• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC. CHUNYA; ANZENI KUTUMIA BENKI NA MITANDAO YA SIMU KUPOKEA FEDHA ZA TASAF ILI KUWA NA USALAMA ZAIDI

Imewekwa: May 17th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga amewataka walengwa wote wa TASAF kuhakikisha wanapokea malipo ya Fedha kupitia kwenye akaunti zao za Benki au mitandao ya simu kwa Mujibu wa maelekezo wanayopatiwa na wawezeshaji wa TASAF ili kuhakikisha usalama wa fedha hizo unazingatiwa ndipo tuendelee kufanya vizuri katika kuzisimamia fedha hizo kama Serikali ya awamu ya Sita inavyoelekeza.

Ametoa kauli hiyo jana tarehe 16/05/2024 katika viwanja vya ofisi ya kata ya Matwiga iliyopo kwenye kijiji cha Isangawana, wakati akizungumza na walengwa wa TASAF kutoka kijiji cha Isangawana ikiwa ni sehemu ya kuhimiza matumizi sahihi ya fedha hizo kwa walengwa.

“Wale ambao hawajaanza kupokea fedha zao kupitia kwenye akaunti au mitandao ya simu, niwaombe tuanze kuchukua fedha wote kupitia kwenye akaunti au mitandao ya simu, asiwepo mtu yeyote anayepokea fedha mkononi mimi kama Mkuu wa wilaya naagiza kupitia kikao hiki asipewe, maana kuweka fedha kwenye akaunti au kwenye simu ndio utaratibu mzuri wa kulinda fedha zenu maana fedha hazitapotea na wala hazitaibiwa” Alisema Mhe Batenga

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa Shughuli za TASAF wilaya ya Chunya Mratibu wa TASAF wilaya ya Chunya Ndugu David Ngowo ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwakuipatia fedhe zaidi ya Bilioni 1.7 (1,701,577,599.00/=) kwaajili ya kuwasaidia walengwa wa TASAF jambo linaloendelea kuimarisha ustawi wa wa wananchi wa wilaya ya Chunya kwa Ujumla wake.

“Fedha za TASAF wilaya ya Chunya zimetolewa katika awamu kumi na saba (17) kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2023 mpaka May 2024. Huku Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikipokea Fedha kiasi cha shilingi Bilioni moja, milioni mia saba na moja, laki tano na sabini na sana mia tano tisini na tisa. Kwa niaba ya uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa fedha hizo” Alisema Ngowo

Kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Chunya, Mkuu wa Divisheni ya Kilimo ndugu Cutherth Mwinuka amemwambia Mkuu wa wilaya ya Chunya kwamba Halmashauri ya wilaya ya Chunya Inashika nafasi ya Tatu Kitaifa kwa matumizi ya mifumo ya Kibenki katika utekelezaji wa Shughuli za TASAF hivyo fedha za TASAF ziko salama kwa kiwango kikubwa

“Kwa wilaya ya Chunya asilimia tisini na nane ya wanufaika (98%) wanatumia mfumo wa kielektroniki kupokea malipo, Hivyo katika Taifa hili la Tanzania wilaya ya Chunya ni ya tatu kwa walengwa wa TASAF kupokea fedha zao kupitia simu na mitandao ya Kifedha”

Pamoja na Shughuli nyingene zilizofanyika kwenye Mkutano huo, Mkuu wa wilaya ya Chunya alikagua kaya za walenga wawili kwa niaba ya walengwa wengine wa TASAF ili kuona na kujiridhisha juu ya maelekezo, mafunzo na miongozo ya matumizi ya Fedha za TASAF kwa walengwa

Katibu Tawala wa wilaya ya Chunya Ndugu Anakleth Michombero akizungumza kwenye Mkutano wa Mkuu wa wilaya na walengwa wa TASAF Isangawana

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Cuthbeth Mwinuka akizungumza wakati wa Mkutano wa Mkuu wa wilaya na Walengwa wa TASAF uliofanyika Jana katika Kijiji cha Isangawana

Mratibu wa TASAF Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu David Ngowo akizungumza Mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya pamoja na walengwa wa TASAF Jana kwenye Mkutano na walengwa wa TASAF

Diwani wa Kata ya Matwiga Mhe Mh. Frank E. Malambughi akiwasalimia walengwa wa TASAF kutoka Kijiji cha Isangawana wakati Mkuu wa wilaya ya Chunya alipowatembea na kuzungumza nao

Mkuu wa wilaya ya Chunya (Kushoto aliyenyoosha mikono akizungumza) akizungumzana na Bi Happy Mbaruk mnufaika wa TASAF kutoka Kijiji cha Isangawana alipokuwa anawatembelea wanufaika hao Nyumbani kwao

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.