• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA YASHIRIKI MAONESHO YA UTALII “KARIBU KUSINI”

Imewekwa: September 26th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikiwa ni moja na sehemu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeshiriki maonesho ya utalii yenye jina “KARIBU KUSINI”yanayofanyika Mkoani Iringa yenye lengo la Kukuza utalii mikoa ya Nyanda za Juu kusini kwani mikoa hiyo ina vivutio vingi ambavyo havipatikani maeneo mengine


Halmashauri ya wilaya ya Chunya imewakilishwa na Mkurugenzi mtendaji wilaya ya Chunya,Afisa Utalii wilaya ya Chunya Ndugu Petro Haule pamoja na afisa Biashara wa wilaya ya Chunya ndugu Sebastiana Mapinga wamesema maonesho hayo ni muhimu kwanza kubadilishana uzoefu na mbinu mpya zinazohusu utalii na hata kufungua fursa za kibiashara kupitia Utalii kwani Wilaya ya Chunya ina vivutio mbalimbali kama vile Bwawa la Viboko Zingwa matundasi, Kambi ya wapigania uhuru, Mlima Mwene na vingine ambavyo vinaweza kutumika kuvutia fursa za kibiashara


Akizungumza mbele ya wageni mbalimbali waliotembelea banda la maonesho la Mkoa wa Mbeya afisa utalii wa wilaya ya Chunya ndugu Petro Haule amesema Maonesho hayo yanamaana kubwa sana kwa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwani kupitia maonesho hayo watu Mbalimbali watakuja Chunya kuona vivutio hivyo na pia kuja kuwekeza katika fursa Mbalimbali za kibiashara


“Kupitia maonesho hayo sisi kama wilaya ya Chunya tumejifunza mambo mengi muhimu yanayohusu namna sahihi ya kutunza na kuhifadhi vivutio vyetu na hata miundombinu ya kuvifikia vivutio hivyo lakini sisi tuliowakilisha wilaya ya Chunya tumeona namna wenzetu walivyotumia fursa ya utalii kufungua biashara mbalimbali hivyo Chunya tunaenda kulifanyika kazi jambo hilo”


Wageni Mbalimbali wametembelea Banda la Mkoa wa Mbeya wakiwepo viongozi wa wizara, Mikoa na wilaya lakini viongozi na wadau wa Taasisi mbalimbali za serikali na taasisi zisizo za Kiserikali ambapo kwa asilimia kubwa wameonesha utayari wa kutembelea mkoa wa Mbeya na Fulsa zzinazopatikana kwenye sekta ya Madini wilayani Chunya imekuwa ni kivutio kikubwa kwa viongozi mbalimbali na wananchi waliotembelea Banda la Mkoa wa Mbeya


Maonesho ya Utalii yaliyopewa jina “KARIBU KUSINI” yanafanyika Mkoani Iringa, Manispaa ya Iringa eneo la Kihesa-Kilolo barabara ya kuelekea Dodoma, Maonesho hayo leo yamefikia siku ya nne na yanataraji kudumu kwa siku tano ambapo kilele cha Maonesho hayo itakuwa tarehe 27/9/2023

Afisa utalii Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Petro Haule akifafanua jambo mbele ya Viongozi Mbalimbali waliotembelea kuona vivutia vya utalii vilivyopo Mkoa wa Mbeya, Alye vaa shart la Kitenge ni Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Mbarali Missana Kalela Kwangula akisaini kitabu katika Banda la utalii Mkoa wa Mbeya wakati wa Maonesho ya KARIBU KUSINI

Afisa Utalii wilaya ya Chunya Ndugu Petro Haule akishirikiana na Afisa utalii wilaya ya Rungwe Ndugu Numwagile Bughali wakifafanua vivutio vya utalii vinavyopatikana katika Mkoa wa Mbeya kwa Ujumla wake wakati wa maonesho ya utalii yanayoenda kwa jina la KARIBU KUSINI yanayoendelea mkoani Iringa

Baadhi ya Maafisa kutoka wilaya ya Chunya na Rungwe wakiwa juu ya moja ya kivutio cha Utalii (Daraja la MUNGU) ambapo maji ya Mto Ruaha mdogo yanapita chini lakini Juu kuna mawe. wa kwanza Kutoka Kulia ni Joshua Sengo (Afisa Habari wilaya ya Chunya) anayefuata ni Petro Haule (Afisa Utalii kutoka wilaya ya Chunya), Noah Kibona (Afisa Habari wilaya ya Rungwe na wa Mwisho ni Numwaghile Bugali (Afisa utalii wilaya ya Rungwe)

Baadhi ya washiriki wa Maonesho ya Utalii "KARIBU KUSINI" wakiwa kwenye picha ya Pamoja kwenye Kabuli la Mashujaa (LIGALU) Lugalo ya sasa eneo ambalo watanzania kupitia Chifu Mkwawa waliwashinda Wajerumani wakati wa harakati za Kupinga Ukoloni


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.