• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA, WALIOVAMIA ENEO LA MRADI WA KILIMO CHA SOYA KIJIJI CHA MASIANO CHUNYA WAONDOKE

Imewekwa: September 20th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mheshimiwa Mubarak Alhaji Batenga amewataka wananchi wa kijiji cha Masiano wilayani Chunya waliovamia eneo la mradi la kilimo cha Soya kuondoka kwenye eneo hilo mara moja ili kupisha utekelezaji wa mradi wa kilimo cha zao la Soya utakaotekelezwa na serikali hivi punde kupitia udhamini wa benki ya dunia.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara kijiji cha Masiano, Septemba 19, 2024, Mheshimiwa Batenga amesema wananchi wote waliovamia eneo la mradi wa kilimo cha  Soya katika kijiji cha Masiano kilichopo Wilayani Chunya kuondoka .

“Waliovamia eneo la mradi wanapaswa kuondoka na Serikali itawapa kila kaya heka 50 pamoja na hati miliki katika eneo lililopo msitu wa kijiji ili kupisha utekelezaji wa mradi huu mkubwa wa kilimo cha Soya”, amesema Batenga.

Mhe. Batenga aliongeza kuwa, wananchi wa Masiaono na Mapogolo ndio wanufaika wa kwanza mara baada ya mradi wa kilimo cha Soya kuanza kutekelezwa huku akiwataka vijana kujipanga vyema kushiriki kwenye mradi huo ili kujiongezea kipato na kujikwamua kiuchumi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Batenga amesema kupitia mpango bora wa matumizi ya ardhi, Serikali imetenga eneo lenye ekari 2594 lililopo kijiji cha Mapogolo na Shoga kwaajili ya wafugaji wa Kijiji cha Masiano na Mapogolo ambapo Serikali itapanda majani kwaajili ya malisho, kuchimba mabwawa ya maji upatikanaji na kujenga majosho ya mifugo.

“Wananchi wa kijiji cha Masiano munapaswa kuheshimu mpango bora wa matumizi ya ardhi ambao mumeupitisha kupitia mikutano yenu ya kijiji na mpango huu mumeuhuisha kulingana na mahitaji yaliyopo sasa, kuwa na matumizi bora ya ardhi kutaondoa migogoro ya ardhi pamoja na serikali kuweza kuwaletea wananchi maendeleo” amesema DC Batenga.

Kwa upande wa wananchi wa kijiji cha Masiano walimueleza Mhe. Batenga changamoto zilizopo kwenye kijiji chao ikiwemo ubovu wa barabara, kutokukamilika kwa madarasa ya shule na upungufu wa madawati, ukosefu wa nishati ya umeme, upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na kutokuwepo kwa zahanati kwenye kijiji hicho ambapo serikali imeahidi mwaka huu wa fedha kuzipatia ufumbuzi wa haraka.

Mhe. Batenga yupo kwenye ziara yake ya kawaida ya kukutana na wananchi kwa kila kijiji kusikiliza kero zao na kutatua. Wakati wa mkutano huu Mhe. Batenga amewakikishia wananchi kuwa kazi ya Serikali ni kutengeneza mazingira wezeshi kwa wananchi wake kujipatia kipato na kujikwamua kiuchumi, mradi wa kilimo cha Soya utakapoanza, Serikali itapeleka huduma zote muhimu za kijamii ikiwemo kuchonga barabara, huduma ya umeme na maji, kujenga zahanati, kujenga shule na huduma nyingine zote za kijamii.

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Batenga akizungumza na wananchi wa kitongoji  cha Masiano kilichopo kata ya Chokaa

Baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Masiano waliojitokeza kwenye Mkutano wa Hadhara wa Mkuu wa wilaya ya Chunya ili kupeleka Kero zao zipatiwe ufumbuzi

Moja kati ya wananchi wengi waliojitokeza kutoa kero za kijiji chao Mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Batenga wakati wa Mkutano wa Hadhara wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Batenga akisikiliza na kuandika kero za wananchi wakati wa Mkutano wa Hadhara kwenye kitongoji cha Masiano kilichopo kijiji cha Mapogoro kata ya Chokaa

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.