• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA: NDANI YA MWEZI MMOJA MKUTANO MKUU UFANYIKE

Imewekwa: February 7th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Mhe Mbaraka Alhaji Batenga ameagiza uongozi wa Kipembawe Saccos kuitisha Mkutano mkuu ndani ya mwezi mmoja ili kuhakikisha wananchama wote wanashiriki kikamilifu katika maamuzi yoyote watakayoona yanafaa kwa manufaa ya Kipembawe Saccos

Agizo hilo limetolewa jana tarehe 6/2/2024 katika Mkutano Mkuu maalumu ulioketi ukumbi wa Alfani Lupa ambapo lengo la mkutano huo ilikuwa kusomewa taarifa ya mwenendo wa Kipembawe Saccos baada ya wajumbe kutokuwa na taarifa yoyote kutoka kwa uongozi kwani ni Zaidi ya miaka miwili mkutano mkuu haujaitishwa

“Afisa Ushirika simamia hili ndani ya mwezi mmoja kuanzia leo tarehe 6/2/2024 mpaka tarehe 6/3/2024 mkutano mkuu uitishwe na taarifa za mkutano huo zitolewe wiki mbili kabla ya mkutano na mkutano huo lazima uhudhuliwe na Zaidi ya asilimia 75 ya wanachama. Katika taarifa zenu mtakazo wasilishwa kwa wanachama wenu lazima ziwe wazi na zijumuishe taarifa ya watu mnao wadai, dhamana zao zikoje, sifa za kukopeshwa zilikuwaje na mambo mengine, maafisa ushirika wasaidieni viongozi kuandaa taarifa ambazo zitakidhi matakwa ya wananchama” Alisema Mhe Batenga

Aidha Mhe Batenga aliwataka viongozi na wanachama wa Kipembawe Saccos kuhakikisha wanakuwa Mabalozi wazuri wa Saccos yao ili watu wengine walio nje ya Saccos hiyo wavutike kuwa wanachama kwani uhai wa Saccos yoyote ile ni uwepo wa idadi kubwa ya wanachama na kama wanachama wanapopungua ni dalili ya kufa kwa Saccos

“Ni kazi kwetu sote kuhakikisha watu walio nje ya Saccos yetu waipende Saccos na wajiunge ili uhai wa Saccos uendelee maana uhai wa Saccos yoyote ile ni uwepo wa Idadi kubwa ya wanachama ambao wanajiunga kila mwaka au kwa kipindi ambacho Saccos wanaweza kupanga kupokea wanachama wapya” Alisema Batenga

Mjumbe wa Bodi ya Kipembawe Saccos ndugu Biniford Andrew Matola kwa Niaba ya viongozi wenzake wa bodi alikili wazi kukiuka kanuni na taratibu zinazoongoza Saccos yao kwa kushindwa kuitisha mkutano mkuu kwa karibu miaka miwili huku akisema hawakuwa na lengo lolote baya juu ya Saccos hiyo bali changamoto mbalimbali ndizo zilikuwa kikwazo cha wao kushindwa kuitisha mikutano hiyo

Awali akitoa taarifa kwa wajumbe wa Mkutano huo maalumu katibu wa Kipembawe Saccos ndugu Aman Daniel Hussein lengo la Saccos hiyo ilikuwa ni kuwana na Zaidi ya wanachama 800 lakini kwa sasa ina wanachama 105 akitaja sababu iliyopelekea kuwa na idadi hiyo ya wanachama ni changamoto zilizojitokeza za kuyumba uzalishaji wa zao la Tumbaku jambo lililopelekea hata wanachama kuyumba kiuchumi


Ndugu Aman Daniel Hussein Katibu wa Kipembawe Saccos akisoma taarifa Mbelaya ya Mkuu wa wilaya na wajumbe walio Hudhuria kikao hucho Maalumu

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.