• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA “SERIKALI WILAYANI CHUNYA ITAENDELA KUWAUNGA MKONO VIONGOZI WA DINI KATIKA SHUGHULI ZAO ZA KILA SIKU”

Imewekwa: April 20th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka Saimon Mayeka amewahakikishia wananchi wa wilaya ya Chunya kuwa serikali itaendela kushirikiana na viongozi wote wa dini bila kujali utofauti wa dini hizo katika kuhakikisha maendeleo ya wananchi waliopo wilayani Chunya Yanafikiwa huku akiwakumbusha kwamba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina Dini lakini serikali inatambua kwamba wananchi wake wana dini

Ametoa kauli hiyo mapema jana wakati wa futari ya pamoja iliyoandaliwa na ofisi ya Mkuu wa wilaya, Mkurugenzi, Mbunge pamoja na marafiki wengine iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) jioni ya tarehe 19/04/2023 ambapo waislamu pamoja na watu mbalimbali walialikwa kushiriki

“Madhehebu ya dini yamekuwa na mchango Mkubwa sana katika maendeleo ya nchi hii hasa katika maeneo ya maadili. Sisi kama serikali hatusiti kushirikiana na nyinyi hasa kwa wilaya ya chunya, kwani wananchi wa Chunya wanahitaji kupata mafundisho yaliyomema na kuenenda kama mwenyezi MUNGU alivyowatarajia”

Mkuu wa wilaya pia amewataka wananchi wote wilayani Chunya kwa kushirikiana na viongozi wa dini kuhakikisha tunarudi kwenye maadili yetu ya awali huku akiwasisitiza utandawazi ni mzuri kama ukitumiwa vizuri na masema tusipoangalia katika eneo hili la malezi iko siku tutapata viongozi wasio na maadili

“watoto zamani walikuwa watoto wa jamii nzima lakini hapa katikati mambo yameharibika hivyo turudi kwenye maadili yetu ya zamani, tusipoangalia haitashangaza kukapata viongozi wasio kuwa na maadili” alisema Mayeka

Akizungumza Mbele ya Mkuu wa wilaya Kaimu sheikh Mkuu wa wilaya ya Chunya, Sheikh Abdallah Mush amemshukuru Mkuu wa wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Chunya pamoja na Mbunge wa Jimbo la Lupa kwa namna walivyoona ni vema kuandaa futari kwaajili ya waumini wa dini ya Kiislamu pamoja na wananchi wote waliojumuika katika futari hiyo ya pamoja

“Namshukuru mwenyeezi MUNGU aliyetujalia kupata futari ya pamoja na ndugu zetu wote waliojumuika katika futari hii ya pamoja, ama hakika nitoe shukrani nyingi kwaniaba ya waislamu wa Chunya, Hatuna cha kukulipa ila mwenyeezi Mungu Atakulipa, Pia amewashukuru viongozi wa dini nyingine waliojumuika katika futari ya pamoja”

Akiwawakilisha waumini wa madhehebu ya dini ya kikristo Mch Lyos K. Mwalyosi ambaye ni mweneykiti wa jukwaa la wakristo wilayani Chunya amesema kwa niaba  ya waumini wa dini ya kikristo wilayani Chunya kwamba wanamuwakilisha vema mkuu wa wilaya na amesema wao wako pamoja naye katika kila hatua ili kuhakikisha wananchi wa wilaya ya Chunya wanapata maendeleo

“Niseme wazi tu mkuu wa wilaya pasina shaka tunakuwakilisha vizuri na tuko pamoja” alisema Mchungaji Mwalyosi

Kaimu Sheikh Mkuu wilaya ya Chunya Sheikh Abdallah Mush Akitoa Shukrani kwa Mkuu wa wilaya, Mkurugenzi , Ofisi ya Mbunge pamoja na Wadau mbalimbali kwa kuandaa futari kwaajili ya waumini wa dini ya Kiislamu pamoja na wananchi wote waliojumuika katika futari hiyo ya pamoja


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.