• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA “UDUMAVU NI UZEMBE WA WAZAZI/WALEZI”

Imewekwa: July 5th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka amewataka wazazi na walezi wa watoto wilayani Chunya kuhakikisha wanashirikiana kwa pamoja ili kuwapatia watoto lishe bora itakayowasaidia kukua vizuri na hata kuwa na uwezo mzuri wa akili darasani jambo litakalosaidia kupata Taifa lenye watu imara hapo Mbeleni

Mhe Mayeka ametoa Kauli hiyo jana Julai 4, 2023 ambapo alikuwa Mgeni Rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya lishe na Afya ya kijiji ambayo huadhinishwa kila roba ya mwaka ambapo jana maadhimisho hayo yamefanyika kiwilaya katika kijiji cha Isangawana kilichopo kata ya Isangawana

“Ukizembea kwenye Mambo ya Lishe lazima uone tofauti ya Makuzi kati ya Mtoto wako na mtoto wa jirani yako na wala usianze kutafuta mchawi, ni uzembe wenu baba na Mama wa mtoto maana MUNGU amegawa vyakula vya makundi yote katika kila eneo, hivyo kukosa lishe bora kwa mtoto wako ni suala la uzembe tu na kupuuzia mnapopewa Elimu na wataalamu wa lishe” alisema Mhe Mayeka.

Aidha Mkuu wa wilaya ya Chunya amekemea imani potofu zinazotokana na baadhi ya watu wakiwepo baadhi ya viongozi wa dini kuhusu afya zao huku akiwataka kutumia akili zao wenyewe au panapobidi wapate ushauri kutoka sehemu sahihi

“Ukikuta mafundisho yana kukataza kwenda hospitali kimbia eneo hilo maana sio salama na sisi serikali tunachukua hatua kwa watumishi wa namna hiyo na hata sasa kuna mtumishi (Mchungaji) mmoja tunamshikilia kwa kueneza imani potofu pia Niwapongeze wanaume wote mliojitokeza katika Mafunzo kuhusu lishe yatakayotolewa na wataalamu wa Afya na niwape pole na kuwashangaa wanaume wote wanaofikiri suala la lishe ni la mama peke yake bila kujua mtoto akipata udumavu familia nzima itakosa utulivu wa uzalishaji mali na hata wakati mwingine mtoto kuwa na uelewa mdogo awapo shuleni hivyo zingatieni miongozo ya lishe kama mnavyoelekezwa na watalamu wa lishe” Alisema Mhe. Mayeka

Afisa Maendeleo ya Jamii Vincent Msolla kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya amewataka wananchi kupeleka watoto kliniki ili wapate ushauri sahihi kutoka kwa watalamu wa Afya kuliko kusibiri tatizo litokee kwa mtoto ndipo wajitokeze Jambo linalofanya watumie muda mrefu kumuhudia mtoto huyo na hata serikali pia kutumia fedha nyingi

“Mahudhuria ya watoto kliniki sio mazuri kabisa na hilo sio jambo jema kwa mtoto mwenyewe na hata kwa familia hivyo tuhasishane kupeleka watoto kiliniki” Alisema Msolla

Awali akitoa salamu mbele ya Mgeni rasmi Mganga Mkuu wa wilaya Daktari Darison Andrew amesema bado wananchi hawajitokezi ipasavyo kuleta watoto wao kupata Chanjo kwani Halmashauri ya wilaya ya Chunya ina watoto  elfu sabini (58,411) lakini ni watoto elfu arobaini na moja tu ( 41,000) wanaofika katika vituo vya afya kupata Chanjo

“Tuna watoto wengi hawapati chanjo, Tunatamani wazazi wa kiume wawe sehehumu kuleta watoto wao kupata Chanjo, tunao watoto elfu hamsini na nane lakini ni watoto elfu arobaini na moja tu wanaopata Chanjo”

Siku ya Afya na Lishe huadhimishwa kila baada ya miezi mitatu ambapo kila kijiji kinatakiwa kuadhimisha siku hiyo na Mkuu wa wilaya katika kila hafla ya siku za lishe kwa vijiji mara nyingi hufika na kuzungumza na wananchi kuhusu umuhimu wa lishe kama alivyofanya leo katika Kijiji cha Isnagawana.

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S. Mayeka (Aliyeshika kikombe chekundu) akipata ufafanuzi hatua mbalimbali zilizotumika kutengeneza uji wa lishe katika siku ya Afya na Lishe kijiji cha Isangawana

Baadhi ya Wananchi Wa kijiji cha Isangawana wakiendelea na Darasa la uandaaji wa Uji wa Lishe katika siku ya Afya na Lishe

Mhudumu wa Afya ngazi ya jamii Ndugu Emily Kifubasi akielezea makundi mbalimbali ya vyakula kwa Mkuu wa wilaya akiongozana na viongazi mbalimbali wa wilaya ya Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.