• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA AMEWATAKA MAAFISA USAFIRISHAJI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA MASUALA YA USALAMA CHUNYA.

Imewekwa: November 24th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka amewataka maafisa usafirishaji (waendesha Badoboda, maguta pamoja na bajaji) na wananchi waliojitokeza kuwa wazalendo wenye kuipenda wilaya yao ya Chunya na Nchi kwa ujumla wake kuhakikisha wanashiriki kikamilisha katika masuala ya usalama

Ametoa kauli hiyo mapema jana wakati akikabidhi zawadi kwa timu  ya Yanga A iliyoibuka mshindia wakati wa kuhitimisha mashindano ya Mayeka Usalama Cup yalitamaatika jana katika uwanja wa mpira wa miguu Sabasaba ambapo timu ya Yanga A iliwafunga timu ya Simba A gori moja kipindi cha kwanza gori lililoduma dakika zote tisini na kuifanya Yanga kuwa Mabingwa wa Mashindano hayo

“Michezo ni urafiki, michezo ni upendo, Mimi ninaamini mtatusaidia pia kwenye  uslama wa wilaya yetu tunatamani kuwa na vijana ambao ni  wazalendo mnatamani kuiona Chunya inaendelea Pamoja na mashindano leo kuisha tutapanga na viongozi wenu twende  Hospitali ya wilaya, mkoa ili tukaone wenzetu ambao walipata madhira kupitia kazi hii ya usafirishaji na hii itatusaidia na sisi kuendelea kuchukua tahadhari”

Mhe Mayeka aliwapongeza timu ya Yanga kwa ushindi walioupata huku akisema mashindano haya kwa mwaka huu yamefanikiwa kwa kiwango kikubwa lakini mwaka ujao mashindano hayo yataratibiwa kwa namna nyingine bora zaidi hivyo amewataka vijana hao kujiandaa na kuendeleza upendo kupitia michezo

“Niwapongeze Yanga kwa kushinda leo,, Mimi kwakweli ni kama mzazi mimi yeyote angeshinda kati yenu nafurahi ingawa Mimi ni ni samba, Hiki kilichofabnyika hapa tumefanya yanga na samba lakini lengo ni kupata wachezaji baadaye tutakuwa na timu moja na ndomaana niliwambia msikamiane sana ili msiumizane kwani baadaye mtakuwa timu moja na mashindano haya tulitaka kuona wachezaji na tumewaona kwa mimi nawapongeza sana”

Awali akitoa salamu la Jeshi la Polisi wilaya ya Chunya Mkuu wa polisi wilya ya Chunya SSP Nestory M John amemshukuru Mkuu wa wilaya ya Chunya kwa kuandaa mashindano ya Mayeka usalama Cup yenye lengo la kuhimiza maafisa usafirishaji kuzingatia usalama wao kwanza na baadaye usalama wa abiria wake huku akihimiza kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya watu wenye nia ovu kwa wilaya ya Chunya  pamoja na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pindi tu wanapokuwa na mashaka na abiria.

“Sisi kama upande wa jeshi la polisi tumefurahi na tumerizishwa na namna mlivyojitokeza na mlivyoshiriki.Ujumbe umefika na tumejikumbusha kuhusu Bima, usalama wetu kwanza, namna tunavyobeba abiria wetu tuwe makini na abaria hao maana wengine ni waharibifu na sisi wenye tuzingatie alama za barabarani tusizidishe spidi”

Mashindano ya Mayeka Usalama Cup yametamatika jana kwa michezo miwili ambapo mchezo wa Mapema ulihusisha timu za Simba B ikicheza na Yanga B kusaka mshindi wa Tatu na Timu ya Simba B iliibuka kidedea kwa gori moja na Baadaye Mchezo wa Fainali ambapo Yanga A ilicheza na Simba A matokeo ya gori moja yakaipatia Ushindi timu ya Yanga.

Wachezaji wa timu ya Yanga A wakiwa wameketi chini na nyuso za furaha baada ya kupata ushindi dhidi ya Simba A katika mashindano ya Mayeka Usalama Cup

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S.Mayeka akimkabidhi kombe Kapteni wa timu ya Yanga A  iliyopata ushindi katika mashindano ya Mayeka Usalama Cup katika Uwanja wa mpira wa miguu  Saba saba 

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S.Mayeka akimkabidhi kombe Kiongozi wa timu ya Yanga A  kiasi cha Tshs 100,000/= katika mashindano ya Mayeka Usalama Cup katika Uwanja wa mpira wa miguu  Saba saba .

Timu ya Simba Awakiwa wameketi chini  kwaajili ya shamlashamla  zilizokuwa zikiendelea katika uwanja wa Mpira wa miguu Saba saba baada ya mchezo kumalizika 

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.