• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA "WAPENI SIKU SABA WAFANYE USAFI, BAADA YA HAPO KAMATENI SHERIA ICHUKE MKONDO WAKE”

Imewekwa: November 26th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka amewaasa wananchi wa wilaya ya Chunya kuzingatia suala la usafi katika maeneo yao huku wakijua  Chunya ni ya wananchi wenyewe na amewaagiza viongozi wa kata kutumia sheria ndogo za Halmashauri ili kuwachukulia hatua wale watu wanaokiuka suala la usafi katika mazingira yao kwani waweza kusababisha magonjwa ukizingatia msimu tunaouendea ni msimu wa Mvua

Ametoa wito huo mwishoni mwa juma wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Ifumbo katika Mkutano wa hadhara baada ya kukamilika kwa ziara ya kamati ya usalama wilaya pamoja na wataalamu mbalimbali kukagua shamba lenge mgogoro kwa watu wa familia moja na kulipatia ufumbuzi sauala hilo

“Suala la usafi mlisimamie. Sheria ndogo ndogo za Halmashaurin zipo zinazoeleza adhabu mbalimbali kwa watu wanaokiuka taratibu zetu, zitumieni, msisubiri msukumwe. Sasa hivi tunaenda kwenye msimu wa Mvua tutapata kipindupindu na nyiniyi mnakumbuka hapa tumehangaika na kichocho, sasa ili tusiendelee kuhangaika na Magonjwa haya tena tafadhari zingatieni suala la usafi na mimi niwaombe kila mtu ajisimamie mweyewe kwenye kaya yake maana mji huu ni wa kwenu. Mimi natoa maagizo mtendaji wa kata mtendaji wa kijiji wapeni siku saba kila mtu afanye usafi kwenye maeneo yake na yeyote atakaye kiuka kamateni waleteni Chunya ili sheria ichukue mkondo wake”

Awali akitoa salamu za wananchi wa kata ya Ifumbo kwa Mkuu wa wilaya ya Chunya Diwani wa kata hiyo Mh. Weston S. Mpyila  ameishukuru serikali kwa ujumla wake kwa namna inavyowajali wananchi wa ifumbo kwa kuendelea kutoa fedha ili kujenga miradi mbalimbali yenye manufaa kwa wananchi ikiwepo sekta ya Afya, Sekta ya Barabara, sekta ya Elimu, sekta ya Maji na maeneo mengine

“Sasa hivi tuna zahanati Luparmeket na imekamilika na inatoa huduma, wananchi wanawapongeza sana serikali kwa ujenzi huo Mhe Dc kitua cha afya kimeanza kujengwa toka 2016 lakini bado hakijakamilika, Milioni 77 zinahitajika kukamilika Lakini na wewe mhe Dc unaweza kulisemea jambo hilo ili kituo hicho kiweze kukamilika lakini pia Tukupongeze sana kwenye eneo la miundombinu wananchi wanashukuru kwa ujenzi wa barabara ya Kiwanja mpaka hapa ifumbo lakini tunaomba eneo la kilometa 1 lililobakia basi Mungu akiwajalia pia palekebishwe”

Ziara hiyo ya Mkuu wa wilaya ya Chunya ilihusisha wataalamu toka sekta ya madini ambapo Ndugu Laurent Mayalla ambaye ni afisa madini Mkazi wilaya ya Chunya amewaahidi wananchi wa kata ya Ifumbo kufika katani hapo kutoa elimu ya Madini ili wananchi wengi zaidi nao washiriki kwenye mchakato wa uchimbaji na uchakataji wa madini

 “Nashukuru kwa fursa hii madini ni maisha na utajiri, Serikali ya awamu ya sita inatawaka wananchi mshiriki kwenye sekta hiyo na nimemsikia Mhe Diwani kwamba kuna wananchi wanataka kushiriki huko hivyo niwaahidi jumatano kwenye ofisi ya kata wenye kutaka kushiriki kwenye mambo ya madini tukutane pale tujadiliane ili tuoine namna gani mtashiriki ipasavyo.

Diwani wa kata ya Ifumbo Mh. Weston S. Mpyila akitoa salamu za wananchi wa Ifumbo mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya wakati wa mkutano wa Hadhara na wananchi wake

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa Hadhara wakiwa tayari kumsikiliza Mkuu wa wilaya ya Chunya alipofika Ifumbo kuzungumza na wananchi wa Ifumbo

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka aliyenyoosha mkono akioneshwa mipaka ya Shamba lenye mgogoro balipofanya ziara katika kata ya Ifumbo ili kutatua mgogoro huo

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S. Mayeka (Mwenye shati la Blue na yuko katika aliyeinua mkono) akizungumza na wananchi wenye mgogoro wa Shamba ambao ni kaka na Mdogo wake wa kike

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.