• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA YA MFANO, WATU WATAKUJA KUIGA

Imewekwa: July 5th, 2023

Mkuu wa wilay ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka amesema endapo wananchi wa wilaya ya Chunya wataamua vema kama serikali inavyotaka basi wilaya ya Chunya itakuwa ni eneo la watu kuja kujifunza namna bora ya ufugaji wenye tija ambao utapelekea mifugo inayopatikana wilayani Chunya kuwavutia wanunuzi wengi jambo litakalo inua vipato vya wananchi kwa ujumla.

Mhe Mayeka ametoa kauli hiyo Jana July 4, 2023 alipokuwa anazungumza na wafugaji, wakulima kutoka kata ya Kambikatokto na Mafyeko pamoja na wataalamu kutoka Ngazi za vijiji, kata na halmashauri kilichoketi katika viwanja vya shule ya Msingi Bitimanyanga chenye lengo la kueleza mpanga wa serikali wa kuwatambua wafugaji ili wagawiwe maeneo ya malisho kulingana na idadi ya mifugo wanayomiliki.

“Kwa idadi ya mifugo tuliyonayo laki mbili na kitu, idadi ya watu kulingana na sensa ya 2022 ambapo Chunya ina watu laki tatu na arobaini hivi na eneo letu la mraba ambalo ni zaidi ya hekta elfu kumi na tatu tunaweza kuishi bila shida na mifugo yetu bila migogoro yoyote kati ya wafugaji na wakulima, hivyo ni muhimu tutambue wafugaji wetu wako wangapi, wana idadi gani ya mifugo ndipo tuwagawie maeneo yaliyotengwa kwa malisho ambapo serikali itapeleka mahitaji yote yanayohitajika kwa ufugaji bora”. Alisema Mhe. Mayeka

Mhe Mayeka amewataka watu wote waliovamia maeneo ya malisho yaliyotengwa kwa mujibu wa Mpango wa Matumizi bora ya Ardhi wa mwaka 2006 kuanza kuondoka kwani serikali itapita kuhakiki maeneo hayo hivi karibuni na kuanza kuyatumia kama mpango wa matumizi bora ya ardhi unavyoelekeza na kwasasa maeneo hayo takwimu zinaonesha kuvamiwa kwa kiasi kikubwa

“Wakulima wote waliovamia eneo la malisho kwa mujibu wa Mpango wa Matumizi bora ya ardhi wa mwaka 2006 wajiandae kupisha kwani muda si mrefu maeneo hayo yatakuwa Ranchi za mifugo na wafugaji ambao wamejenga eneo la malisho kupunguziwa eneo hilo kulingana na idadi ya mifugo aliyonayo” alisema Mhe. Mayeka.

Afisa kilimo wilaya ya Chunya Ndugu, Cuthberth Mwinuka ametaja changamoto zinazokabili eneo la malisho ambapo amesema uvamizi wa maeneo ya marisho kutoka kwa wakulima lakini wananchi kujenga kwenye maeneo ya malisho pamoja na ongezeko la mifugo kwenye baadhi ya maeneo. Kuingizwa mifugo kihole hupelekea ugumu kupata idadi kamili ya mifugo

“Eneo la malisho linapungua sana jambo linalopeleka migogoro ya wakulima na wafugaji, changamoto kubwa ni maeneo ya malisho kuvamiwa na shughuli nyingine ikiwepo kulima, maeneo ya malisho kuwa na mifugo mingi kulinganisha na eneo jambo linalosababishwa na uingizaji hole kutoka nje ya wilaya na hata wakati mwingine ndani ya wilaya” alisema Mwinuka.

Julius Nguvumali, Abdalah Marijani na Bize Kefasi Kilongozi kwa niaba ya wajumbe wengine wa kikao hicho kwanza wameishukuru serikali kuja na mpango huo ambao utafanya wakulima kuwa huru katika shughuli zao na wafugaji kufuga kwa uhuru tofauti na ilivyo sasa, Pamoja na shukrani hizo wametamani kujua ni lini hasa zoezi hilo litanza huku wakitamani ikiwezekana iwe mapema sana na kila hoja waliyouliza imejibiwa palepale na Mkuu wa wilaya.

Kikao hiki kimekuja ikiwa ni mwendelezo wa kikao kilichowakutanisha wafugaji kutoka Tarafa ya kiwanja kilichoketi mapema wiki iliyopita ambapo lengo kubwa ni kuwafikia wafugaji wote ili kuwasiaidia waweze kufuga kwa tija tofauti na ilivyo sasa.

Mkuu wa wilaya Mhe. Mayeka akizungumza na wafugaji katika viwanja vya Shule ya msingi Biti manyanga

Afisa kilimo na mifugo wa Wilaya Ndugu Cuthbert Mwinuka akitoa taarifa ya mifugo mbele ya Mkuu wa wilaya na wajumbe wengine wa kikao

Ndugu Abdallah Marijani kutoka Kambi katoto akichangia katika kikao cha wafugaji kilichoongozwa na Mkuu wa wilaya

Ndugu Julius Nguvumali akichangia katika kikao cha wafugaji 

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.