku mbili, bado ziara inaendelea siku ya tatu ili kuhitimisha ziara hiyo ambapo kwa siku ya leo tarehe 4/10/2023 kamati itatembelea miradfi yenye thamani ya shilingi milioni mia mbili kumi na mbili (212, 000,000)

Wajumbe wa kamati ye Fedha, Uongozi na Mipango wakiendelea na ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa shule Mpya ya Msingi Kipembawe inayojengwa katika kata ya Mafyeko

Mwenyekiti wa kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Mhe Bosco S Mwanginde 9Aliyeshika Fimbo katika na akionekana akizungumza kwa ishara) wakati akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri hiyo

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Mhe Bosco Mwanginde (Aliyeshika Ubao kwa mkono wake wa kulia) akikagua namna ubao wa shule ya msingi Kipembawe ulivyowekwa tayari kwa matumizi. Aliyeshika ubao kwa Mkono wa Kushoto ni Diwani wa Kata ya Mafyeko Mhe. Geofrey  Z. Kamaka

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.