• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CCM YATOA MAAGIZO KWA UONGOZI WA WILAYA YA CHUNYA

Imewekwa: February 5th, 2024

Halmashauri ya wilaya ya Chunya imeagizwa kutumia fedha kutoka vifungu ambavyo havina shida ya mifumo ili kutekeleza miradi mbalimbali ikiwepo ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa shule ya Msingi Makongolosi na vyumba vitatu vya Madarasa shule ya msingi Chunya mjini ili kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira mazuri ya kusomea ili fedha husika zitakapopatikana zinarejeshwa eneo lake

Akizungumza jana tarehe 4/2/2024 Viwanja vya shule ya msingi Bwawani katika Maadhimisho ya kutimiza miaka 47 ya Chama cha Mapinduzi kwa niaba ya chama mkoa wa Mbeya Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Mbeya Ngugu Ndele Mwaselela amesema ni kazi ya chama kusikiliza kero za wananchi

“Mkurugenzi tumie fedha kutoka vifungu ambavyo havina changamoto kuanza kutekeleza ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa shule hii ya Makongolosi na ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Chunya Mjini, viongozi wa kamati za ujenzi fikeni ofisi ya Mkurugenzi jumatatu ili muanze kufuatilia vifaa na taratibu nyingine na madarasa yaanze kujengwa” Alisema Mwaselela

Mwaselela amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwaajili ya utekelezaji wa  miradi  mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya Elimu, sekta ya Afya ,Barabara na miradi mingine ambayo iimetekelezwa na inaendelea kutekelezwa Wilayani chunya na Tanzania kwa ujumla.

‘’Naomba niwape salamu za Mhe Rais ameleta hapa Chunya miradi mikubwa sana ya Elimu na tumetembelea na kuona Shule ya Msingi Amani imejengwa kama Chuo kikuu leo  watoto wetu wanakwenda shuleni  wanasoma na  kukaa katika mazingira safi na salama, Pia vituo vya afya na taa za barabarani tunaona leo miaka 47 ya CCM tunaona mafanikio makubwa”. Alisema mhe, Mwaselela

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  ndugu John Maholani amekiri kuyapokea maagizo yote yaliyotolewa na kuahidi kuyatekeleza kwa kuyatafutia ufumbuzi ikiwa ni pamoja na  kupeleka lori la kubebe taka katika mamlaka ya Mji mdogo Makongolosi  pamoja na kero zingine.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Noel chiwanga amesema kuwa chama cha Mapinduzi ndicho kilichopewa jukumu la kusikiliza na kutatua kero za wananchi hivyo wao kama viongozi wako tayari kupokea maelekezo yote kutoka kwa mgeni rasmi lakini pia kusikiliza na kuzitolea majibu kero mbalimbali za Wananchi.

“Chama cha Mapinduzi ndicho chenye Jukum la kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi yawezekana huduma zinazotolewa zina weza kuwa na malalamiko sasi sisi ndio wenye Nyumba lazima tusikilize kero zenu na na tuone namna ya kuzitatu”. alisema Chiwanga

Aidha Mhe. Sailon Mbalawata wa kata ya Bwawani na Mhe,Kasimu Haule  wameeleza mafaanikio Makubwa   na miradi  na mbalimali iliyotekelezwa katika kata hizo Ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule za kisasa , kituo cha Afya , miundombinu ya Barabara na miradi mingine ambayo imetatuliwaa na kupuza kero mbalimbali za waanchi ikiwa ni pamoja na kupunguza msingamano wa wanafunzi darasani pamoja na kuboresha huduma za Afya.

Salvatory Mwandambile  , Tumaini Mwamakula, Ibrahim Semsokwe na wengine wemeeleza changamoto mbalimbali ikiwemo kero ya Barabara  ,uchakavu wa miundombinu soko la Makonolosi, Uhaba wa maji wakati wa kiangazi na umeme  ambapo kero hizo zimeweza kupewa ufumbuzi na majibu papo hapokupitia Wataalam wa Halmashauri ya WIlaya ya Chunya pamoja na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi.

Maadhimisho yaho yameudhuriwa na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi katika Ngazi mbalimbali , Wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Wananchi  Maadhimisho hayo yameenda sambamba na Kutembelea na kukagua miradi mbalimnali ikiwa ni pamoja na mradi wa  ujenzi wa ofisi ya Chama hicho , shule ya Msingi Amani na Kituo cha Afya cha Makongolosi.

Ndele Mwaselela akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi pamoja na Wananchi wakati alipowasili katika viwanja vya Shule ya Msingi Makongolosiyaliko fanyikia   Maadhimisho ya miaka 47 ya CCM .

Afisa tarafa wa tarafa ya Kiwanja Ndugu Erick Nyoni akimwakilisha Mkuu wa WIlaya ya Chunyu akitoa  neno la shukrani kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Miradi mikubwa ya Maendeleo ilitokelezwa Wilayani Chunya.

Mhe.  kassim Haule  diwani wa kata ya Makongolosi akitoa mufafanuzi juu ya kero  ya barabara ya Mwaoga  katika Mkutano wa kusikiliza kero wakati wa maadhimisho ya ya sherehe ya miaka 47 ya chama  cha Mapinduzi

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Dr Andrew Darison akitoa maelezo kuhusu ukamilishwaji wa kituo cha Afya Makongolosi kwa Mgeni rasmi  ndugu Ndele Mwaselela wakati  wa maadhimisho ya miaka 47 ya Chama cha Mapinduzi alipotembelea na kukagua kituo hicho.

Salvatory  Mwandambile katibu wa chama cha waendesha Boda boda Mamlaka ya Mji mdogo Makongolosi  akitoa kero zinazowakabili kwa Mgeni rasmi ndugu Ndele Mwaselela wakati wa sherehe za Maadhimisho ya miaka 47 ya Chama cha Mapinduzi


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.