• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA YAUNGA MKONO KWA VITENDO MAAMUZI YA MKUTANO MKUU MKUU WA CCM.

Imewekwa: January 25th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaj Batenga amesema kuwa serikali ya  Wilaya ya Chunya inaungana na wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Chunya   kuunga mkono maamuzi yaliyofanywa na Mkutano Mkuu Maalum wa Chama  wa kupitisha jina la Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Taifa  kuwa mgombea wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika 2025, kwasababu ya utekeleza wa ilani ya CCM kwa vitendo ikihusisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kutatua kero za Wananchi.

Kauli hiyo ameitoa tarehe 24/01/2025 wakati akitoa salam za serikali mbele ya katibu mwenezi wa CCM Mkoa wa Mbeya  katika hafla ya kumpongeza Dkt Samia Suluhu Hassani  kwa kupitishwa na Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM kuwa Mgombea wa kiti cha Urais na viongozi wengine wa kitaifa .

“Tunazo sababu kama wananchi wa Chunya za kuunga mkono uamuzi wa mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, sisi kama serikali tulipewa ilani tukaitekeleza, Chama  cha Mapinduzi ndio kimetupa ilani tukaitekeleza chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan, tunayo mambo mengi yamemefanyika  katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na uwepo wa umeme katika vijiji na utekelezaji unaenda mpaka kwenye vitongoji, ujenzi wa stendi mpya ya mabasi ,ujenzi wa uwanja wa kisasa na miradi mingine ya maendeleo  na Wananchi wa Chunya wanaelewa”amesema Mhe. Batenga.

Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Mbeya Ndugu Frank Uwagire akizungumza na wanachama wa Chama cha Mapinduzi na Wanachunya amepongeza uongozi wa serikali ya Chunya kwa utekelezaji mzuri wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa uwanja wamichezo wa kisasa, ujenzi wa stendi ya mabasi ya kisasa na miradi mingine ambayo ni majibu ya utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi.

“Nitoe pongezi kwa serikali  yaWilaya ya   Chunya kwa kazi kubwa na   nzuri mnayoifanya ya kusimamia utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambayo leo inatufanya tunatembea vifua mbele ikiwemo  ujenzi wa stendi mpya ya kisasa, ujenzi wa uwanja wa kisasa , soko la dhahabu la kisasa , na leo ukija Chunya unaikuta dunia yote iko Chunya kwasababu ya dhahabu , lakini pia makusanyo makubwa ya mapato mnapeleka kwenye miradi ya maendeleo,  Chama Cha mapinduzi Mkoa wa Mbeya  tunawapongeza sana “amesema Uwagire.

Aidha makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Umoja wa Vijana CCM Wilaya(UVCCM), Umoja wa wanawake Tanzania(UWT) , Jumuiya ya Wazazi Wilaya, Baraza la wazee Wilaya na Wanachunya  wametoa matamko yao yakuunga Mkono maamuzi yaliyofanywa na Halmashauri kuu na Mkutano Mkuu wa CCM wa kumpitisha mgombea urais na  Viongozi wengine  kwa ngazi ya kitaifa kutokana na kazi nzuri zilizofanywa na  Dkt Samia pamoja na Viongozi wengine .

Hafla ya pongezi kwa Viongozi walioteuliwa kwa nafasi mbalimbali za kitaifa kupitia Chama cha Mapinduzi imehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa serikali , Makundi mbalimbali   ya Uongozi ndani ya CCM, na wananchi   kupitia maamuzi ya Mkutano Mkuu  wa Chama cha Mapinduzi  kilichoketi Tarehe 18 na 19 Januari 2025 katika Ukumbi  wa Jakaya  Kikwete uliopo makao makuu ya nchi Dodoma.

Katibu mwenezi wa CCM Mkoa wa Mbeya ndugu Frank Uhagile akizungumza na wanachama wa chama cha mapinduzi na Wanachunya waliokusanyika katika hafla ya kumpongeza dkt Samia suluhu Hassan kwa kupishwa na Mkutano Mkuu kuwa mgombea wa kiti cha urais .

Wanachama wa chama cha mapinduzi waliokusanyika katika hafla ya kumpongeza Dkt Samia Suluhu Hassan iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ( Sapanjo).

Wanachama wa chama cha Mapinduzi wakiwa kwenye maandamano kuelekea ukumi wa mikutano wa halmashauri ya Wilaya ya Chunya ( Sapanjo) kwaajili ya hafla ya kumpongeza Dkt Samia Suluhu Hassan.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.