• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Halmashauri Chunya yaingiza 4.1bn/- robo tatu 2021/22

Imewekwa: May 14th, 2022

HALMASHAURI ya Wilaya ya Chunya imefanikiwa kuingiza kiasi cha shilingi bilioni 4.1 kutokana na mapato ya ndani kwa kipindi cha robo tatu cha mwaka wa fedha unaoelekea ukingoni 2021/22.

Mapato hayo yaliyoingizwa katika kipindi cha miezi mitatu kutoka Januari hadi Machi mwaka huu, ni sawa na asilimia 86 ya malengo ya ukusanyaji mapato katika Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kilichofanyika Machi 13, 2022, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bosco Mwanginde amesema, dhumuni la kikao hicho ni kujadili mipango mbalimbali ya kimaendeleo ambayo wamejiwekea kwa utaratibu wa kila baada ya miezi mitatu.

“Naomba kuwaomba viongozi wenzangu kushirikiana na wataalam wetu katika kusimamia shughuli za maendeleo kwa uadilifu, uaminifu na ufuatiliaji wa karibu ili shughuli hizo za kimaendeleo ziweze kufanyika vizuri,” alisema Mwanginde.

Aidha, aliwaasa waheshimiwa madiwani na wataalam kuepuka kuanzisha migogoro isiyo ya lazima katika miradi wanayoisimamia.

Katika muda wa maswali ya papo kwa hapo, Mhe. Benson Msomba Diwani wa Kata ya Kasanga aliulizia mpango wa Halmashauri kuhusu kuhamisha machinjio yaliyozungukwa na makazi ya watu kutokana na kukua kwa mji.

Akijibu swali hilo Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Mwanginde amesema, Halmashauri ya Wilaya ya Chunya imetenga eneo la machinjio ya kisasa katika kijiji cha Kibaoni ambapo halmashauri imepanga kutenga bajeti kwaajili ya kuanza hatua za awali za ujenzi wa machinjio hiyo.

Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Mhe. Mwanginde amewataka waheshimiwa madiwani pamoja na wataalam wa Halmashauri kuhakikisha wanakusanya mapato kwa wingi ili kutimiza malengo waliyojiwekea.

“Hatuwezi kwenda na Halmashauri haiwezi kuendelea bila kuwa na mapato ya ndani, rai yangu kwenu waheshimiwa haya mambo yote tunayoyajadili hapa mapato ya ndani makusanyo yanatoka kwenye kata zetu twendeni tukashirikiane na wataalam wetu kukusanya mapato."

“Sisi kama madiwani ni wajibu wetu kuwa karibu na hii miradi, mradi ule ukiwa kwenye kata yako na ukausimamia vizuri unakupa heshima na wewe kwa sababu hautakuwa na ubadhirifu na hautajengwa kwa kiwango cha chini." Alisema Mwanginde.


Mhe. Ramadhan A. Shumbi makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya chunya akiwasilisha taarifa ya Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango kwenye kikao cha baraza la madiwani kwa robo ya tatu.

Mh Anaklet Michombero katibu tawala wa wilaya ya chunya ambaye alimwakilisha Mkuu wa wilaya akitoa salamu za Mkuu wa wilaya kwenye kikao cha Baraza la Madiwani

Waheshimiwa madiwani wakiwa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya Tatu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya chunya Mh Bosco Mwanginde akifafanua jambo kwenye kikao cha Baraza la Madiwani

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.