• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA “USIPOKULA LISHE KAMA TIBA UTAISHIA KUNYWA DAWA KAMA LISHE”.

Imewekwa: October 31st, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaj Batenga ametoa rai kwa wananchi na kinamama wajawazito kuhakikisha  wanazingatia  ulaji wa vyakula ambavyo vimezingatia misingi ya lishe ili kuboresha afya ya mwili na akili lakini pia kujiepusha na maradhi mbalimbali yanayotokana na ulaji mbovu kama vile udumavu na utapiamlo  kwani  wasipokula lishe bora  basi wataishia kula dawa kama lishe.

Kauli hiyo ameitoa leo Octoba 30/2024 wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Lishe Kitaifa ambapo kiwilaya maadhimisho hayo yamefanyika kata ya Matundasi katika viwanja vya Shule ya Msingi Matundasi.

“Tunasema tunazingatia lishe lakini ni muhimu kwa kina mama wajawazito kuzingatia mnakula nini  mnapokuwa na mimba lakini pia  hata ukijifungua kuzingatia unakula nini ili yule mtoto naye anaponyonya aweze kunyonya mlo kamili kupitia maziwa  na hiyo ndio lishe vinginevyo watoto hao itakuwa shida huko tunako kwenda bila kujua kwamba tatizo lilianzia wapi  kumbe tatizo lilianza na wazazi wenyewe pale ambapo hatukuwapa lishe ya kutosha pindi wakiwa tumboni mpaka wanakuja kuzaliwa”.

Mhe.Batenga pia amezungumzuia suala la uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024  huku akiwaagiza  watoto wote kuwahimiza wazazi wao na ndugu zao kwenda kupiga kura siku hiyo kwani ni haki yao ya kidemokrasia ya kuwachagua viongozi wanaowataka.

“Tarehe 27 Novemba ikifika itakuwa siku ya mapunziko ninyi wanafunzi hamtakuja Shule  hivyo nawatuma watoto wote siku hiyo muwakumbusha baba, mama dada kaka  na wengine wenye miaka 18 na zaidi wakapige kura nyinyi  mtabaki nyumbani  siku hiyo  mkilinda nyumba ili wazazi waende wakapige kura na kuwachagua viongozi wao wanao wataka” alisema Batenga

Naye kaimu Mganga mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Chunya ndugu  Ryoba Kebasho amesema kuwa suala la Lishe linaanza kabla mtoto hajazaliwa  yaani pale ambapo wazazi wanapanga mipango ya kupata mototo ili kumjenga mtoto atakaepatikana kuanzia akiwa tumboni mwa mama yake.

Vilevile, Daktari Kebasho amesisitiza wakinamama wajawazito kupatiwa elimu kuhusu lishe na afya ili kujenga kizazi cha kesho kilicho bora na kujiepusha na madhara yanayoweza kujitokeza kwa kukosa lishe.

“Mama kabla hajapata ujauzito anatakiwa kula lishe bora ili kuanza maandalizi ya kujenga mtoto atakaepatikana baadae  kuanzia akiwa tumboni na baada ya kuzaliwa ikiwa ni pamoja na kutumia virutubisho vinavyotolewa katika vituo vya afya kwani mtoto asipopatiwa lishe bora hawezi kukuwa vizuri kimwili na kiakili “alisema Ryoba.

Maadhimisho ya siku ya Lishe kitaifa hufanyika tarehe 31 Oktoba ambapo kwa mwaka huu Wilaya ya Chunya yamefanyika katika kata ya Matundasi huku yakiwa yamepambwa  na burudani mbalimbali zilizobebe jumbe kuhusu lishe chini ya kauli mbiu isemayo Mchongo ni Afya yako, Zingatia unachokula.

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mbaraka Alhaji Batenga akizungumzia umuhimu wa Lishe wakati wa maadhimisho ya siku ya Lishe Kitaifa ambapo wilayani Chunya Maadhimisho hayo yamefanyika katika  Viwanja vya Shule ya Msingi Matundasi kata ya Matundasi .

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitalli ya Wilaya  ndugu Ryoba Kashebo akielezea namna ambavyo elimu ya Lishe imekuwa ikitolewa katika jamii wakati wa Maadhimishao ya siku ya Lishe  viwanja vya Shule ya Msingi Matundasi kata ya Matundasi

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Matundasi wakitoa elimu kuhusu lishe kwa njia ya burudani wakati wa maadhimisho ya siku ya Lishe yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya msingi Matundasi.

Wnanafunzi na wazazi waliojitokeza wakati wa Maadhimisho ya siku ya lishe yaliyoodhimishwa katika viwanja vya Shule ya msingi Matundasi wilayani Chunya


 

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.