• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA “POLENI WAKULIMA WA TUMBAKU, …SASA TUKATE BIMA”

Imewekwa: March 10th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka Simon Mayeka amesema namna bora ya kukabiliana na Majanga Mbalimbali katika maisha ya kawaida ya wananchi wilayani Chunya wakiwepo wakulima wa Tumbaku ni kuwa na Bima, Jambo ambalo litasaidia pale yanapotokea majanga yanayoweza kusabisha Mkulima kushindwa kuvuna Mazo yao vizuri

Mhe: Mayeka amesema hayo Jana wakati alipowatembelea wakulima wa zao la Tumbaku walio athiriwa na Mvua ya Mawe iliyonyesha mapema wiki hii ambapo zaidi ya ekari 90 zimeharibiwa katika vyama vya msingi vya Lupatinga tinga na Mtande ambapo karibu kilo laki moja zinakadiriwa kuharibiwa na mvua hiyo

“Kwanza miwapeni pole wakulima wote mliokumbwa na kadhia hii ya Mvua ya Mawe, kweli tumeona ni uharibifu Mkubwa ambao umefanywa namvua hii, Pamoja na uharibifu huu, Ni muhimu sasa wakulima tuanze kufikiria kukata Bima, wakulima hawa waliopata uharibifu huu tungekuwa tunashuhudia sasa wakipata fidia kupia bima zao kuliko hali hii tunayoishuhudia sasa”

Mkuu wa wilaya amewata viongozi wa vyama vya msingi vya tumbaku kuanza kufikiria uwepo wa mfuko wa maafa kwa wakulima wa zao la Tumbaku ili yanapotokea mambo kama haya basi mfuko huo utumike angalau kumsaidi mkulima ambaye amekumbwa na kadhia hiyo, huku akiwata chama kikuu cha Msingi kuchua hiyo kama agenda kuanza kuzungumza kwenye vikao

Pia amewataka viongozi wa vyama vya ushirika kutafuta njia mbadala ya kuwasaidia wakulima waliopata madhara kutokana na mvua ya mawe ili waweze kuwalipa wafanyakazi waliokuwa wamewaajiri kwa msimu huu kwani kwasasa wakulima hao hawana namna tena ya kuwalipa wafanyakazi hao kutokana na mazao ambayo yalikuwa tegemeo lao kuharibiwa na mvua ya mawe.

Kwa Mujibu wa Afisa Kilimo wilaya ya Chunya Ndugu MWINUKA amesema bado wanaendela kufanya tathimini ya uharibifu wa mvua hiyo katika wilaya nzima na pindi itapokuwa imekamilika basi taarifa rasmi itatolewa idadi ya ekari zilizoathirika katika wilaya nzima pamoja na kilo zinazokadiriwa kupotea kutokana na uharibifu huo

Meneja wa bank ya CRDB tawi la Chunya na Afisa uhusiano wa Banki ya Azania tawi la Mbeya waliambatana na Mkuu wa wilaya, wamewasisitiza wakulima kuhakikisha wanakata Bima ili angalau kupata fidia ya uharibifu unaokuwa umejitokeza pale changamoto kama hii inapojitokeza huku wakisisitiza kwamba karibu kila mwaka walimu wamekuwa wakishuhudia uharibifu wa tumbaku kutokana na Mvua ya mawe

Akiwa katika ziara hiyo hiyo Mhe. Mayeka amepitia kukagua maendeleo ya ujenzi wa Sule ya Sekondari ya wasichana Mayeka inayojengwa katika Kata ya Lupatinga Tinga ambapo amehimiza kukamilishwa mapema hatua ya ujenzi iliyopo sasa ili wakaguzi wafike kukagua kiwango cha ujenji huo ukilinganisha na thamani ya fedha zilizotolewa kwaajili ya ujenzi kwa hatua hiyo.

“Mumalize ili tuje kukagua tuone thamani ya mradi kama inalingana na thamani ya fedha iliyotolewa kwani hatuwezi kuleta fedha zingine bila kufanya ukaguzi na kujiridhisha kwamba ujenzi unaoendelea unakidhi viwango stahiki” amesema Mhe Mayake

Mhe. Mayeka pia alitembelea ujenzi wa jengo la abiria katika kituo cha Mabasi Lupa na kuwataka watumiaji wa jengo hilo kutumia kama lilivyokusudiwa na kuwataka wamiliki wa mabasi kutumia kituo hicho tofauti na ilivyosasa ambapo bado kuna baadhi ya mabasi bado yanatumia ujanja ujanja kushusha na kupakia abiria eneo ambalo sio kituo cha mabasi.

Mkuu wa wilaya amehitimisha ziara yake kwa kuzungmza na baadhi ya wanachama wa chama cha ushirika cha Mtande ambapo kwanza amewapa pole kwa uharibifu huo lakini pamoja na kusisitiza suala la bima kwa wakulima pia amehimiza wazazi kuendela kuwasimamia watoto kusoma kwa bidii pamoja na kushirki katika ujenzi wa Taifa huku akisema maendleao ya Taifa la Tanzania ni kwa faida ya wanajamii wenyewe

Ziara hiyo imekuja ikiwa ni siku chache baada ya kuwepo kwa taarifa za uharibifu Mkubwa wa zao la Tumbaku uliotokana na Mvua kubwa ya mawe wilayani humo ambapo wakulima kumi na sita (16) kutoka chama cha ushirika cha Lupatinga tinga na wananchama kumi na tisa (19) kwa Chama cha ushirika Mtande wamepata athari kutokana mvua hiyo huku tathimini ikiendela kwa vyama vingine

Mwenyekiti wa chama Cha Ushirika Mtande, akielezea kiwango cha uharibifu wa Tumbaku mbele ya Mkuu wa wilaya alipotembelea kujionea uharibifu katika zao la Tumbaku kutokana mvua ya mawe

Moja ya Mashamba yaliyopata uharibifu kutokana na Mvua ya mawe

Afisa kilimo wilaya Chunya Ndugu Curthbet Mwinuka na Mwenyekiti wa Chama Cha Ushirika Cha Lupatinga tinga Ndugu Jilala (Mwenye suti nyeusi) walioinama chini wakifafanua Jambo mbele ya Mkuu wa wilaya Chunya alipotembelea kuona  uharibifu wa mvua ya mawe kwa wakulima wa Tumbaku

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.