• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA “WATENDEENI HAKI WAKULIMA ILI WAPATE HAKI YAO”

Imewekwa: April 30th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mrakibu mwandamizi wa Uhamiaji Mhe Mbarak Alhaji Batenga amewataka vyama vya Ushirika, Makampuni yanayonunua Tumbaku na watu wote wanaohusika kwenye mchakato wa ununuzi wa Tumbaku kuhakikisha wanatenda haki kwa wakulima kwakuhakikisha mizani zinazotumika kupima Tumbaku kuthibitishwa na mamlaka husika ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima.

Ametoa maelekezo hayo Jana tarehe 29/4/2024 wakati akizungumza na wakulima waliojitokeza kuuza Tumbaku kwenye Chama Cha Msingi Mtanila ikiwa ni Chama cha kwanza katika Mkoa wa Kitumbaku Chunya kuanza kuuza Tumbaku huku Kampuni ya Premium Active wakisema malipo kwa wakulima ambao Tumbaku yao imenunuliwa siku hiyo yatalipwa ndani ya siku 14 kwa mujibu wa Sheria.

“Niombe mizani inayotumika kupima mizigo ya Tumbaku ya wakulima iwe imethibitishwa na mamlaka husika ili mkulima aweze kupata haki yake kadiri ya kujituma kwake ili tusije tukaingia kwenye migogoro na wakulima kwani imeshatokea maeneo mengine mkulima anaamini ana kilo kadhaa na mizani inatoa jibu tofauti” Alisema Mhe Batenga

Aidha Mhe Batenga ameonya wakulima kujiingiza kwenye utoroshaji wa Tumbaku jambo ambalo linaweza kupelekea kukamatwa na kufunguliwa Mashitaka kwa Mujibu wa Sheria na Miongozo ya kilimo cha zao la Tumbaku hivyo wahakikishe kila mmoja anauza Tumbaku yake kwenye maeneo waliyokubaliana kuuza Tumbaku.

“Niwaombe wakulima, utoroshaji wa Tumbaku utahatarisha kupotea kwa haki yako maana tutakukamata na kukuweka ndani kwa mujibu wa Sheria, taratibu na miongozo ya zao la Tumbaku, Naomba msitoroshwe Tumbaku iwe kutoka Chama kimoja kwenda chama Kingine lakini pia kutorosha kwenda nje ya wilaya, hivyo kila mtu ahakikishe anatenda haki katika nafasi yake” Aliongeza Mhe Batenga

Fredy Essau Meneja wa kampuni ya ununuzi wa Tumbaku ya Premium Mkoa wa kitumbaku Chunya amesema wao kama Kampuni wanajivunia kuwa Kampuni ya kwanza kuanza ununuzi wa Tumbaku kwani lengo lao kama Kampuni ni kuwapa fursa wakulima lakini pia kwa kuanza mapema kununua Tumbaku itapelekea wakulima wanaofanya kazi na Kampuni ya Premium watapata fedha Mapema kuliko wengine

“Kimsingi najivunia sana kuwa Kampuni nunuzi kwa Chama Cha Msingi Mtanila na kama ulivyoona wakulima wamehamasika na niwapongeze wakulima wa Mtanila na kwa dalili hii maana yake wakulima watapata pesa kwa wakati na wataanza mapema maandalizi ya kilimo kwa Msimu ujao” Alisema Fredy

Kwa niaba ya wakulima wa Chama cha Msingi cha Ushirika Mtanila Nuru Martini Kambaulaya amesema hali ya soko ni nzuri na Mitumba yao wataendelea kupeleka kwenye chama chao cha Msingi maana Bei ni nzuri tofauti na ilivyokuwa hapo awali hivyo wakulima wote tupeleke Tumbaku zetu kwenye vyama vya Msingi

Mkuu wa wilaya ya Chunya alifika kwenye Chama Cha Msingi Mtanila kuona zoezi la ununuzi wa Tumbaku linavyoenda na baadaye aliendelea na ziara yake ya kukagua miundombinu ya Barabara zitakazotumiwa na wakulima kusafirisha Tumbaku kutoka eneo moja kwenda kwenye Maghala ya Tumbaku tayari kwa kuuza Tumbaku hiyo kwa Makampuni waliyoingia nayo Mkataba.

Mkuu wa wilaya ya Chunya akikagua mwenendo wa soko la Tumbaku Chama cha Msingi cha Ushirika cha Mtanila Jana alipotembelea zoezi la ununuzi lililoanza Jana (Aliye vaa shati la Blue bahari ni Bw Faustine Mtweve Katibu wa wadau wa Tumbaku Mkoa wa Kitumbaku Chunya, Kushoto kwa Mkuu wa wilaya ni Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Chunya

Meneja wa kampuni ya ununuzi wa Tumbaku ya Premium Mkoa wa kitumbaku Chunya Bw Fredy Essau akizungumza Mbele ya Mkuu wa wilaya na wanachama wa Chama Cha Ushirika cha Mtanila Jana wakati Mkuu wa wilaya alipotembelea kuona mwenendo wa soko

Wanachama wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Mtanila wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Chunya alipotembelea kuona mwenendo wa soko la Tumbaku jana

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.