• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC Mayeka awataka wanachama AMCOS kulipa madeni kuepuka kufilisiwa

Imewekwa: March 11th, 2022

MKUU wa Wilaya ya Chunya, Mayeka Simon Mayeka amewataka waachama wa Lupa AMCOS kulipa madeni wanaodaiwa na wadhamini kwa wakati ili kuepuka adha zinazoweza kuwakuta ikiwemo kufilisiwa.

Mayeka ameyasema hayo alipofanya kikao na Wanachama wa Lupa AMCOS wanaojishughulisha na ulimaji wa zao la tumbaku katika ofisi za AMCOS hiyo.

“Hatujaja hapa kuzuia watu wasilipe madeni, isije ikawa watu wanajua Mkuu wa Wilaya amekuja kurusha taulo kwamba sasa hawatalipa, tumekuja hapa kuangalia taratibu zilizotumika ni sahihi, wanaodaiwa wanadaiwa kiasi hicho na huyo aliyekuja kama dalali yupo kihalali?” Alisema Mh. Mayeka.

“Kwa taratibu za kiushirika nyinyi wenyewe mnajua namna mnavyoishi na mnavyoshirikiana, kwa hiyo nyie ndio mnaweza kuendeleza Lupa AMCOS ni nyinyi wenyewe akaiuwa AMCOS yenu.” Alisisitiza Mh. Mayeka.

Aidha, Mheshimiwa Mayeka amewaasa wanachama hao kufuata utaratibu, kwani Serikali haipo tayari kukaa kimya na kuacha mambo yakiharibika.

“Sisi kama Serikali hatuwezi kukaa kimya tukaacha mambo yaende ndivyo sivyo, lazima kila kitu kifuate utaratibu, lakini sUala la kulipa hilo linaeleweka, kwa hiyo mtu asije akakaa akafikiri Mkuu wa Wilaya amekuja kuzuia watu wasilipe.” Alitahadharisha Mh. Mayeka.

Mayeka ameutaka uongozi wa AMCOS hiyo kuhakiki madeni yote upya na kuhakikisha wadaiwa wote wanashirikishwa kwenye uhakiki wa madeni hayo na kisha zoezi la kulipa liendelee.

“Mwende mkahakiki madeni yote, na yanapohakikiwa watu wa ushirika wawepo, mtu mmoja mmoja aende kuhakiki deni lake na Afisa Ushirika ayathibitishe hayo madeni.

Pia Mkuu wa Wilaya alitumia nafasi hiyo kusitisha zoezi la kufilisiwa na kukamatwa kwa wanachama wanaodaiwa ili kila uongozi na wanachama kuhakiki upya madeni yao.

“Mimi nadhani hili zoezi lililokuwa liendelee la kuja kufilisiwa na kukamatwa lisitishwe kwanza, mhakiki madeni yenu kila mtu aridhike kwamba hili ni deni langu halafu sasa tukae mnalilipaje”. Alisema Mayeka  

Naye Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Mbeya Bw. Richard Zengo alisema, vyama vya ushirika vinaendeshwa kwa mujibu wa masharti na masharti hayo yanawekwa na wanaushirika wenyewe.

 

Aidha Zengo aliongeza kwa kusema kuwa, kuna kila sababu ya uongozi kuhakikisha unafanya marejeo mapya ya madeni ilikuwepo na uhalisia wa madeni na wadhamini wathibitishe kuwepo na madeni hayo.

Kwa upande wa Afisa Tarafa wa Tarafa ya Kipembawe Ndg. Kassim Kirondomara alieleza sababu mbalimbali zinazopelekea wanachama kuwa na madeni ndani ya AMCOS hiyo, akiitaja moja ya sababu kubwa ni wanachama kutorosha tumbaku na kwenda kuuza sehemu nyingine, na wengine kuuza pembejeo wanazopewa kwa ajili ya kilimo cha tumbaku.

“Kimsingi Mkuu wa Wilaya wapo watu ambao wametorosha tumbaku na wapo ambao wameuza pembejeo na kupelekea kulaza madeni kwa makusudi.”  Alisema Ndg. Kirondomara

Wanachama wa LUPA AMCOS wakiwa kwenye kikao na Mkuu wa Wilaya ya Chunya kilichofanyika katika Ukumbi wa Lupa AMCOS

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mh Mayeka Simon Mayeka wa katikati akiwa na Das wa wilaya ya Chunya Mh Anaklet Michombero pamoja na mwenyekiti wa Lupa AMCOS kwenye kikao kilicho wakutanisha Wanachama na Viongozi mbalimbali wa Wilaya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.