• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC. “MARUFUKU VIKAO KUFANYIKA PORINI, VIKAO VYOTE VIFANYIKE HADHARANI NA KWA MUJIBU WA SHERIA”

Imewekwa: April 16th, 2023

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilayani chunya chini ya mwenyekiti wake ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe, Mayeka Simon Mayeka amewataka wananchi wa wilaya ya chunya kuhakikisha wanafuata kanuni, taratibu na sheria za nchi katika maeneo yao kwani bila Amani maeneo yetu hayatatawalika na hata shughuli za kiuchumi zitashindwa kufanyika

Amesema hayo mwisho wa juma wakati akiongoza kamati hiyo kukagua miradi ya maendeleo inayofanyika katika kijiji cha sipa kata ya Kambikatoto na baadaye kuongea na wananchi wa kijiji hicho ambapo amesema kijiji hicho kilikuwa na mafanikio makubwa sana jambo ambalo lilikuwa linapelekea kuwa na vigezo vya kuwa kata lakini wasipozuia mambo ya hovyo, yanayofanywa kinyume na sheria za nchi wanaweza kusabibisha kuporomoka kabisa

“Kuna kikundi kinaitwa wazee sijui wazee wa mila wao wanaona wako juu ya sheria na wanataka wao ndo wafanye maamuzi na nasikia kuna vikao vinafanyika porini, sasa ni marufuku kufanya vikao porini, vikao vyote vya kijiji vina utaratibu wake, Vikao vya kijiji vifanyike kwa utaratibu na vifanyike hadharani uongozi ujue vikao hivyo akiwepo mweshimiwa Diwani”

Aidha Mhe Mayeka amewataka viongozi wa serikali maeneo mbalimbali wilayani Chunya kuhakikisha mazao yanauzwa na kununuliwa kwa uataratibu uliowekwa na serikali lakini pia vipimo vinavyotumika viwe vipimo halali, na amewakumbusha kwamba Makamu wa Rais alishatoa mwongozo kwamba Lumbesa hazikubaliki na mazao yauzwe na kununuliwa kwa kilo.

“Mtendaji vipimo hivi havikubaliki kabisa, vinamuumiza mkulima, Viongozi wetu walishaagiza kazi yetu ni kutekeleza. Mazao yapimwe kwa mizani na sio kuuzwa kwa vipimo mbalimbali kama debe na vinginevyo”

Amewataka wananchi wa Chunya kuheshimu mpango wa matumizi bora ya ardhi wa mwaka 2007 ambao umeweka wazi maeneo ya makazi, maeneo ya malisho, maeneo ya hifadhi, maeneo ya mapitio ya wanyama pamoja na maeneo mengine mengi kulingana na matumizi husika, kwani kuendelea kukaa katika maeneo hayo ni kujiandalia hasara yako ya baadaye

 “Mimi nawambia inawezekana mwaka jana ulikaa, mwaka huu unakaa hatujui mambo ya kesho, lakini muda utafika utatoka katika maeneo hayo, Tukishasema hili eneo la shoroba (Mapitio ya wanyama) basi ondokeni, tukisema eneo hili ni hifadhi au eneo hili sio la makazi ni la malisho ya mifugo basi msijenge nyumba za kudumu hapo kwani kuendelea kuishi na kujenga makazi ya kudumu katika maeneo hayo ni kujitakia hasara ya baadaye kwani muda utafika ambao utaondolewa kwa lazima”

Mkutano huo wa hadhara ulitanguliwa na kikao cha ndani ambapo kamati hiyo ikiongozwa na Mkuu wa wilaya ambapo Mambo mbalimbali yalijadiliwa na baadaye kamati hiyo kupitia mwenyekiti wake iliwataka viongozi hao kuhakikisha wanafanya kazi kwa kushirikiana, kwa uwazi na kwa umoja bila kujali kabila, dini na hata eneo ambalo mtu ametoka

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.