• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA”MKAWE MFANO WA KUIGWA KATIKA JAMII”

Imewekwa: November 11th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S.Mayeka amewataka wahitimu wa mafunzo ya jeshi la akiba (mgambo) kuwa mfano wa kuigwa   kutokana  na mambo mbalimbali ambayo wamejifunza  yatakayo wawezesha kuisaidia jamii na Taifa kwa ujumla  ikiwa ni pamoja  ulinzi na usalama, kuwa tayari watakapohitajika  katika mambo mbalimbali ya kujenga Taifa .

Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 11/11/2023 wakati wa  hafla ya kufunga mafunzo ya jeshi la akiba (Mgambo) katika viwanja vya mpira wa miguu  Bitimanyanga katika kata ya Mafyeko yaliyohudhuriwa na washiriki zaidi ya mia moja na sabini (170) na yamedumu zaidi ya siku tisini (90)

“Mkawe mfano wa kuigwa katika jamii kwa kufanya mambo mazuri ya kuisaidia jamii  na kuwa tayari kutekeleza majukum yenu mliyofundishwa pale mtakapohitajika katika  mambo mbalimbali  yanayoweza kujitokeza kama vile uharibifu wa mazingira, mafuriko, ajali na majanga mengineyanayoweza kutokea katika vijiji vyenu na Taifa kwa ujumla” amesema Mh. Mayeka.

Aidha Mhe. Mayeka  amewataka wananchi kuheshimu mafunzo hayo yanapojitokeza kwa awamu nyingine  na kuacha kubeza kwa kutoa maneno yasiofaa kuipotosha jamii  kuhusu mafunzo hayo kwani mafunzo ya Mgambo yapo kwa mujibu wa sheria hivyo watakaoonekana kubeza mafunzo hayo hatua zitachukuliwa zidi yao.

‘’Wananchi mafunzo ya Mgambo ni kwa mujibu wa sheria hata Mhe. Rais anajua Mafunzo haya lakini kuna wananchi hawajui kama kubeza au kutoa maneno yasiyofaa juu ya mafunzo haya ni kinyume na sheria, niombe sana yatakaporudi mafunzo haya kwa kipindi kingine wananchi mjitokeze kwa wingi na wale wanaobeza na kuongea maneno yasiyofaa waache na wajue ni kinyume cha sheria wanaweza wakachukuliwa hatua alisema Mhe. Mayeka”

Naye mwakilishi wa Mshauri wa mafunzo ya Mgambo wa Mkoa Luteni Ngaji Vinac Ipela  amewataka wahitimu wa mafunzo ya Mgambo kwendelea kuwa wazalendo na wakakamavu na wenye utayari wa kuisadia jamii na Taifa pale watakapohitajika kutekeleza majukum yao kwani Taifa linawategemea.

Akisoma risala kwa Mgeni rasmi mmoja ya wahitimu wa mafunzo ya Mgambo ndugu Ramadhani Kasambandege amesema kuwa katika kipindi chote cha mafunzo wameweza kujifunza mambo mbalimbali  kwa nazalia na vitendo ambayo yatawasaidia wao kama viajana  kuweza kujipatia ajira lakini pia kuisaidia jamii inayowazunguka na taifa kwa ujumla .

“ Kwakipindi chote cha mafunzo tumejifunza mambo mbalimbali kama vile ujasiriamali, mbinu za kivita,  huduma ya kwanza , zimamoto na uokoaji, kwata , usomaji wa ramani, utimamu wa mwili, usalama wa raia, kuzuia na kupambana na rushwa, kuzuia wahamiaji haramu na mengine mengi” alisema Ramadhani.

Awali akitoa salamu zake diwani wa kata ya Mafyeko Mhe.Jofre Kamaka    Amewapongeza vijana waliofanikiwa kuhitimu mafunzo ya mgambo na kuwataka wakayafanyie kazi yale yote waliyojifunza na kuibadilisha jamii  kwa mambo mazuri  ikiwa ni pamoja kuonyesha  uzalendo kwa nchi yao na kuisaidia jamii pale inapowahitaji..

Mafunzo ya mgambo yalianza 3/7/2023 na kuhitimishwa leo 11/11/2023 ambapo jumla ya vijana 177 kutoka katika kijiji cha Bitimanyanga na Mafyeko   ambapo  wanaume 144 na wanawake 30 wamehitimu Mafunzo hayo ambapo masomo mbalimbali yamewasilishwa kwa washiriki wa mafunzo hayo ili kuwajengea uwezo wa kukabiliana na Changamoto zozote zinazoweza kujitokeza katika jamii na Taifa kwa ujumla wake

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka akisalimiana na viongozi waliojitokeza kumpokea wakati wa hafla ya ufungaji wa mafunzo ya Jeshi l akiba (Mgambo) leo katika viwanja vya mpira wa Miguu Bitimanyanga

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S ,ayeka akikagua vijana wahitimu wa mafunzo ya jesho la Akiba (Mgambo) katika viwanja vya Mpira wa miguu Bitimanyanga

Askari wa jeshi la akiba (Mgambo) wakitoa salamu kwa Mgeni rasmi wakati wa Hafla za ufungaji wa Mafunzo ya Jeshi hilo katika viwanja vya mpira wa Miguu Bitimanyanga

Askari wa jeshi la akiba (Mgambo) pamoja na wananchi waliojitokeza kwenye hafla ya ufungaji wa Mafunzo ya jeshi la akiba Bitimanyanga wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Chunya akitoa hotuba katika Hafla hiyo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.