• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

FAIDA MNAYOPATA LAZIMA IONEKANE KWENU NA KWA JAMII YENU

Imewekwa: January 15th, 2024

Kamati ya Fedha, Uchumi na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya imewataka wanawake, vijana na wale wenye ulemavu walionufaika na mkopo wa asilimia 10 ambazo  ni fedha za serikali zinazotokana na mapato ya Ndani  kuhakikisha matunda ya  kukopeshwa kwao yanaonekana kwa walengwa kwanza na baadaye kwa jamii inayowazunguka kwakufanya hivyo mtakuwa mmetiza lengo la serikali la kuwainua wananchi wake kiuchumi

Hayo yametolewa mwishoni mwa juma wakati kamati ya Fedha, Uchumi na Mipango ilipotembelea kikundi cha Wanawake Jamii kilichopo kata ya Lupa ili kujionea shughuli zinazofanywa na kikundi hicho tangu kilipoanza kukopeshwa na Halmashauri ya wilaya ya Chunya mwaka 2019 kwa fedha zinazotengwa kwaajili ya kuwakopesha vijana wanawake na wenye ulemavu maarufu kama asilimia kumi

“Kile mnachokipata kama faida lazima tukione kwenu kama wanakikundi na baadaye tukione kwa jamii inayowazunguka, nje ya hapo maana ya lengo la ninyi wanawake, vijana na wenye ulemavu la kukopeshwa na Serikali inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan litakuwa bado halijatimia hivyo lazima tuone mabadiliko kwanza kwenu ninyi wenye na baadaye jamii yenu” Amesema Mhe Shumbi

Kamati hiyo pia imewapongeza wanawake wa kikundi hicho kwakurejesha fedha walizokopeshwa lakini pia kwa namna ambavyo hawakukata tamaa baada ya mradi wa kufuga kuku kushindwa kuendelea kutokana na changamoto mbalimbali na kuamua kuhamia  kwenye mradi wa kufuga Nyuki huku lengo lao likibaki kuwa la kujikwamua kiuchumi

Kamati hiyo imewashauri  kikundi cha wanawake Jamii kuona uwezekano wa kumiliki misitu yao wenyewe ili kurahisisha utekelezaji wa mradi wao wa ufugaji wa Nyuki jambo litakalo wasaidia kukabiliana na changamoto za uharibifu wa mazingira unaotokana na shughuli za kibinadamu kwenye misitu mbalimbali ambayo ndiyo hutumika kama maeneo yao ya kuweka mizinga

Wakati akitoa taarifa ya miradi wa kikundi hicho mwenyekiti  wa kikundi Bi Vumilia Kilindu amesema faida wanazopata wanakumbuka kurudisha kwa jamii inayowazunguka kwani mpaka sasa wamechangia mifuko kumi ya saruji katika ujenzi wa shule ya Msingi Lupatingatinga, wametoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya laki tano (500,000) kwa wanafunzi wasiojiweza kwenye shule ya msingi Lupatingatinga na wataendeleo kufanya hivyo

Akitoa salamu za Shukrani kwa kamati hiyo Mhasibu wa kikundi hicho Bi Delista Hyera ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwanza kuwakopesha fedha na kuendelea kuwapa ushauri wa mara kwa mara, pamoja na kutembelewa na maafisa maendeleo ya Jamii lakini amesema ushauri na maelekezo ya kamati hiyo wameupokea kwa dhati na wataufanyia kazi ili waendelee kufanya vizuri zaidi

Kikundi hicho mpaka sasa kina jumal ya wanachama 16, kina miliki mzinga Zaidi ya mia mbili ambapo 151 tayari imewekwa katika msitu mbalimbali na 57 iko tayari muda si mrefu itapelekwa kwenye msitu wa Inyonga ulioko kata ya Mafyeko na huwa wavuna karibu lita mia tano za asali na kuziuza hatimaye kuboresha maisha yao kama wanakikundi na baadaye  kurudisha kwa jamii inayowazunguka

Mjumbe wa kamati ya Fedha Uchumi na Mipango Mh. Benson B. Msomba Diwani wa Kata ya Kasanga akichangia jambo mbele ya wana Kikundi cha ufugaji wa Nyuki kilicho Lupa

Mh. Phide K. Mwalukasa mjumbe wa kamati ya Fedha, Uchumi na Mipango Halmashauri ya wilaya ya Chunya akichangia jambo wakati kamati hiyo ilipotembelea kikundi cha wanawake jiamini kilichopo Lupa

Bi Vumilia Kilindu Mwenyekiti wa miradi wa kikundi cha wanawake Jiamini akisoma taarifa ya kikundi mbele ya Kamati ya Fedha, Uchumi na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya pindi walipotembelea kuona maendeleo ya kikundi hicho

Bi Delista Hyera ambaye ni Mhasibu wa kikundi cha Mwanamke Jiamini kilichopo Lupa akitoa shukrani zake kwa kamati ya Fedha, Uchumi na Mipango walipotembelea kukagua maendeleo ya kikundi hicho ambapo ni wanufaika wa mikopo ya asilimia kumi

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.