• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DED CHUNYA "MMETUWAKILISHA VIZURI, MATOKEO TUMEYAONA"

Imewekwa: November 2nd, 2023

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona amezipongeza timu za Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwa uwakilishi mzuri katika mashindano yaliyoandaliwa na shirikisho la michezo Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) yaliyofanyika jijini Dodoma.


Ametoa pongezi hizo leo tarehe 02 November, 2023 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya uliopo jengo jipya la utawala wakati akikabidhiwa vikombe pamoja na medali za ushindi kutoka kwa timu za Halmashauri ya Chunya zilizoshiriki Michezo Mbalimbali  SHIMISEMITA iliyotamatika hivi karibuni Jijini Dodoma.


“Niwapongeze wote ambao mmekwenda Dodoma kwenye mashindano haya mmeshiriki na matokeo yake tumeyaona niwapongezeni sana kwa hilo  na sasa Tujipange kwa Mwaka unaokuja tufanye maandalizi ya kutosha ili tukafanye vizuri zaidi, tumesha anza kutengeneza uwanja wetu wa mpira pale (Mbugani) na lengo tuwe na uwanja waFootball,  Netball, Volleyball pamoja na Basketball yaani tuwe na viwanja vyote” alisema Kambona


Pia Kambona amemwagiza Mkuu wa Idara ya Utumishi Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuhakikisha Idara na vitengo vyote vinatenga bajeti za michezo kwa mwaka 2024/2025 ili kuhakikisha timu yetu inashiriki michezo yote kwa mashindano ya SHIMISEMITA mwaka 2024


 “Afisa Utumishi kwenye bajeti ya Mwaka ujao tukubaliane sasa kila idara  zitenge fedha za michezo ili kurahisisha ushiriki wa timu yetu kwa kipindi kijacho au tukiona inafaa tupunguze bajeti za idara na vitengo ili fedha zote za michezo zikae kwa Mkurugenzi kwa maana ya utawala ili muda ukifika tunakuwa na uhakika wa bajeti”.


Awali akitoa taarifa ya safari iliyodumu kwa siku 14 kiongozi wa msafara huo ambaye pia ni mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii Ndugu Vicent Msolla pamoja na kumshukuru Mkurugenzi mtendaji kwa namna alivyowawezesha kushiriki mashindano hayo ameomba kuendeleza mazoezi pamoja na kupata Makocha wenye weledi wa kuwaongoza katika mazoezi hayo jambo litakaloleta mafanikio makubwa zaidi mwaka ujao.


Timu za halmashauri ya wilaya ya chunya zimeshiriki michezo mbalimbali ikiwemo Mpira wa miguu kwa wanaume, mpira wa pete wanawake, mpira wa Mikono Handball kwa Wanaume na wanawake, Mchezo wa Kuvuta kamba wanaume na wanawake, Kurusha Tufe wanaume na wanawake, Riadha, Karata pamoja na Mchezo wa Bao..


 Halmashuri ya wilaya ya Chunya katika mashindano ya SHIMISEMITA 2023 imefanikiwa kutwa makombe mawili (2) na Medali Moja (1) Kuvuta kamba Wanaume Mshindi wa kwanza, Kuvuta kamba Wanawake Mshindi wa Tatu na kurusha Tufe Mshindi wa Tatu kwa Upande wa Wanaume

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona (kulia) akikabidhiwa Cheti cha Ushiriki wa SHIMISEMITA 2023 na Kiongozi wa Msafara Ndugu Vicent Msolla

Ridhawani Mshighati Kepteni wa timu ya wanaume kuvuta kamba na mwakilishi wa timu ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya Kurusha Tufe akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji Medali ya ushindi wa Tatu kurusha Tufe

Kepteni Msaidizi wa timu ya wanawake kuvuta kamba Bi Joyce Kisula akimkabidhi kombe la mshindi wa tatu kwa timu ya Halamshauri ya wilaya ya Chunya Kuvuta kamba (KE) Mkurugenzi Mtnedaji wilaya ya Chunya

Mkurugenzi mtednaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona akipeana mkono na Ndugu Vicent Msola Kiongozi wa Msafara wa timu ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati wa Hafla ya kukabidhi makombe na medali mapema leo

Mkurugenzi mtednaji Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona (Aliyeshika Makombe) akifurahia ushindi wa timu za Halmashauri katika Mashindano ya SHIMISEMITA 2023 yaliyotamatika Jijini Dodoma (Kushoto kwa Mkurugenzi ni Afisa utumishi na Utawala Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu John Mahalani

Afisa utumishi na Utawala wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu John Maholani (Aliyeshika cheti na Kombe katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi wa Timu iliyoshiriki mashindano ya SHIMISEMITA 2023 jijini Dodoma

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.