• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC CHUNYA “TUSHIRIKIANE KUFAIFANYA CHUNYA KUWA SEHEMU SALAMA KWA BIASHARA NA UWEKEZAJI”.

Imewekwa: June 4th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Biashara wilayani Chunya amewata Watumishi wa Umma na wale wa Taasisi binasfi pamoja na Wafanyabiashara kushirikiana kuifanya wilaya ya Chunya kuwa Eneo salama la Biashara na uwekezaji ili kuwavutie wafanyabiashara wengi na hata wawekezaji kuja kuwekeza Chunya

Akizungumza kwenye kikao cha Barza la Biashara kilichoketi tarehe 2/6/2023 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) amesema upande mmoja ukitambua nafasi ya upande mwingine itasaidia kufanikisha biashara ya upande mmoja na kufanya hivyo lengo la serikali ya awamu ya sita ya kuletea ajira kwa wananchi wake, kuwainua wafanya Biashara na kuwatelea huduma bora wananchi wake linatimia kwa urahisi

“Wafanyakazi wa Serikali shirikianeni na wafanyabiashara kuhakikisha wanafanikiwa katika kazi zao kwani wako wananchi na wanachunya kwa ujumla wamejiajiri kupitia biashara na wameajiri watu wengine wengi hivyo mnapotaka kuwafungia biashara zao mfikilie watu wengine wanaofaidika kupitia biashara husika” amesema Mayeka

Aidha Mhe Mayeka ameongeza kusema kuwa kwa kipindi ambacho atakuwepo wilayani Chunya atahakikisha wafanya kazi wa serikali wanakuwa rafiki kwa wafanya baishara jambo ambalo litaongeza idadi ya wafanyabaishara, ambao kupitia biashara zao serikali itakusanya kodi ambazo zitatumika maeneo mbalimbali ya huduma kwa wananchi wa Chunya

“Kwa Muda ambao Mungu atanijalia kuwepo Chunya, Natamani kuona wafanyabiashara na Taasisi zote zinazowahusu wafanyabiashara kuwa na uhusiano mzuri Jambo ambalo litasaidia kuwainua wafanyabiashara wengi ambapo baadaye Makusanyo ya kodi yataongezekana lakini pia watu wengi watapata ajira nyingi na hatimaye maisha yao kubadilika kutokana na vipato hivyo”

Kupitia kikao hicho wafanyabiashara kwa nyakati tofauti wametoa kero wanazokumbana nazo wawapo katika biashara zao na kero kubwa ni watumishi wa Halmashauri kuchelewesha kutoa huduma, wakati mwingine kutokuwepo ofisini kipindi ambacho wafanyabiashara wanapohitaji huduma mbalimbali

Josia M Nandi (Mmiliki wa nyumba za starehe) yeye alisema “Kufanyike utaratibu mzuri wa namna ya ulipaji wa kodi kwa Vinywaji nje ya hapo tutaonekana wafanyabiashara wa huduma hizo hatutaki kulipa kodi, hivyo ni muhimu suala hilo litazamwe vizuri”

Lukas Malangalila yaye alijikita katika changamoto ya vizuizi vya mazao alisema “Shughuli zinazojitokeza kwenye vizuizi (Mageti) mbalimbali ni ngumu na zina usumbufu mkubwa kwa wafanya biashara. Nikuombe ukae vizuri na watu wa halmashauri ili warekebishe hilo”

Akijibu moja ya hoja walioitoa wajumbe wa Kikao hicho waliotaka kujua changamoto inayokwamisha ujenzi wa kituo cha Mabasi wilayani Chunya, Afisa rasilimali watu ndugu John Maholani akimuwakilisha Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya chunya alisema

“Tayari taratibu za awali za ujenzi wa kituo hicho cha mabasi zimeanza kwani tayari mkandarasi mshauri wa kazi amepatikana ambaye ni Chuo Kikuu Cha Sayansi na Teknolojia (MUST) na tayari wamewasilisha mchoro wa kwanza na sasa hivi karibu watakuja kuleta mchoro wa mwisho na taratibu nyingine ziendelee hivyo ni hivi karibu ujenzi wa kituo hicho cha Mabasi utaanza” alisema Maholani

Afisa Biashara wilaya ya Chunya Bw. Rodrick Mwakisole alipata nafasi ya kutoa elimu kwa ufupi kuhusu Mfumo mpya wa kukusanya mapayo (TAUS) kwamba nimfumo rahisi na rafiki kwa wafanyabiashara kwani wanaweza kufanya malipo yoyote kutoka eneo walilopo bila kufika katika ofisi za Halmashauri

“Mfumo umetengenezwa na watanzania wenyewe jambo ambalo litarahisisha kufanya marekebisho pale itakapotakiwa kufanya hivyo na mfumo huu ni rahisi kwakuwa taratibu zote za kuomba leseni na hata kulipia tozo mbalimba mteje anaweza kufanya bila kufika ofisi za halmashauri jambo ambalo litapunguza gharaza za usafiri kwa mteja” amesema Mwakisole

Kikao cha Baraza la Biashara huketiwa mara mbili kwa mwaka jambo ambalo husaidia kutatua Changamoto mbalimbali zinazowakumba wafanyabaishara, Wakuu wa idara wa halmashauri ya wilaya ya Chunya na Jeshi la Polisi walipata nafasi ya kujibia hoja zilizotolewa na wafanyabiashara na hoja nyingine zinazohitaji mchakato kupata majibu zinaendelea kushughulikiwa ili katika kikao kijacho zitatolewa ufafanuzi wa hatua zilizo chukuliwa

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka Akizungumza jambo katika kikao cha Baraza la Biashara


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.